< Warumi 10 >
1 Ndugu zangu, shauku ya moyo wangu na maombi yangu kwa Mungu ni kwa ajili ya Waisraeli, kwamba waokolewe.
Brethren, indeed the desire of my heart and my prayer to God in their behalf, is for their salvation.
2 Kwa maana ninaweza nikashuhudia wazi kwamba wao wana juhudi kubwa kwa ajili ya Mungu, lakini juhudi yao haina maarifa.
For I testify to them, that they have a zeal of God, but not according to perfect knowledge;
3 Kwa kuwa hawakuijua haki itokayo kwa Mungu, wakatafuta kuweka haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu.
for being ignorant of God's righteousness, and seeking to establish their own righteousness, they have not submitted to the righteousness of God.
4 Kwa maana Kristo ni ukomo wa sheria ili kuwe na haki kwa kila mtu aaminiye.
For Christ is the end of the law unto righteousness to every one who believes.
5 Mose anaandika kuhusu haki ile itokanayo na sheria, kwamba, “Mtu atendaye matendo hayo ataishi kwa hayo.”
For Moses describes the righteousness which is of the law, that the man having done this shall live in it.
6 Lakini ile haki itokanayo na imani husema hivi: “Usiseme moyoni mwako, ‘Ni nani atakayepanda mbinguni?’” (yaani ili kumleta Kristo chini)
But the righteousness of faith speaks thus, Say not in thy heart, Who shall ascend up into heaven? that is, to bring Christ down:
7 “au ‘Ni nani atashuka kwenda kuzimu?’” (yaani ili kumleta Kristo kutoka kwa wafu.) (Abyssos )
or, Who shall descend into the abyss? that is, to bring him up from the dead. (Abyssos )
8 Lakini andiko lasemaje? “Lile neno liko karibu nawe, liko kinywani mwako na moyoni mwako,” yaani, lile neno la imani tunalolihubiri.
But what says it? The word is nigh thee, in thy mouth, and in thy heart: that is, the word of faith, which we preach.
9 Kwa sababu kama ukikiri kwa kinywa chako kwamba “Yesu ni Bwana,” na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokoka.
That if you may confess with your mouth the Lord Jesus, and may believe with your heart that God raised him from the dead, you shall be saved:
10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini na hivyo kuhesabiwa haki, tena kwa kinywa mtu hukiri na hivyo kupata wokovu.
for with the heart it is believed unto righteousness; and with the mouth it is confessed unto salvation.
11 Kama yasemavyo Maandiko, “Yeyote amwaminiye hataaibika kamwe.”
For the scripture says, Every one believing on him shall not be ashamed.
12 Kwa maana hakuna tofauti kati ya Myahudi na Myunani, yeye ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao.
For there is no difference between Jew and Greek: for the same is Lord of all, rich unto all that call on him.
13 Kwa maana, “Kila mtu atakayeliitia Jina la Bwana, ataokolewa.”
For every one who may call on the name of the Lord shall be saved.
14 Lakini watamwitaje yeye ambaye hawajamwamini? Nao watawezaje kumwamini yeye ambaye hawajamsikia? Tena watamsikiaje bila mtu kuwahubiria?
Then how can they call on him on whom they have not believed? and how can they believe on him of whom they have not heard? and how shall they hear without a preacher?
15 Nao watahubirije wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, “Tazama jinsi ilivyo mizuri miguu yao wale wanaohubiri habari njema!”
And how can they preach, unless they may be sent forth? as has been written, How beautiful are the feet of those, who preach the gospel of good things!
16 Lakini si wote waliotii Habari Njema. Kwa maana Isaya asema, “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu?”
But they have not all heard the gospel. For Isaiah says, Lord, who has believed our report?
17 Basi, imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la Kristo.
Then faith comes by hearing, and hearing by the word of Christ.
18 Lakini nauliza: Je, wao hawakusikia? Naam, wamesikia, kwa maana: “Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu.”
But I say, Have they not all heard? Yea, truly, Their sound has gone out into all the earth, and their words unto the ends of the world.
19 Nami nauliza tena: Je, Waisraeli hawakuelewa? Kwanza, Mose asema, “Nitawafanya mwe na wivu kwa watu wale ambao si taifa. Nitawakasirisha kwa taifa lile lisilo na ufahamu.”
But I say, Whether does not Israel know? Moses first says, I will provoke you to jealousy with that which is no nation, and with a nation void of understanding I will anger you.
20 Naye Isaya kwa ujasiri mwingi anasema, “Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta. Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakunitafuta.”
But Isaiah is bold, and says, I was found by those not seeking after me; and made manifest to those not inquiring after me.
21 Lakini kuhusu Israeli anasema, “Mchana kutwa nimewanyooshea watu wakaidi na wasiotii mikono yangu.”
But to Israel he says, All day long have I reached forth my hands to a gainsaying and disobedient people.