< Warumi 15 >

1 Sisi tulio na nguvu, hatuna budi kuchukuliana na kushindwa kwa wale walio dhaifu wala si kujipendeza nafsi zetu wenyewe.
Linu kwetu tukolete tu swanela ku kutusa bufokoli bu ba fokola, imi ni kusa litabisa tubene.
2 Kila mmoja wetu inampasa kumpendeza jirani yake kwa mambo mema, ili kumjenga katika imani.
Tusiye zumwi ni zumwi kwetu atabise ya bambene naye kwezina zi lotu, ili kuti a zakwe naye.
3 Kwa maana hata Kristo hakujipendeza mwenyewe, bali kama ilivyoandikwa: “Matukano yao wale wanaokutukana wewe yalinipata mimi.”
Mi ni heiba Kirisite kena abali tabisi mwine. Nihakubulyo, ibena bo bulyo sina mukuñolelwe, “Matapa abo ba bamituki aba wili hangu.”
4 Kwa maana kila kitu kilichoandikwa zamani, kiliandikwa kutufundisha, ili kwamba kwa saburi na faraja tunayopata katika Maandiko tuwe na tumaini.
Kakuti zonse zi bañoletwe ku masule ziba ñolwa che intaelo zetu, ili kuti che inkulonde ni che insusuwezo ya mañolo tube ni insepo.
5 Mungu atoaye saburi na faraja, awajalie ninyi roho ya umoja miongoni mwenu mnapomfuata Kristo Yesu,
Linu Ireeza we inkulonde ni insusuwezo a mihe mizezo iswana kuzwilila kwa Jesu Kirisite.
6 ili kwa moyo mmoja mpate kumtukuza Mungu aliye Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo.
A pange bulyo ili kuti cha muzezo umwina ni mulomo umwina mutembe Ireeza ni Isi wa Simwine wetu Jesu Kirisite.
7 Karibishaneni ninyi kwa ninyi kama Kristo alivyowakaribisha ninyi ili kumletea Mungu utukufu.
Kuzwaho mutambule zumwi ni zumwi sina Kirisite mwa ba mitambwili, chentumbo ya Ireeza.
8 Kwa maana nawaambia kwamba, Kristo amekuwa mtumishi kwa wale waliotahiriwa ili kuonyesha kweli ya Mungu na kuthibitisha zile ahadi walizopewa baba zetu wa zamani,
Chingi ni wamba bulyo Kirisite abapangwa buhikana bwa mupato kwi neku lyo buniti bwa Ireeza, cha kwi zuzikiza insepiso zi bahewa ku bazazi,
9 pia ili watu wa Mataifa wamtukuze Mungu kwa rehema zake. Kama ilivyoandikwa: “Kwa hiyo nitakutukuza katikati ya watu wa Mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.”
mi ku Basikunze ni kuha ikanya kwa Ireeza cha chishemo chakwe. Kwina bulyo sina mu kuñolelwe, “Kuzwaho kanihe ikanya mukati ka Basikunze ni kuzimba intumbo che zina lyako.”
10 Tena yasema, “Enyi watu wa Mataifa, furahini pamoja na watu wa Mungu.”
Hape iti, “Musange, inwe mu Basikunze, ni bantu bakwe.”
11 Tena, “Msifuni Bwana, ninyi watu wa Mataifa wote, na kumwimbia sifa, enyi watu wote.”
Mi hape, “Mutembe Simwine, mubose Basikunze; musiye bantu bonse ba mutembe.”
12 Tena Isaya anasema, “Shina la Yese litachipuka, yeye atakayeinuka ili kutawala juu ya mataifa. Watu wa Mataifa watamtumaini.”
Hape, Isaya uti, “Kakube ni muhisi wa Jese, mi iye yesa buke ku yendisa hewulu li Basikunze. Basikunze ka babe ni insepo mwali.”
13 Mungu wa tumaini awajaze ninyi furaha yote na amani katika kumwamini, ili mpate kujawa na tumaini tele kwa nguvu ya Roho Mtakatifu.
Linu Ireeza we insepo amizuze kusanga ni inkozo yonse cha ku zumina, ili kuti mube ni ku kwatinsana munsepo, cha ziho zo Luhuho Lujolola.
14 Ndugu zangu, mimi mwenyewe ninasadiki kwamba mmejaa wema na ufahamu wote, tena mnaweza kufundishana ninyi kwa ninyi.
Name ni mwine ni zuwisisa chenu, ba mwangu. Ni zuwisisa kuti nanwe bulyo mwi zwile bulotu, kwizula inzibo yonse. Ni zuwisisa kuti nanwe bulyo muwola kuli nyemuna zumwi ni zumwi.
15 Nimewaandikia kwa ujasiri vipengele kadha wa kadha katika waraka huu kama kuwakumbusha tena kwa habari ya ile neema Mungu aliyonipa,
Kono ni miñolela cha bundume bungi kwenu cha zintu zimwi ili ku mihupulisa hape, chebaka lye mpo ibahewa ime cha Ireeza.
16 ili kuwa mhudumu wa Kristo Yesu kwa watu wa Mataifa nikiwa na huduma ya kikuhani ya kutangaza Injili ya Mungu, ili watu wa Mataifa wapate kuwa dhabihu inayokubaliwa na Mungu, iliyotakaswa na Roho Mtakatifu.
Iyi mpo ibali kuti ni swanela ku ba ni muhikana wa Jesu Kirisite yo tumitwe ku Basikunze, kuha sina mupurisita ivangeli ya Ireeza. Ni swanela kutenda bulyo ili kuti inubu i Basikunze pona chi itambulwa, ku jolozwa cha Luhuho Lujolola.
17 Kwa hiyo ninajisifu katika Kristo Yesu, kwenye utumishi wangu kwa Mungu.
Imi kusanga kwangu kwina mwa Jesu Kirisite ni muzintu za Ireeza.
18 Kwa maana sitathubutu kusema kitu chochote zaidi ya kile ambacho Kristo amefanya kwa kunitumia mimi katika kuwaongoza watu wa Mataifa wamtii Mungu kwa yale niliyosema na kufanya,
Njikuti kese ni wambe chimwi kwande yecho Kirisite cha ba maniselezi kuzwa kwangu cha ku kuteka ku Basikunze. Izi zintu zitendwa cha linzwii ni mutendo,
19 kwa nguvu za ishara na miujiza, kwa uweza wa Roho wa Mungu, hivyo kuanzia Yerusalemu hadi maeneo yote ya kandokando yake mpaka Iliriko, nimekwisha kuihubiri Injili ya Kristo kwa ukamilifu.
cha ziho za zisupo ni zikomokisa, ni cha ziho za Luhuho Lujolola. Ichi chi bapangahali bulyo kuti kuzwa mwa Jerusalema, mi ni kuzimbuluka umo mane ku kasika kwa Iliriko, ili kuti niwole kutwala linzwi lya Kirisite cho kwizula.
20 Hivyo ni nia yangu kuhubiri Habari Njema, si pale ambapo Kristo amekwisha kujulikana, ili nisije nikajenga juu ya msingi wa mtu mwingine.
Che iyi nzila, intakazo yangu ibali ya kuwamba ivangeli, kono isiñi kwe zibitwe Kirisite chezina, ili kuti kanzi ni zaki hewulu lya mutomo wa zumwi muntu.
21 Lakini kama ilivyoandikwa: “Wale ambao hawajahubiriwa habari zake wataona, nao wale ambao hawajazisikia watafahamu.”
Mukwikalile sina mu kuñolwe: “Abo kubali basena ba ba wambilwe zakwe mwize mu mubone, mi nabo basena ba bazuwi kaba zuwe.”
22 Hii ndiyo sababu nimezuiliwa mara nyingi nisiweze kuja kwenu.
Kuzwaho ni ba kaniswa tungi kukwiza kwenu.
23 Lakini sasa kwa kuwa hakuna nafasi zaidi kwa ajili yangu katika sehemu hii, ninatamani kuja kwenu kama ambavyo nimekuwa na shauku kwa miaka mingi.
Kono hanu, ka nisina chibaka mwezi zikiliti, mi ni ba lyolelwe cha zillimo zingi kwiza kwenu.
24 Nimekusudia kufanya hivyo nitakapokuwa njiani kwenda Hispania. Natarajia kuwaona katika safari yangu na kusafirishwa nanyi mpaka huko, baada ya kufurahia ushirika wenu kwa kitambo kidogo.
Monse muniyendela kwa Sipeini, ni sepa ku mibona ha nihita, mi ni ku nisindikizwa munzila chenu, hani mana ku likola kuli kopanya nanwe che nako zana.
25 Sasa, niko njiani kuelekea Yerusalemu kwa ajili ya kuwahudumia watakatifu huko.
Kono hanu ni kaya kwa Jerusalema kuka tendela ba zumine.
26 Kwa kuwa imewapendeza watu wa Makedonia na Akaya kufanya changizo kwa ajili ya maskini walioko miongoni mwa watakatifu huko Yerusalemu.
Sina hakubali kulotu ku tabisa kwa Masedonia ni Akaya kuha chimwi ku basena mukati ka bazumine mwa Jerusalema.
27 Imewapendeza kufanya hivyo, naam, kwani ni wadeni wao. Kwa maana ikiwa watu wa Mataifa wameshiriki baraka za rohoni za Wayahudi, wao ni wadeni wa Wayahudi, ili Wayahudi nao washiriki baraka zao za mambo ya mwilini.
Eee, ku bali kutabiswa kwabo, imi, luli, cho kuti ba bali ku bakolota. Mi heiba Basikunze ba bali abeli muzintu zabo za luhuho, ba bakolota nabo cha ku batenda muzintu zi boneka.
28 Kwa hiyo baada ya kukamilisha kazi hii na kuhakikisha kuwa wamepokea kila kitu kilichokusanywa, nitapitia kwenu nikiwa njiani kwenda Hispania.
Kuzwaho, ha ni mana uwu mutendo ni ku bona kuti batambula zonse zi baletwa, ka ni yende kwa Sipeini ni ku mipotela hani hita.
29 Ninajua kwamba nitakapokuja kwenu, nitakuja na wingi wa baraka za Kristo.
Nizi kuti ha nikeza kwenu kani ni ze mu kwizula che mbuyoti ya Kirisite
30 Basi, ndugu zangu, nawasihi kwa Jina la Bwana wetu Yesu Kristo na kwa upendo wa Roho Mtakatifu, kujiunga nami katika taabu zangu mkiniombea kwa Mungu.
Hanu ni mi susuweza, ba mwangu, cha Simwine wetu Jesu Kirisite, imi ni chelato lya Luhuho, kuti mulike hahulu mubonse name mwi intampelo kwa Ireeza changu.
31 Ombeni ili nipate kuokolewa mikononi mwa wale wasioamini walioko Uyahudi, na kwamba utumishi wangu upate kukubaliwa na watakatifu wa huko Yerusalemu,
Mulapele kuti ni bukelezwe kwa bana basa kuteki mwa Judea, ili kuti kutenda kwangu mwa Jerusalema ku tambulwe ku bazumine.
32 ili kwa mapenzi ya Mungu niweze kuja kwenu kwa furaha, nami niburudishwe pamoja nanyi.
Mulapele kuti ni ze kwenu che intabo che intato ya Ireeza, ili kuti Ime, hamwina nanwe, ni wane impumulo.
33 Mungu wa amani na awe pamoja nanyi nyote. Amen.
Mi Ireeza we inkozo abe nanwe mubonse. Amen.

< Warumi 15 >