< Warumi 10 >

1 Ndugu zangu, shauku ya moyo wangu na maombi yangu kwa Mungu ni kwa ajili ya Waisraeli, kwamba waokolewe.
Frères, le désir de mon cœur et la prière que j'adresse à Dieu concernent Israël, afin qu'il soit sauvé.
2 Kwa maana ninaweza nikashuhudia wazi kwamba wao wana juhudi kubwa kwa ajili ya Mungu, lakini juhudi yao haina maarifa.
Car je témoigne à leur sujet qu'ils ont un zèle pour Dieu, mais non selon la connaissance.
3 Kwa kuwa hawakuijua haki itokayo kwa Mungu, wakatafuta kuweka haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu.
Car, ignorant la justice de Dieu, et cherchant à établir leur propre justice, ils ne se sont pas soumis à la justice de Dieu.
4 Kwa maana Kristo ni ukomo wa sheria ili kuwe na haki kwa kila mtu aaminiye.
Car Christ est l'accomplissement de la loi pour la justice de quiconque croit.
5 Mose anaandika kuhusu haki ile itokanayo na sheria, kwamba, “Mtu atendaye matendo hayo ataishi kwa hayo.”
Car Moïse écrit au sujet de la justice de la loi: « Celui qui les met en pratique vivra par elles. »
6 Lakini ile haki itokanayo na imani husema hivi: “Usiseme moyoni mwako, ‘Ni nani atakayepanda mbinguni?’” (yaani ili kumleta Kristo chini)
Mais la justice de la foi dit ceci: « Ne dis pas en ton cœur: « Qui montera au ciel? (c'est-à-dire de faire descendre le Christ);
7 “au ‘Ni nani atashuka kwenda kuzimu?’” (yaani ili kumleta Kristo kutoka kwa wafu.) (Abyssos g12)
ou bien: « Qui descendra dans l'abîme? (c'est-à-dire de faire remonter le Christ d'entre les morts.)" (Abyssos g12)
8 Lakini andiko lasemaje? “Lile neno liko karibu nawe, liko kinywani mwako na moyoni mwako,” yaani, lile neno la imani tunalolihubiri.
Mais que dit-il? « La parole est près de toi, dans ta bouche et dans ton cœur », c'est-à-dire la parole de la foi que nous prêchons:
9 Kwa sababu kama ukikiri kwa kinywa chako kwamba “Yesu ni Bwana,” na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokoka.
que si tu confesses de ta bouche que Jésus est Seigneur et si tu crois dans ton cœur que Dieu l'a ressuscité des morts, tu seras sauvé.
10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini na hivyo kuhesabiwa haki, tena kwa kinywa mtu hukiri na hivyo kupata wokovu.
Car c'est du cœur qu'on croit, ce qui entraîne la justice, et de la bouche qu'on confesse, ce qui entraîne le salut.
11 Kama yasemavyo Maandiko, “Yeyote amwaminiye hataaibika kamwe.”
Car l'Écriture dit: « Celui qui croit en lui ne sera pas déçu. »
12 Kwa maana hakuna tofauti kati ya Myahudi na Myunani, yeye ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao.
En effet, il n'y a pas de distinction entre le Juif et le Grec, car le même Seigneur est le Seigneur de tous, et il est riche pour tous ceux qui l'invoquent.
13 Kwa maana, “Kila mtu atakayeliitia Jina la Bwana, ataokolewa.”
En effet, « Quiconque invoquera le nom du Seigneur sera sauvé. »
14 Lakini watamwitaje yeye ambaye hawajamwamini? Nao watawezaje kumwamini yeye ambaye hawajamsikia? Tena watamsikiaje bila mtu kuwahubiria?
Comment donc invoqueront-ils celui en qui ils n'ont pas cru? Comment croiront-ils en celui qu'ils n'ont pas entendu? Comment entendront-ils sans prédicateur?
15 Nao watahubirije wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, “Tazama jinsi ilivyo mizuri miguu yao wale wanaohubiri habari njema!”
Et comment prêcheront-ils sans être envoyés? Comme il est écrit: « Qu'ils sont beaux les pieds de ceux qui annoncent la Bonne Nouvelle de la paix, qui apporte des nouvelles heureuses de bonnes choses! »
16 Lakini si wote waliotii Habari Njema. Kwa maana Isaya asema, “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu?”
Mais ils n'ont pas tous écouté l'heureuse nouvelle. Car Ésaïe dit: « Seigneur, qui a cru à notre rapport? »
17 Basi, imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la Kristo.
Ainsi, la foi vient de l'ouïe, et l'ouïe de la parole de Dieu.
18 Lakini nauliza: Je, wao hawakusikia? Naam, wamesikia, kwa maana: “Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu.”
Mais, dis-je, n'ont-ils pas entendu? Oui, très certainement, « Leur son s'est répandu dans toute la terre, leurs paroles jusqu'aux extrémités du monde. »
19 Nami nauliza tena: Je, Waisraeli hawakuelewa? Kwanza, Mose asema, “Nitawafanya mwe na wivu kwa watu wale ambao si taifa. Nitawakasirisha kwa taifa lile lisilo na ufahamu.”
Mais je demande: Israël ne le savait-il pas? D'abord Moïse dit, « Je vous provoquerai à la jalousie avec ce qui n'est pas une nation. Je te mettrai en colère contre une nation dépourvue d'intelligence. »
20 Naye Isaya kwa ujasiri mwingi anasema, “Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta. Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakunitafuta.”
Ésaïe est très audacieux et dit, « J'ai été trouvé par ceux qui ne m'avaient pas cherché. J'ai été révélé à ceux qui ne m'avaient pas demandé. »
21 Lakini kuhusu Israeli anasema, “Mchana kutwa nimewanyooshea watu wakaidi na wasiotii mikono yangu.”
Mais à propos d'Israël, il dit: « Tout le jour, j'ai tendu mes mains vers un peuple désobéissant et rebelle. »

< Warumi 10 >