< Warumi 14 >

1 Mkaribisheni yeye ambaye imani yake ni dhaifu, lakini si kwa kugombana na kubishana juu ya mawazo yake.
A tego, kto jest słaby w wierze, przyjmujcie, [lecz] nie po to, aby sprzeczać się [wokół] spornych kwestii.
2 Mtu mmoja imani yake inamruhusu kula kila kitu, lakini mwingine ambaye imani yake ni dhaifu, hula mboga tu.
Jeden bowiem wierzy, że może jeść wszystko, a inny, [będąc] słaby, jada jarzyny.
3 Yeye alaye kila kitu asimdharau yeye asiyekula. Wala yeye asiyekula kila kitu asimhukumu yule alaye kila kitu, kwa maana Mungu amemkubali.
Ten, kto je, niech nie lekceważy tego, który nie je, a ten, kto nie je, niech nie potępia tego, który je, bo Bóg go przyjął.
4 Wewe ni nani hata umhukumu mtumishi wa mtu mwingine? Kwa bwana wake tu anasimama au kuanguka. Naye atasimama kwa sababu Bwana anaweza kumsimamisha.
Kim jesteś ty, że sądzisz cudzego sługę? Dla własnego Pana stoi albo upada. Ostoi się jednak, gdyż Bóg może go utwierdzić.
5 Mtu mmoja anaitukuza siku fulani kuwa ni bora kuliko nyingine, na mwingine anaona kuwa siku zote ni sawa. Basi kila mmoja awe na hakika na yale anayoamini.
Jeden bowiem czyni różnicę między dniem a dniem, a drugi każdy dzień ocenia [jednakowo]. Każdy niech będzie dobrze upewniony w swoim zamyśle.
6 Yeye anayehesabu siku moja kuwa takatifu kuliko nyingine, hufanya hivyo kwa kumheshimu Bwana. Naye alaye nyama hula kwa Bwana, kwa maana humshukuru Mungu, naye akataaye kula nyama hufanya hivyo kwa Bwana na humshukuru Mungu.
Kto przestrzega dnia, dla Pana przestrzega, a kto nie przestrzega dnia, dla Pana nie przestrzega. Kto je, dla Pana je, bo dziękuje Bogu, a kto nie je, dla Pana nie je i dziękuje Bogu.
7 Kwa kuwa hakuna hata mmoja wetu anayeishi kwa ajili yake mwenyewe, wala hakuna hata mmoja wetu afaye kwa ajili yake mwenyewe.
Nikt bowiem z nas dla siebie nie żyje i nikt dla siebie nie umiera.
8 Kama tunaishi, tunaishi kwa Bwana, nasi pia tukifa tunakufa kwa Bwana. Kwa hiyo basi, kama tukiishi au kama tukifa, sisi ni mali ya Bwana.
Bo jeśli żyjemy, dla Pana żyjemy, jeśli umieramy, dla Pana umieramy. Dlatego czy żyjemy, czy umieramy, należymy do Pana.
9 Kwani kwa sababu hii hasa, Kristo alikufa na akawa hai tena kusudi apate kuwa Bwana wa wote, yaani, waliokufa na walio hai.
Gdyż po to Chrystus umarł, powstał i ożył, aby panować i [nad] umarłymi, i nad żywymi.
10 Basi kwa nini wewe wamhukumu ndugu yako? Au kwa nini wewe unamdharau ndugu yako? Kwa kuwa sote tutasimama mbele ya kiti cha Mungu cha hukumu.
Dlaczego więc ty potępiasz swego brata? Albo czemu lekceważysz swego brata? Wszyscy bowiem staniemy przed trybunałem Chrystusa.
11 Kwa kuwa imeandikwa: “‘Kama vile niishivyo,’ asema Bwana, ‘kila goti litapigwa mbele zangu, na kila ulimi utakiri kwa Mungu.’”
Jest bowiem napisane: Jak żyję, mówi Pan, ugnie się przede mną każde kolano i każdy język będzie wysławiał Boga.
12 Hivyo basi kila mmoja wetu atatoa habari zake mwenyewe kwa Mungu.
Tak więc każdy z nas sam za siebie zda rachunek Bogu.
13 Kwa hiyo tusiendelee kuhukumiana: Badala yake mtu asiweke kamwe kikwazo au kizuizi katika njia ya ndugu mwingine.
A tak już nie osądzajmy jedni drugich, ale raczej uważajcie na to, aby nie dawać bratu powodu do potknięcia się lub upadku.
14 Ninajua tena nimehakikishiwa sana katika Bwana Yesu kwamba hakuna kitu chochote ambacho ni najisi kwa asili yake. Lakini kama mtu anakiona kitu kuwa ni najisi, basi kwake huyo kitu hicho ni najisi.
Wiem i jestem przekonany przez Pana Jezusa, że nie ma niczego, co by samo w sobie było nieczyste. Tylko dla tego, kto uważa coś za nieczyste, [to] dla niego [jest] nieczyste.
15 Kama ndugu yako anahuzunishwa kwa sababu ya kile unachokula, basi huenendi tena katika upendo. Usiruhusu kile unachokula kiwe sababu ya kumwangamiza ndugu yako ambaye Kristo alikufa kwa ajili yake.
Lecz jeśli z powodu pokarmu twój brat jest zasmucony, już nie postępujesz zgodnie z miłością. Nie zatracaj swoim pokarmem tego, za którego umarł Chrystus.
16 Usiruhusu kile ambacho unakiona kuwa chema kisemwe kuwa ni kiovu.
Niech więc wasze dobro nie będzie bluźnione.
17 Kwa maana Ufalme wa Mungu si kula na kunywa, bali ni haki, amani na furaha katika Roho Mtakatifu.
Królestwo Boże bowiem to nie pokarm i napój, ale sprawiedliwość, pokój i radość w Duchu Świętym.
18 Kwa sababu mtu yeyote anayemtumikia Kristo kwa jinsi hii, anampendeza Mungu na kukubaliwa na wanadamu.
Kto bowiem w tym służy Chrystusowi, podoba się Bogu i cieszy się uznaniem u ludzi.
19 Kwa hiyo na tufanye bidii kutafuta yale yaletayo amani na kujengana sisi kwa sisi.
Tak więc dążmy do tego, co [służy] pokojowi i wzajemnemu zbudowaniu.
20 Usiiharibu kazi ya Mungu kwa ajili ya chakula. Hakika vyakula vyote ni safi, lakini ni kosa kula kitu chochote kinachomsababisha ndugu yako ajikwae.
Z powodu pokarmu nie niszcz dzieła Bożego. Wszystko wprawdzie jest czyste, ale [staje się] złe dla człowieka, który je ze zgorszeniem.
21 Ni afadhali kutokula nyama wala kunywa divai au kufanya jambo lingine lolote litakalomsababisha ndugu yako ajikwae.
Dobrze jest nie jeść mięsa i nie pić wina ani żadnej [rzeczy], przez którą twój brat się obraża, gorszy albo słabnie.
22 Je, wewe unayo imani? Ile imani uliyo nayo, uwe nayo nafsini mwako mbele za Mungu. Heri mtu yule asiye na sababu ya kujihukumu nafsi yake kwa ajili ya kile anachokifanya.
Masz wiarę? Miej ją sam u siebie przed Bogiem. Szczęśliwy ten, kto samego siebie nie potępia [w tym], co uważa za dobre.
23 Lakini kama mtu ana shaka kuhusu kile anachokula, amehukumiwa, kwa sababu hakula kwa imani. Kwa kuwa chochote kinachofanywa pasipo imani ni dhambi.
Lecz kto ma wątpliwości, jeśli je, jest potępiony, bo nie je z wiary. Wszystko bowiem, co nie jest z wiary, jest grzechem.

< Warumi 14 >