< Warumi 10 >

1 Ndugu zangu, shauku ya moyo wangu na maombi yangu kwa Mungu ni kwa ajili ya Waisraeli, kwamba waokolewe.
Brothers, my heart's desire and prayer to God for Israel is for their salvation.
2 Kwa maana ninaweza nikashuhudia wazi kwamba wao wana juhudi kubwa kwa ajili ya Mungu, lakini juhudi yao haina maarifa.
For I bear them witness that they have a zeal for God, but not according to real knowledge.
3 Kwa kuwa hawakuijua haki itokayo kwa Mungu, wakatafuta kuweka haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu.
For they, failing to understand God's righteousness and seeking to establish their own righteousness, have not submitted to God's righteousness.
4 Kwa maana Kristo ni ukomo wa sheria ili kuwe na haki kwa kila mtu aaminiye.
Now for everyone who believes into righteousness, Christ is the end of the law
5 Mose anaandika kuhusu haki ile itokanayo na sheria, kwamba, “Mtu atendaye matendo hayo ataishi kwa hayo.”
—Moses writes about the righteousness that is from the law: “The person who does these things will live by them.”
6 Lakini ile haki itokanayo na imani husema hivi: “Usiseme moyoni mwako, ‘Ni nani atakayepanda mbinguni?’” (yaani ili kumleta Kristo chini)
But the righteousness that is from faith speaks like this: “Do not say in your heart, ‘Who will ascend into heaven?’” (that is, to bring Christ down)
7 “au ‘Ni nani atashuka kwenda kuzimu?’” (yaani ili kumleta Kristo kutoka kwa wafu.) (Abyssos g12)
“or, ‘Who will descend into the abyss?’” (that is, to bring Christ up from the dead). (Abyssos g12)
8 Lakini andiko lasemaje? “Lile neno liko karibu nawe, liko kinywani mwako na moyoni mwako,” yaani, lile neno la imani tunalolihubiri.
So what does it say? “The message is near you, in your mouth and in your heart” (that is, the message of faith that we proclaim):
9 Kwa sababu kama ukikiri kwa kinywa chako kwamba “Yesu ni Bwana,” na kuamini moyoni mwako kwamba Mungu alimfufua kutoka kwa wafu, utaokoka.
That if you confess with your mouth, “Jesus is Lord,” and believe in your heart that God raised Him from the dead, you will be saved.
10 Kwa maana kwa moyo mtu huamini na hivyo kuhesabiwa haki, tena kwa kinywa mtu hukiri na hivyo kupata wokovu.
Because with the heart one believes into righteousness, and with the mouth one promises into salvation.
11 Kama yasemavyo Maandiko, “Yeyote amwaminiye hataaibika kamwe.”
Because the Scripture says: “Everyone who believes on Him will never be put to shame”;
12 Kwa maana hakuna tofauti kati ya Myahudi na Myunani, yeye ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao.
because there is no distinction between Jew and Greek, since the same Lord of all is rich to all who call upon Him;
13 Kwa maana, “Kila mtu atakayeliitia Jina la Bwana, ataokolewa.”
because: “Everyone who calls on the name of the Lord will be saved.”
14 Lakini watamwitaje yeye ambaye hawajamwamini? Nao watawezaje kumwamini yeye ambaye hawajamsikia? Tena watamsikiaje bila mtu kuwahubiria?
How then will they call on Him in whom they have not believed? And how can they believe on Him of whom they have not heard? And how will they hear without someone proclaiming it?
15 Nao watahubirije wasipopelekwa? Kama ilivyoandikwa, “Tazama jinsi ilivyo mizuri miguu yao wale wanaohubiri habari njema!”
And how will they proclaim unless they are sent? As it is written: “How timely is the arrival of those who bring good news of peace, of those who announce the good things.”
16 Lakini si wote waliotii Habari Njema. Kwa maana Isaya asema, “Bwana, ni nani aliyeamini ujumbe wetu?”
(However, they did not all obey the gospel; because Isaiah says: “Lord, who has believed our message?”)
17 Basi, imani chanzo chake ni kusikia, na kusikia huja kwa neno la Kristo.
So, the faith is from a message, and that message is by the Word of God.
18 Lakini nauliza: Je, wao hawakusikia? Naam, wamesikia, kwa maana: “Sauti yao imeenea duniani pote, nayo maneno yao yameenea hadi miisho ya ulimwengu.”
But I say, did they really not hear? Indeed yes: “Their voice has gone out into all the earth, and their spoken words to the ends of the inhabited world.”
19 Nami nauliza tena: Je, Waisraeli hawakuelewa? Kwanza, Mose asema, “Nitawafanya mwe na wivu kwa watu wale ambao si taifa. Nitawakasirisha kwa taifa lile lisilo na ufahamu.”
Again I say, did Israel really not know? First Moses says: “I will provoke you to jealousy by a non-nation, I will move you to anger by a senseless nation.”
20 Naye Isaya kwa ujasiri mwingi anasema, “Nimeonekana na watu wale ambao hawakunitafuta. Nilijifunua kwa watu wale ambao hawakunitafuta.”
But Isaiah is so bold as to say: “I was found by those who were not seeking me; I was revealed to those who were not asking for me.”
21 Lakini kuhusu Israeli anasema, “Mchana kutwa nimewanyooshea watu wakaidi na wasiotii mikono yangu.”
But concerning Israel he says: “All day long I have held out my hands to a disobedient and contrary people.”

< Warumi 10 >