< Warumi 11 >
1 Basi nauliza: Je, Mungu amewakataa watu wake? La, hasha! Mimi mwenyewe ni Mwisraeli, tena uzao wa Abrahamu kutoka kabila la Benyamini.
I say then, Hath God cast off his people? Far be it I For I myself am an Israelite, of the seed of Abraham, of the tribe of Benjamin.
2 Mungu hajawakataa watu wake, ambao yeye aliwajua tangu mwanzo. Je, hamjui yale Maandiko yasemayo kuhusu Eliya, jinsi alivyomlalamikia Mungu kuhusu Israeli?
God hath not cast off his people, which he foreknew. Do ye not know what the Scripture saith in the passage concerning Elijah? how he pleadeth to God against Israel:
3 Alisema, “Bwana, wamewaua manabii wako na kuzibomoa madhabahu zako, nimebaki mimi peke yangu, nao wanataka kuniua?”
“Lord, they have killed thy prophets, they have dug down thine altars; and I am left alone, and they are seeking my life.”
4 Je, Mungu alimjibuje? “Nimejibakizia watu elfu saba ambao hawajapiga magoti kumwabudu Baali.”
But what saith the answer of God to him? “I have reserved to myself seven thousand men, who have not bowed the knee to Baal.”
5 Vivyo hivyo pia, sasa wapo mabaki waliochaguliwa kwa neema ya Mungu.
In the same way then at this present time also there is a remnant, according to the election of grace.
6 Lakini ikiwa wamechaguliwa kwa neema, si tena kwa msingi wa matendo. Kama ingekuwa kwa matendo, neema isingekuwa neema tena.
And if it is by grace, it is no longer on account of works; otherwise grace ceaseth to be grace; but if it is of works, there is then no grace; otherwise work ceaseth to be work. How is it then?
7 Tuseme nini basi? Kile kitu ambacho Israeli alikitafuta kwa bidii hakukipata. Lakini waliochaguliwa walikipata. Waliobaki walifanywa wagumu,
What Israel seeketh after, that Israel did not obtain; but the elect obtained it, and the rest were hardened;
8 kama ilivyoandikwa: “Mungu aliwapa bumbuazi la mioyo, macho ili wasiweze kuona, na masikio ili wasiweze kusikia, hadi leo.”
as it is written: “God gave them a spirit of slumber, eyes that were not to see, and ears that were not to hear, unto this day.”
9 Naye Daudi anasema: “Karamu zao na ziwe tanzi na mtego wa kuwanasa, kitu cha kuwakwaza waanguke, na adhabu kwao.
And David saith, “Let their table become a snare, and a trap, and a stumbling-block, and a recompense to them;
10 Macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona, nayo migongo yao iinamishwe daima.”
let their eyes be darkened, that they may not see; and bow down their back alway.”
11 Hivyo nauliza tena: Je, Waisraeli walijikwaa ili waanguke na kuangamia kabisa? La, hasha! Lakini kwa sababu ya makosa yao, wokovu umewafikia watu wa Mataifa, ili kuwafanya Waisraeli waone wivu.
I say then, Did they stumble in order to fall? God forbid! But by their offence salvation is come to the gentiles to excite them to emulation.
12 Basi ikiwa kukosa kwao kumekuwa utajiri mkubwa kwa ulimwengu, tena kama kuangamia kwao kumeleta utajiri kwa watu wa Mataifa, kurudishwa kwao kutaleta utajiri mkuu zaidi.
But if their offence is the riches of the world, and their loss the riches of the gentiles, how much more will their fullness be?
13 Sasa ninasema nanyi watu wa Mataifa. Maadamu mimi ni mtume kwa watu wa Mataifa, naitukuza huduma yangu
For I am speaking to you gentiles; inasmuch as I am the apostle of the gentiles, I magnify my office,
14 ili kuwafanya watu wangu waone wivu na hivyo kuwaokoa baadhi yao.
that I may, if possible, excite to emulation those who are my flesh, and may save some of them.
15 Kwa kuwa ikiwa kukataliwa kwao ni kupatanishwa kwa ulimwengu, kukubaliwa kwao si kutakuwa ni uhai baada ya kufa?
For if the rejection of them is the reconciliation of the world, what will the reception of them be, but life from the dead?
16 Kama sehemu ya donge la unga uliotolewa kuwa limbuko ni mtakatifu, basi unga wote ni mtakatifu, nalo shina kama ni takatifu, vivyo hivyo na matawi nayo.
And if the first portion of the dough is holy, so also will be the lump; and if the root is holy, so will be the branches.
17 Lakini kama baadhi ya matawi yalikatwa, nawe chipukizi la mzeituni mwitu ukapandikizwa mahali pao ili kushiriki unono pamoja na matawi mengine kutoka shina la mzeituni,
And if some of the branches have been broken off, and thou, a wild olive, hast been grafted in among them, and become a partaker with them of the root and fatness of the olive-tree,
18 basi usijivune juu ya hayo matawi. Kama ukijivuna, kumbuka jambo hili: si wewe unayelishikilia shina, bali ni shina linalokushikilia wewe.
boast not over the branches; for if thou boast, thou dost not bear the root, but the root thee.
19 Basi utasema, “Matawi yale yalikatwa ili nipate kupandikizwa katika hilo shina.”
Thou wilt say then, The branches were broken off, that I might be grafted in.
20 Hii ni kweli. Matawi hayo yalikatwa kwa sababu ya kutokuamini kwake, lakini wewe umesimama tu kwa sababu ya imani. Kwa hiyo usijivune, bali simama kwa kuogopa.
Be it so. It was for their unbelief that they were broken off, and thou standest through thy faith; be not high-minded, but fear.
21 Kwa maana kama Mungu hakuyahurumia matawi ya asili, wala hatakuhurumia wewe.
For if God spared the natural branches, take care lest he spare not thee.
22 Angalia basi wema na ukali wa Mungu: Kwa wale walioanguka, ukali, bali kwako wewe wema wa Mungu, kama utadumu katika wema wake. La sivyo, nawe utakatiliwa mbali.
Behold then the goodness and the severity of God; toward those who fell, severity; but toward thee God's goodness, if thou continue in his goodness; otherwise thou also wilt be cut off.
23 Wao nao wasipodumu katika kutokuamini kwao, watapandikizwa tena kwenye shina, kwa maana Mungu anao uwezo wa kuwapandikiza tena kwenye hilo shina.
And they also, if they do not continue in their unbelief, will be grafted in; for God is able to graft them in again.
24 Ikiwa wewe ulikatwa kutoka kile ambacho kwa asili ni mzeituni mwitu na kupandikizwa kinyume cha asili kwenye mzeituni uliopandwa, si rahisi zaidi matawi haya ya asili kupandikizwa tena kwenye shina lake la mzeituni!
For if thou hast been cut off from an olive-tree wild by nature, and hast against thy nature been ingrafted into a good olive-tree, how much more shall these, the natural branches, be ingrafted into their own olive-stock?
25 Ndugu zangu, ili msije mkajidai kuwa wenye hekima kuliko mlivyo, nataka mfahamu siri hii: Ugumu umewapata Israeli kwa sehemu hadi idadi ya watu wa Mataifa watakaoingia itimie.
For I would not have you ignorant, brethren, of this mystery, lest ye should be wise in your own conceits, that blindness hath to some extent come upon Israel, until the fullness of the gentiles shall have come in.
26 Hivyo Israeli wote wataokolewa. Kama ilivyoandikwa: “Mkombozi atakuja kutoka Sayuni; ataondoa kutokumcha Mungu katika Yakobo.
And thus will all Israel be saved; as it is written, “There shall come out of Zion the Deliverer; he shall turn away ungodliness from Jacob.
27 Hili ndilo agano langu nao nitakapoziondoa dhambi zao.”
And this will be my covenant with them, when I shall have taken away their sins.”
28 Kwa habari ya Injili, wao ni adui wa Mungu kwa ajili yenu, lakini kuhusu kule kuteuliwa kwao ni wapendwa, kwa ajili ya mababa zao wa zamani,
In regard to the gospel, they are enemies for your sakes; but in regard to God's choice, they are beloved for the fathers' sake.
29 kwa maana akishawapa watu karama, Mungu haziondoi, wala wito wake.
For in respect to his gifts and his calling, there is no change of purpose with God.
30 Kama vile ninyi wakati fulani mlivyokuwa waasi kwa Mungu lakini sasa mmepata rehema kwa sababu ya kutokutii kwao,
For as ye in times past were disobedient to God, but have now obtained mercy through their disobedience,
31 hivyo nao Waisraeli wamekuwa waasi ili kwamba wao nao sasa waweze kupata rehema kwa ajili ya rehema za Mungu kwenu.
so they too have now become disobedient, that they also may obtain mercy through the mercy shown to you.
32 Kwa maana Mungu amewafunga wanadamu wote kwenye kuasi ili apate kuwarehemu wote. (eleēsē )
For God delivered up all to disobedience, that he might have mercy upon all. (eleēsē )
33 Tazama jinsi kilivyo kina cha utajiri wa hekima na maarifa ya Mungu! Tazama jinsi ambavyo hukumu zake hazichunguziki, na ambavyo njia zake zisivyotafutikana!
O the depth of the riches, and of the wisdom, and of the knowledge of God! How unsearchable are his purposes, and his ways past finding out!
34 “Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana? Au ni nani ambaye amekuwa mshauri wake?”
For “who hath known the mind of the Lord? or who hath been made his counselor?”
35 “Au ni nani aliyempa chochote ili arudishiwe?”
or “who first gave to him, and shall receive a return?”
36 Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake, viko kwake na kwa ajili yake. Utukufu ni wake milele! Amen. (aiōn )
For from him, and through him, and to him are all things. To him be the glory for ever! Amen. (aiōn )