< Warumi 11 >
1 Basi nauliza: Je, Mungu amewakataa watu wake? La, hasha! Mimi mwenyewe ni Mwisraeli, tena uzao wa Abrahamu kutoka kabila la Benyamini.
Amaiba: le, na da dilima adole ba: sa, “Gode da Ea fidafa dunu Isala: ili amo yolesila: ?” Hame mabu! Na amola na da Isala: ili dunu. Na da A: ibalaha: me egaga fi dunu amola Bediamini fi amo ganodini esala.
2 Mungu hajawakataa watu wake, ambao yeye aliwajua tangu mwanzo. Je, hamjui yale Maandiko yasemayo kuhusu Eliya, jinsi alivyomlalamikia Mungu kuhusu Israeli?
Gode Ea musa: dunu fi amo E hemonega degabo ilegeiba: le, amo E da hame yolesi. Dilia dawa: - Gode Sia: Dedei amo ganodini, Elaidia da Godema Isala: ili dunu ilia hou olelema: ne amane fofada: i,
3 Alisema, “Bwana, wamewaua manabii wako na kuzibomoa madhabahu zako, nimebaki mimi peke yangu, nao wanataka kuniua?”
“Hina Gode! Amo fi dunu ilia da dia balofede dunu huluane medole legei dagoi. Ilia da Dia oloda huluane ougili mugului dagoi. Nisu fawane da Dia hou hame yolesi. Ilia da na medole legemusa: , logo hogolala.”
4 Je, Mungu alimjibuje? “Nimejibakizia watu elfu saba ambao hawajapiga magoti kumwabudu Baali.”
Be Gode da Elaidiama bu adole i, “Nama hawa: hamomusa: gini, Na da dunu 7000 agoane ilegei dagoi. Disu hame, be ilia huluane da ogogosu ‘gode’ liligi ea dio amo Ba: ile, ema hame sia: ne gadosu.”
5 Vivyo hivyo pia, sasa wapo mabaki waliochaguliwa kwa neema ya Mungu.
Wali, amola agoaiwane hou diala. Isala: ili dunu fi ganodini, wali dunu bagahame ilima Gode da udigili asigiba: le, E da amo dunu Ea hou lalegagumusa: , ili ilegei dagoi.
6 Lakini ikiwa wamechaguliwa kwa neema, si tena kwa msingi wa matendo. Kama ingekuwa kwa matendo, neema isingekuwa neema tena.
Ilia hou moloidafa hamoiba: le hame, be Gode da ilima udigili hahawane asigiba: le fawane, E da ili ilegei. Be Gode da dunu ilia hou moloidafa hamoiba: le ilima ilegei ganiaba, Ea hahawane dogolegele asigi hou da ogogosu udigili asigi hou agoane ba: la: loba.
7 Tuseme nini basi? Kile kitu ambacho Israeli alikitafuta kwa bidii hakukipata. Lakini waliochaguliwa walikipata. Waliobaki walifanywa wagumu,
Isala: ili dunu da ilia hogoi helebeba: le, ilia hanai liligidafa hamedafa ba: i. Be Gode da Isala: ili dunu bagahame fawane, amo ilegei dagoiba: le, E da ili fawane afadenei bu moloidafa hamoi ba: i. Be eno huluane, ilia ge da ga: si agoane hamoiba: le, Gode Ea wele sia: su hame nabi.
8 kama ilivyoandikwa: “Mungu aliwapa bumbuazi la mioyo, macho ili wasiweze kuona, na masikio ili wasiweze kusikia, hadi leo.”
Gode Sia: da agoane dedei diala, “Gode da ilia asigi dawa: su amola ilia dogo dioiwane hamoi. Musa: amola wali, ilia hame ba: sa amola hame naba.”
9 Naye Daudi anasema: “Karamu zao na ziwe tanzi na mtego wa kuwanasa, kitu cha kuwakwaza waanguke, na adhabu kwao.
Gode Sia: Dedei ganodini, Da: ibidi da amane sia: sa, “Ilia lolo nabe amoma masea, ilia sani amo ganodini sa: imu da defea. Ilia dafane, se dabe iasu bagade lamu da defea.
10 Macho yao yatiwe giza ili wasiweze kuona, nayo migongo yao iinamishwe daima.”
Ilia siga mae ba: ma: ne, Dia ilia si wadela: mu da defea. Ilia eso huluane se nababeba: le, dioiwane masunu da defea.”
11 Hivyo nauliza tena: Je, Waisraeli walijikwaa ili waanguke na kuangamia kabisa? La, hasha! Lakini kwa sababu ya makosa yao, wokovu umewafikia watu wa Mataifa, ili kuwafanya Waisraeli waone wivu.
Amaiba: le, na dilima adole ba: sa! Yu dunu ilia sadenane dafabeba: le, ilia dafawane bu mae wa: legadoma: ne dafabela: ? Hame mabu! Ilia wadela: i hou hamoiba: le, Dienadaile dunu da Gode Ea gaga: su hou ba: i dagoi. Amaiba: le Yu dunu da wali mudasu hou ba: sa.
12 Basi ikiwa kukosa kwao kumekuwa utajiri mkubwa kwa ulimwengu, tena kama kuangamia kwao kumeleta utajiri kwa watu wa Mataifa, kurudishwa kwao kutaleta utajiri mkuu zaidi.
Yu dunu da wadela: i hou hamobeba: le, Gode Ea hahawane dogolegele iasu da eno osobo bagade fifi asi gala dunuma doaga: i dagoi. Yu dunu da a: silibu hou hame gagui agoane esalebeba: le, Dienadaile dunu da Gode Ea hahawane hou ba: i. Amaiba: le, Yu dunu huluane ilia Yesu Ea fa: no bobogesu fi amo ganodini masea, ninia huluane da Gode Ea hahawane dogolegesu hou baligiliwane ba: mu.
13 Sasa ninasema nanyi watu wa Mataifa. Maadamu mimi ni mtume kwa watu wa Mataifa, naitukuza huduma yangu
Na da wali dili Dienadaile dunuma sia: sa. Gode da na dili Dienadaile dunuma asunasiba: le, na da na hawa: hamosu asigiwane hidale ba: sa.
14 ili kuwafanya watu wangu waone wivu na hivyo kuwaokoa baadhi yao.
Na sia: beba: le, amabela: ? Na fi Isala: ili dunu ilia mudale, mogili ilia Gode Ea hou lalegaguma: bela: ?
15 Kwa kuwa ikiwa kukataliwa kwao ni kupatanishwa kwa ulimwengu, kukubaliwa kwao si kutakuwa ni uhai baada ya kufa?
Bai Gode da Isala: ili fi yolesiba: le, eno fi dunu huluane musa: Ema ha lai esalu e da bu yosia: le, Ea na: iyado dunu fi hamoi dagoi. Amaiba: le, Gode da Isala: ili dunu fi bu yosia: sea, hou da bogoi bu wa: legadosu agoane ba: mu.
16 Kama sehemu ya donge la unga uliotolewa kuwa limbuko ni mtakatifu, basi unga wote ni mtakatifu, nalo shina kama ni takatifu, vivyo hivyo na matawi nayo.
Dunu da agi fifili, degabo fonobahadi liligi Godema iasea, agi huluane da Gode Ea agi dawa: ma. Ifa gagui galea, di da amo ea difi Godema iasea, amo ifa ea amoda amola da Gode Ea:
17 Lakini kama baadhi ya matawi yalikatwa, nawe chipukizi la mzeituni mwitu ukapandikizwa mahali pao ili kushiriki unono pamoja na matawi mengine kutoka shina la mzeituni,
Gode da fedege agoane, ea ifabi ganodini bugi olife ifa amo ea amoda mogili dadamuni, eno olife udigili iwilaga lelu liligi amo bugi ifaga madelagimusa: sali. Dilia Dienadaile dunu da amo iwilaga dialu olife ifa agoane. Dilia da wali Yu dunu ilia gasa bagade a: silibu esalusu gilisili gagusa.
18 basi usijivune juu ya hayo matawi. Kama ukijivuna, kumbuka jambo hili: si wewe unayelishikilia shina, bali ni shina linalokushikilia wewe.
Amaiba: le, musa: olife ifadafa ea amoda, Gode da dadamuni fasi, amo dilia higale mae ba: ma. Dilia gasa fi hamomu da hamedei. Dilia da amoda fawane. Dilia da difi amoma ha: i manu hame iaha. Difi da dili alema: ne, dilima ha: i manu iaha.
19 Basi utasema, “Matawi yale yalikatwa ili nipate kupandikizwa katika hilo shina.”
Be dilia da amane sia: mu, “Dafawane! Be Gode da ninima ilia sogebi ima: ne, musa: amoda dadamuni fasi dagoi.”
20 Hii ni kweli. Matawi hayo yalikatwa kwa sababu ya kutokuamini kwake, lakini wewe umesimama tu kwa sababu ya imani. Kwa hiyo usijivune, bali simama kwa kuogopa.
Amo da dafawane! Ilia da dafawaneyale hame dawa: beba: le, Gode da ili dadamuni fasi. Dilia da dafawaneyale dawa: beba: le, wali ifadafa ganodini esala. Be amo dawa: beba: le, hidale gasa fi hou mae hamoma. Dilia beda: mu da defea.
21 Kwa maana kama Mungu hakuyahurumia matawi ya asili, wala hatakuhurumia wewe.
Yu dunu da fedege agoane amodadafa galu. Be amo da dafaiba: le, Gode da fadegale fasi. Amaiba: le dawa: ma! Dilia amola e da fadegasa: besa: le, dawa: ma!
22 Angalia basi wema na ukali wa Mungu: Kwa wale walioanguka, ukali, bali kwako wewe wema wa Mungu, kama utadumu katika wema wake. La sivyo, nawe utakatiliwa mbali.
Ninia da amo hou ganodini, Gode Ea asigi hou amola Gode Ea ougi fofada: su hou gilisili ba: sa. E da wadela: i hou hamosu dafai dunuma ougi fofada: su olelesa. Be dilia Ea asigi gogolema: ne olofosu hou dawa: le, mae yolesili Ema fa: no bobogolalea, e da dilima asigilalumu. Be dilia da amo hou yolesisia, E da dili amola dadamuni fasimu.
23 Wao nao wasipodumu katika kutokuamini kwao, watapandikizwa tena kwenye shina, kwa maana Mungu anao uwezo wa kuwapandikiza tena kwenye hilo shina.
Amola Yu dunu ilia bu dafawaneyale dawa: sea, Gode da ilia musa: sogebi amo ganodini bu madelagima: ne salimu. Bai Gode da amo hou hamomusa: defele esala.
24 Ikiwa wewe ulikatwa kutoka kile ambacho kwa asili ni mzeituni mwitu na kupandikizwa kinyume cha asili kwenye mzeituni uliopandwa, si rahisi zaidi matawi haya ya asili kupandikizwa tena kwenye shina lake la mzeituni!
Dilia Dienadaile dunu da fedege agoane udigili iwilaga dialu olife ifa ea amoda. Gode da dili dadamuni, ifabi bugi olife ifa amoga madelagi dagoi. Be Yu dunu da ifabi amoga bugi olife ifa ea fedege agoane gala. Amaiba: le, amo amoda liligi Godema dadamuni fasi liligi, e da bu ifadafa amoga madelagimusa: dawa: sea, asaboiwane ba: mu. Ilia da hedolowane bu madelagimu.
25 Ndugu zangu, ili msije mkajidai kuwa wenye hekima kuliko mlivyo, nataka mfahamu siri hii: Ugumu umewapata Israeli kwa sehemu hadi idadi ya watu wa Mataifa watakaoingia itimie.
Na fi dunu! Na da dafawane wamolegei sia: dilima olelemu hanai gala. Amo nabasea, dili bu dilia dawa: su hou da bagadeyale hame dawa: mu. Isala: ili fi dunu ilia dogo da igiwane hamoi, be amo hou da eso huluane hame dialumu. Be Dienadaile dunu ilia gilisisu ilegei idi Gode da ilegei, amo defele ilia Gode Ea hou lalegagui dagoi ba: sea, Isala: ili dunu ilia hihi hou da yolesiwane ba: mu.
26 Hivyo Israeli wote wataokolewa. Kama ilivyoandikwa: “Mkombozi atakuja kutoka Sayuni; ataondoa kutokumcha Mungu katika Yakobo.
Amalalu, Isala: ili fi dunu huluane ilia Gode Ea gaga: su hou ba: mu. Gode Sia: da amane dedei diala, “Gaga: su Dunu da Saione amoga misini, E da Ya: igobe ea mano huluane ilia wadela: i hou huluane fadegale fasimu.
27 Hili ndilo agano langu nao nitakapoziondoa dhambi zao.”
Na da ilia wadela: i hou gogolema: ne olofosea, amo gousa: su ilima hamomu.”
28 Kwa habari ya Injili, wao ni adui wa Mungu kwa ajili yenu, lakini kuhusu kule kuteuliwa kwao ni wapendwa, kwa ajili ya mababa zao wa zamani,
Yu dunu da Gode Sia: Ida: iwane Gala higabeba: le, ilia Godema ha laiwane hamoi, be dilia Dienadaile dunu fidima: ne amo hou da doaga: i. Be Gode da ilia siba fi ilima Ea ilegei dagoiba: le, ilia da Ea fi dunu esala.
29 kwa maana akishawapa watu karama, Mungu haziondoi, wala wito wake.
Gode da Ea hanaiga dunu fi ilegesa amola ilima hahawane iaha. Amola E da Ea asigi dawa: su hame afadenesa.
30 Kama vile ninyi wakati fulani mlivyokuwa waasi kwa Mungu lakini sasa mmepata rehema kwa sababu ya kutokutii kwao,
Be dilia Dienadaile dunu! Dilia da musa: Gode Ea Sia: hame nabasu. Be Yu dunu ilia hame nabasu hou hamobeba: le, dilia wali Gode Ea gogolema: ne olofosu dawa:
31 hivyo nao Waisraeli wamekuwa waasi ili kwamba wao nao sasa waweze kupata rehema kwa ajili ya rehema za Mungu kwenu.
Amo hou defele, dilia da wali gogolema: ne olofosu dawa: beba: le, Yu fi dunu da wali hame nabasu hou hamonana. Bai ilia da hobea Gode Ea gogolema: ne olofosu ba: ma: ne, agoane hamosa.
32 Kwa maana Mungu amewafunga wanadamu wote kwenye kuasi ili apate kuwarehemu wote. (eleēsē )
Gode da dunu huluanedafa ilima Ea udigili gogolema: ne olofosu hou olelema: ne, E da dunu huluane hame nabasu se iasu udigili hawa: hamosu dunu agoane hamoi dagoi. (eleēsē )
33 Tazama jinsi kilivyo kina cha utajiri wa hekima na maarifa ya Mungu! Tazama jinsi ambavyo hukumu zake hazichunguziki, na ambavyo njia zake zisivyotafutikana!
Gode Ea gagui hou da bagadedafa. Ea asigi dawa: su amola Ea hamonanebe dawa: su hou da baligiliwane bagade. Ea hou hamoi nowa da dawa: ma: bela: ? Ea logoga ahoanebe hou da dawa: mu hamedei.
34 “Ni nani aliyeyafahamu mawazo ya Bwana? Au ni nani ambaye amekuwa mshauri wake?”
Gode Sia: da agoane dedei diala, “Nowa da Hina Gode Ea asigi dawa: su dawa: sala: ? Nowa da Ema fada: i sia: olelema: bela: ?
35 “Au ni nani aliyempa chochote ili arudishiwe?”
Nowa da Godema dabe bu lama: ne liligi iabela: ?”
36 Kwa maana vitu vyote vyatoka kwake, viko kwake na kwa ajili yake. Utukufu ni wake milele! Amen. (aiōn )
Bai E da liligi huluanedafa hahamoi dagoi. E hahawane ba: ma: ne, liligi huluanedafa diala. Ninia Godema mae yolesili nodonanumu da defea. Ama. (aiōn )