< Warumi 15 >

1 Sisi tulio na nguvu, hatuna budi kuchukuliana na kushindwa kwa wale walio dhaifu wala si kujipendeza nafsi zetu wenyewe.
Povinniť jsme pak my silní mdloby nemocných snášeti, a ne sami sobě se líbiti.
2 Kila mmoja wetu inampasa kumpendeza jirani yake kwa mambo mema, ili kumjenga katika imani.
A protož jeden každý z nás bližnímu se lib k dobrému pro vzdělání.
3 Kwa maana hata Kristo hakujipendeza mwenyewe, bali kama ilivyoandikwa: “Matukano yao wale wanaokutukana wewe yalinipata mimi.”
Nebo i Kristus ne sám se sobě líbil, ale jakož psáno jest: Hanění hanějících tebe připadla na mne.
4 Kwa maana kila kitu kilichoandikwa zamani, kiliandikwa kutufundisha, ili kwamba kwa saburi na faraja tunayopata katika Maandiko tuwe na tumaini.
Nebo kteréžkoli věci napsány jsou, k našemu naučení napsány jsou, abychom skrze snášelivost a potěšení písem naději měli.
5 Mungu atoaye saburi na faraja, awajalie ninyi roho ya umoja miongoni mwenu mnapomfuata Kristo Yesu,
Bůh pak snášelivosti a potěšení dejž vám býti jednomyslnými vespolek podlé Jezukrista,
6 ili kwa moyo mmoja mpate kumtukuza Mungu aliye Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo.
Abyste jednomyslně jedněmi ústy oslavovali Boha a Otce Pána našeho Jezukrista.
7 Karibishaneni ninyi kwa ninyi kama Kristo alivyowakaribisha ninyi ili kumletea Mungu utukufu.
Protož přijímejte se vespolek, jakož i Kristus přijal nás v slávu Boží.
8 Kwa maana nawaambia kwamba, Kristo amekuwa mtumishi kwa wale waliotahiriwa ili kuonyesha kweli ya Mungu na kuthibitisha zile ahadi walizopewa baba zetu wa zamani,
Neboť pravím, že Kristus Ježíš byl služebníkem obřízky pro Boží pravost, aby potvrdil slibů otcům,
9 pia ili watu wa Mataifa wamtukuze Mungu kwa rehema zake. Kama ilivyoandikwa: “Kwa hiyo nitakutukuza katikati ya watu wa Mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.”
A aby pohané z milosrdenství slavili Boha, jakož psáno jest: Protož vyznávati tebe budu mezi pohany, a jménu tvému plésati budu.
10 Tena yasema, “Enyi watu wa Mataifa, furahini pamoja na watu wa Mungu.”
A opět dí: Veselte se pohané s lidem jeho.
11 Tena, “Msifuni Bwana, ninyi watu wa Mataifa wote, na kumwimbia sifa, enyi watu wote.”
A opět: Chvalte Hospodina všickni národové, a velebtež ho všickni lidé.
12 Tena Isaya anasema, “Shina la Yese litachipuka, yeye atakayeinuka ili kutawala juu ya mataifa. Watu wa Mataifa watamtumaini.”
A opět Izaiáš dí: Budeť kořen Jesse, a v tom, kterýž povstane, aby panoval nad pohany, pohané doufati budou.
13 Mungu wa tumaini awajaze ninyi furaha yote na amani katika kumwamini, ili mpate kujawa na tumaini tele kwa nguvu ya Roho Mtakatifu.
Bůh pak naděje naplňujž vás všelikou radostí a pokojem u víře, abyste se rozhojnili v naději skrze moc Ducha svatého.
14 Ndugu zangu, mimi mwenyewe ninasadiki kwamba mmejaa wema na ufahamu wote, tena mnaweza kufundishana ninyi kwa ninyi.
Jist jsem zajisté, bratří moji, i já také o vás, že i vy jste plní dobroty, naplněni jsouce všelikou známostí, tak že se i napomínati můžete vespolek.
15 Nimewaandikia kwa ujasiri vipengele kadha wa kadha katika waraka huu kama kuwakumbusha tena kwa habari ya ile neema Mungu aliyonipa,
A však psal jsem vám, bratří, poněkud směle, jako napomínaje vás, podlé milosti, kteráž jest mi dána od Boha,
16 ili kuwa mhudumu wa Kristo Yesu kwa watu wa Mataifa nikiwa na huduma ya kikuhani ya kutangaza Injili ya Mungu, ili watu wa Mataifa wapate kuwa dhabihu inayokubaliwa na Mungu, iliyotakaswa na Roho Mtakatifu.
K tomu abych byl služebníkem Ježíše Krista mezi pohany, slouže evangelium Božímu, aby byla obět pohanů vzácná, posvěcena jsuci skrze ducha svatého.
17 Kwa hiyo ninajisifu katika Kristo Yesu, kwenye utumishi wangu kwa Mungu.
Mám se tedy čím chlubiti v Kristu Ježíši, v Božích věcech.
18 Kwa maana sitathubutu kusema kitu chochote zaidi ya kile ambacho Kristo amefanya kwa kunitumia mimi katika kuwaongoza watu wa Mataifa wamtii Mungu kwa yale niliyosema na kufanya,
Neboť bych nesměl mluviti toho, čehož by skrze mne neučinil Kristus, ku poslušenství pohanů, slovem i skutkem,
19 kwa nguvu za ishara na miujiza, kwa uweza wa Roho wa Mungu, hivyo kuanzia Yerusalemu hadi maeneo yote ya kandokando yake mpaka Iliriko, nimekwisha kuihubiri Injili ya Kristo kwa ukamilifu.
V moci divů a zázraků, v síle Ducha Božího, tak že jsem od Jeruzaléma vůkol až k Illyrické zemi naplnil evangelium Kristovým,
20 Hivyo ni nia yangu kuhubiri Habari Njema, si pale ambapo Kristo amekwisha kujulikana, ili nisije nikajenga juu ya msingi wa mtu mwingine.
A to tak byv žádostiv kázati evangelium, kdež ani jmenován nebyl Kristus, abych na cizí základ nestavěl,
21 Lakini kama ilivyoandikwa: “Wale ambao hawajahubiriwa habari zake wataona, nao wale ambao hawajazisikia watafahamu.”
Ale jakož psáno jest: Kterýmž není zvěstováno o něm, uzří, a ti, kteříž neslýchali, srozumějí.
22 Hii ndiyo sababu nimezuiliwa mara nyingi nisiweze kuja kwenu.
A tímť jest mi mnohokrát překaženo přijíti k vám.
23 Lakini sasa kwa kuwa hakuna nafasi zaidi kwa ajili yangu katika sehemu hii, ninatamani kuja kwenu kama ambavyo nimekuwa na shauku kwa miaka mingi.
Nyní pak nemaje již více místa v těchto krajinách, a žádost maje přijíti k vám od mnoha let,
24 Nimekusudia kufanya hivyo nitakapokuwa njiani kwenda Hispania. Natarajia kuwaona katika safari yangu na kusafirishwa nanyi mpaka huko, baada ya kufurahia ushirika wenu kwa kitambo kidogo.
Kdyžkoli půjdu do Hišpanie, přijdu k vám. Mámť zajisté naději, že tudy jda, uzřím vás, a že vy mne provodíte tam, a však až bych prvé u vás poněkud pobyl.
25 Sasa, niko njiani kuelekea Yerusalemu kwa ajili ya kuwahudumia watakatifu huko.
Nyní pak beru se do Jeruzaléma, službu čině svatým.
26 Kwa kuwa imewapendeza watu wa Makedonia na Akaya kufanya changizo kwa ajili ya maskini walioko miongoni mwa watakatifu huko Yerusalemu.
Nebo za dobré se vidělo Macedonským a Achaiským, aby zbírku nějakou učinili na chudé svaté, kteříž jsou v Jeruzalémě.
27 Imewapendeza kufanya hivyo, naam, kwani ni wadeni wao. Kwa maana ikiwa watu wa Mataifa wameshiriki baraka za rohoni za Wayahudi, wao ni wadeni wa Wayahudi, ili Wayahudi nao washiriki baraka zao za mambo ya mwilini.
Takť sobě to oblíbili, a také povinni jsou jim to. Nebo poněvadž duchovním věcem jejich obcovali pohané, povinniť jsou jim také sloužiti tělesnými.
28 Kwa hiyo baada ya kukamilisha kazi hii na kuhakikisha kuwa wamepokea kila kitu kilichokusanywa, nitapitia kwenu nikiwa njiani kwenda Hispania.
A protož když to vykonám, a jim odvedu užitek ten, půjduť skrze vás do Hišpanie.
29 Ninajua kwamba nitakapokuja kwenu, nitakuja na wingi wa baraka za Kristo.
A vímť, že když přijdu k vám, v hojnosti požehnání evangelium Kristova přijdu.
30 Basi, ndugu zangu, nawasihi kwa Jina la Bwana wetu Yesu Kristo na kwa upendo wa Roho Mtakatifu, kujiunga nami katika taabu zangu mkiniombea kwa Mungu.
Prosímť pak vás, bratří, skrze Pána našeho Jezukrista a skrze lásku Ducha, abyste spolu se mnou modlili se za mne Bohu snažně,
31 Ombeni ili nipate kuokolewa mikononi mwa wale wasioamini walioko Uyahudi, na kwamba utumishi wangu upate kukubaliwa na watakatifu wa huko Yerusalemu,
Abych vysvobozen byl od protivníků v Judstvu, a aby služba tato má příjemná byla svatým v Jeruzalémě,
32 ili kwa mapenzi ya Mungu niweze kuja kwenu kwa furaha, nami niburudishwe pamoja nanyi.
Abych k vám bohdá s radostí přišel, a s vámi poodpočinul.
33 Mungu wa amani na awe pamoja nanyi nyote. Amen.
Bůh pak pokoje se všemi vámi. Amen.

< Warumi 15 >