< Warumi 11 >
1 Basi nauliza: Je, Mungu amewakataa watu wake? La, hasha! Mimi mwenyewe ni Mwisraeli, tena uzao wa Abrahamu kutoka kabila la Benyamini.
I say then, Did God cast off his people? God forbid. For I also am an Israelite, of the seed of Abraham, of the tribe of Benjamin.
2 Mungu hajawakataa watu wake, ambao yeye aliwajua tangu mwanzo. Je, hamjui yale Maandiko yasemayo kuhusu Eliya, jinsi alivyomlalamikia Mungu kuhusu Israeli?
God did not cast off his people which he foreknew. Or wot ye not what the scripture saith of Elijah? how he pleadeth with God against Israel,
3 Alisema, “Bwana, wamewaua manabii wako na kuzibomoa madhabahu zako, nimebaki mimi peke yangu, nao wanataka kuniua?”
Lord, they have killed thy prophets, they have digged down thine altars: and I am left alone, and they seek my life.
4 Je, Mungu alimjibuje? “Nimejibakizia watu elfu saba ambao hawajapiga magoti kumwabudu Baali.”
But what saith the answer of God unto him? I have left for myself seven thousand men, who have not bowed the knee to Baal.
5 Vivyo hivyo pia, sasa wapo mabaki waliochaguliwa kwa neema ya Mungu.
Even so then at this present time also there is a remnant according to the election of grace.
6 Lakini ikiwa wamechaguliwa kwa neema, si tena kwa msingi wa matendo. Kama ingekuwa kwa matendo, neema isingekuwa neema tena.
But if it is by grace, it is no more of works: otherwise grace is no more grace.
7 Tuseme nini basi? Kile kitu ambacho Israeli alikitafuta kwa bidii hakukipata. Lakini waliochaguliwa walikipata. Waliobaki walifanywa wagumu,
What then? That which Israel seeketh for, that he obtained not; but the election obtained it, and the rest were hardened:
8 kama ilivyoandikwa: “Mungu aliwapa bumbuazi la mioyo, macho ili wasiweze kuona, na masikio ili wasiweze kusikia, hadi leo.”
according as it is written, God gave them a spirit of stupor, eyes that they should not see, and ears that they should not hear, unto this very day.
9 Naye Daudi anasema: “Karamu zao na ziwe tanzi na mtego wa kuwanasa, kitu cha kuwakwaza waanguke, na adhabu kwao.
And David saith, Let their table be made a snare, and a trap, And a stumblingblock, and a recompense unto them:
10 Macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona, nayo migongo yao iinamishwe daima.”
Let their eyes be darkened, that they may not see, And bow thou down their back alway.
11 Hivyo nauliza tena: Je, Waisraeli walijikwaa ili waanguke na kuangamia kabisa? La, hasha! Lakini kwa sababu ya makosa yao, wokovu umewafikia watu wa Mataifa, ili kuwafanya Waisraeli waone wivu.
I say then, Did they stumble that they might fall? God forbid: but by their fall salvation [is come] unto the Gentiles, for to provoke them to jealousy.
12 Basi ikiwa kukosa kwao kumekuwa utajiri mkubwa kwa ulimwengu, tena kama kuangamia kwao kumeleta utajiri kwa watu wa Mataifa, kurudishwa kwao kutaleta utajiri mkuu zaidi.
Now if their fall is the riches of the world, and their loss the riches of the Gentiles; how much more their fulness?
13 Sasa ninasema nanyi watu wa Mataifa. Maadamu mimi ni mtume kwa watu wa Mataifa, naitukuza huduma yangu
But I speak to you that are Gentiles. Inasmuch then as I am an apostle of Gentiles, I glorify my ministry:
14 ili kuwafanya watu wangu waone wivu na hivyo kuwaokoa baadhi yao.
if by any means I may provoke to jealousy [them that are] my flesh, and may save some of them.
15 Kwa kuwa ikiwa kukataliwa kwao ni kupatanishwa kwa ulimwengu, kukubaliwa kwao si kutakuwa ni uhai baada ya kufa?
For if the casting away of them [is] the reconciling of the world, what [shall] the receiving [of them be], but life from the dead?
16 Kama sehemu ya donge la unga uliotolewa kuwa limbuko ni mtakatifu, basi unga wote ni mtakatifu, nalo shina kama ni takatifu, vivyo hivyo na matawi nayo.
And if the firstfruit is holy, so is the lump: and if the root is holy, so are the branches.
17 Lakini kama baadhi ya matawi yalikatwa, nawe chipukizi la mzeituni mwitu ukapandikizwa mahali pao ili kushiriki unono pamoja na matawi mengine kutoka shina la mzeituni,
But if some of the branches were broken off, and thou, being a wild olive, wast grafted in among them, and didst become partaker with them of the root of the fatness of the olive tree;
18 basi usijivune juu ya hayo matawi. Kama ukijivuna, kumbuka jambo hili: si wewe unayelishikilia shina, bali ni shina linalokushikilia wewe.
glory not over the branches: but if thou gloriest, it is not thou that bearest the root, but the root thee.
19 Basi utasema, “Matawi yale yalikatwa ili nipate kupandikizwa katika hilo shina.”
Thou wilt say then, Branches were broken off, that I might be grafted in.
20 Hii ni kweli. Matawi hayo yalikatwa kwa sababu ya kutokuamini kwake, lakini wewe umesimama tu kwa sababu ya imani. Kwa hiyo usijivune, bali simama kwa kuogopa.
Well; by their unbelief they were broken off, and thou standest by thy faith. Be not highminded, but fear:
21 Kwa maana kama Mungu hakuyahurumia matawi ya asili, wala hatakuhurumia wewe.
for if God spared not the natural branches, neither will he spare thee.
22 Angalia basi wema na ukali wa Mungu: Kwa wale walioanguka, ukali, bali kwako wewe wema wa Mungu, kama utadumu katika wema wake. La sivyo, nawe utakatiliwa mbali.
Behold then the goodness and severity of God: toward them that fell, severity; but toward thee, God’s goodness, if thou continue in his goodness: otherwise thou also shalt be cut off.
23 Wao nao wasipodumu katika kutokuamini kwao, watapandikizwa tena kwenye shina, kwa maana Mungu anao uwezo wa kuwapandikiza tena kwenye hilo shina.
And they also, if they continue not in their unbelief, shall be grafted in: for God is able to graft them in again.
24 Ikiwa wewe ulikatwa kutoka kile ambacho kwa asili ni mzeituni mwitu na kupandikizwa kinyume cha asili kwenye mzeituni uliopandwa, si rahisi zaidi matawi haya ya asili kupandikizwa tena kwenye shina lake la mzeituni!
For if thou wast cut out of that which is by nature a wild olive tree, and wast grafted contrary to nature into a good olive tree: how much more shall these, which are the natural [branches], be grafted into their own olive tree?
25 Ndugu zangu, ili msije mkajidai kuwa wenye hekima kuliko mlivyo, nataka mfahamu siri hii: Ugumu umewapata Israeli kwa sehemu hadi idadi ya watu wa Mataifa watakaoingia itimie.
For I would not, brethren, have you ignorant of this mystery, lest ye be wise in your own conceits, that a hardening in part hath befallen Israel, until the fulness of the Gentiles be come in;
26 Hivyo Israeli wote wataokolewa. Kama ilivyoandikwa: “Mkombozi atakuja kutoka Sayuni; ataondoa kutokumcha Mungu katika Yakobo.
and so all Israel shall be saved: even as it is written, There shall come out of Zion the Deliverer; He shall turn away ungodliness from Jacob:
27 Hili ndilo agano langu nao nitakapoziondoa dhambi zao.”
And this is my covenant unto them, When I shall take away their sins.
28 Kwa habari ya Injili, wao ni adui wa Mungu kwa ajili yenu, lakini kuhusu kule kuteuliwa kwao ni wapendwa, kwa ajili ya mababa zao wa zamani,
As touching the gospel, they are enemies for your sake: but as touching the election, they are beloved for the fathers’ sake.
29 kwa maana akishawapa watu karama, Mungu haziondoi, wala wito wake.
For the gifts and the calling of God are without repentance.
30 Kama vile ninyi wakati fulani mlivyokuwa waasi kwa Mungu lakini sasa mmepata rehema kwa sababu ya kutokutii kwao,
For as ye in time past were disobedient to God, but now have obtained mercy by their disobedience,
31 hivyo nao Waisraeli wamekuwa waasi ili kwamba wao nao sasa waweze kupata rehema kwa ajili ya rehema za Mungu kwenu.
even so have these also now been disobedient, that by the mercy shewn to you they also may now obtain mercy.
32 Kwa maana Mungu amewafunga wanadamu wote kwenye kuasi ili apate kuwarehemu wote. (eleēsē )
For God hath shut up all unto disobedience, that he might have mercy upon all. (eleēsē )
33 Tazama jinsi kilivyo kina cha utajiri wa hekima na maarifa ya Mungu! Tazama jinsi ambavyo hukumu zake hazichunguziki, na ambavyo njia zake zisivyotafutikana!
O the depth of the riches both of the wisdom and the knowledge of God! how unsearchable are his judgments, and his ways past tracing out!
34 “Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana? Au ni nani ambaye amekuwa mshauri wake?”
For who hath known the mind of the Lord? or who hath been his counsellor?
35 “Au ni nani aliyempa chochote ili arudishiwe?”
or who hath first given to him, and it shall be recompensed unto him again?
36 Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake, viko kwake na kwa ajili yake. Utukufu ni wake milele! Amen. (aiōn )
For of him, and through him, and unto him, are all things. To him [be] the glory for ever. Amen. (aiōn )