< Warumi 1 >
1 Paulo, mtumishi wa Kristo Yesu, aliyeitwa kuwa mtume na kutengwa kwa ajili ya Injili ya Mungu,
Paul, a servant of Jesus Christ, a called apostle, having been separated to the good news of God,
2 Injili ambayo Mungu alitangulia kuiahidi kwa vinywa vya manabii wake katika Maandiko Matakatifu,
which He announced before through His prophets in holy writings,
3 yaani, Injili inayomhusu Mwanawe, yeye ambaye kwa uzao wa mwili alikuwa mzao wa Daudi,
concerning His Son—who has come of the seed of David according to the flesh,
4 na ambaye kwa uwezo wa Roho wa utakatifu alidhihirishwa kuwa Mwana wa Mungu kwa ufufuo wake kutoka kwa wafu, yaani, Yesu Kristo, Bwana wetu.
who is marked out [as the] Son of God in power, according to the Spirit of sanctification, by the resurrection from the dead—Jesus Christ our Lord;
5 Kwa kupitia kwake na kwa ajili ya Jina lake, tumepokea neema na utume ili kuwaita watu miongoni mwa watu wa mataifa yote, waje kwenye utii utokanao na imani.
through whom we received grace and apostleship, for obedience of faith among all the nations, in behalf of His Name;
6 Ninyi nyote pia mko miongoni mwa watu walioitwa ili mpate kuwa mali ya Yesu Kristo.
among whom are also you, the called of Jesus Christ;
7 Kwa wote walioko Rumi wapendwao na Mungu na kuitwa kuwa watakatifu: Neema na amani itokayo kwa Mungu Baba yetu na kwa Bwana wetu Yesu Kristo iwe nanyi.
to all who are in Rome, beloved of God, called holy ones: Grace to you and peace from God our Father and the Lord Jesus Christ!
8 Kwanza kabisa, namshukuru Mungu wangu kwa njia ya Yesu Kristo kwa ajili yenu nyote, kwa sababu imani yenu inatangazwa duniani kote.
First, indeed, I thank my God through Jesus Christ for you all, that your faith is proclaimed in the whole world;
9 Kwa maana Mungu ninayemtumikia kwa moyo wangu wote katika kuhubiri Injili ya Mwanawe, ni shahidi wangu jinsi ninavyowakumbuka
for God is my witness, whom I serve in my spirit in the good news of His Son, how unceasingly I make mention of you,
10 katika maombi yangu siku zote, nami ninaomba kwamba hatimaye sasa kwa mapenzi ya Mungu, njia ipate kufunguliwa kwa ajili yangu ili nije kwenu.
always in my prayers imploring, if by any means now at length I will have a prosperous journey, by the will of God, to come to you,
11 Ninatamani sana kuwaona ili nipate kuweka juu yenu karama za rohoni ili mwe imara,
for I long to see you, that I may impart to you some spiritual gift, that you may be established;
12 au zaidi, ninyi pamoja nami tuweze kutiana moyo katika imani sisi kwa sisi.
and that is, that I may be comforted together among you, through faith in one another, both yours and mine.
13 Ndugu zangu, napenda mfahamu kwamba mara nyingi nimekusudia kuja kwenu (ingawa mpaka sasa nimezuiliwa), ili nipate kuvuna mavuno miongoni mwenu kama nilivyovuna miongoni mwa wengine ambao ni watu wa Mataifa wasiomjua Mungu.
And I do not wish you to be ignorant, brothers, that many times I purposed to come to you—and was hindered until the present time—that some fruit I might have also among you, even as also among the other nations.
14 Mimi ni mdeni kwa Wayunani na kwa wasio Wayunani, kwa wenye hekima na kwa wasio na hekima.
Both to Greeks and to foreigners, both to wise and to thoughtless, I am a debtor,
15 Ndiyo sababu ninatamani sana kuihubiri Injili kwenu pia ninyi mlioko Rumi.
so, as much as in me is, I am ready also to you who [are] in Rome to proclaim good news,
16 Mimi siionei haya Injili ya Kristo kwa maana ni uweza wa Mungu uletao wokovu kwa kila aaminiye, kwanza kwa Myahudi na kwa Myunani pia.
for I am not ashamed of the good news of the Christ, for it is the power of God to salvation to everyone who is believing, both to Jew first, and to Greek.
17 Kwa maana katika Injili haki itokayo kwa Mungu imedhihirishwa, haki ile iliyo kwa njia ya imani hadi imani. Kama ilivyoandikwa: “Mwenye haki ataishi kwa imani.”
For the righteousness of God in it is revealed from faith to faith, according as it has been written: “And the righteous one will live by faith,”
18 Ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni dhidi ya uasi wote na uovu wa wanadamu ambao huipinga kweli kwa uovu wao,
for the wrath of God is revealed from Heaven on all impiety and unrighteousness of men, holding down the truth in unrighteousness.
19 kwa maana yote yanayoweza kujulikana kumhusu Mungu ni dhahiri kwao, kwa sababu Mungu mwenyewe ameyadhihirisha kwao.
Because that which is known of God is revealed among them, for God revealed [it] to them,
20 Kwa maana tangu kuumbwa kwa ulimwengu, asili ya Mungu asiyeonekana kwa macho, yaani, uweza wake wa milele na asili yake ya Uungu, imeonekana waziwazi, ikitambuliwa kutokana na yale aliyoyafanya ili wanadamu wasiwe na udhuru. (aïdios )
for the invisible things of Him from the creation of the world, by the things made being understood, are plainly seen, both His eternal power and Godhead—to their being inexcusable; (aïdios )
21 Kwa maana ingawa walimjua Mungu, hawakumtukuza yeye kama ndiye Mungu wala hawakumshukuru, bali fikira zao zimekuwa batili na mioyo yao ya ujinga ikatiwa giza.
because, having known God they did not glorify [Him] as God, nor gave thanks, but were made vain in their reasonings, and their unintelligent heart was darkened,
22 Ingawa walijidai kuwa wenye hekima, wakawa wajinga
professing to be wise, they were made fools,
23 na kubadili utukufu wa Mungu aishiye milele kwa sanamu zilizofanywa zifanane na mwanadamu ambaye hufa, na mfano wa ndege, wanyama na viumbe vitambaavyo.
and changed the glory of the incorruptible God into the likeness of an image of corruptible man, and of birds, and of quadrupeds, and of reptiles.
24 Kwa hiyo, Mungu akawaacha wazifuate tamaa mbaya za mioyo yao katika uasherati, hata wakavunjiana heshima miili yao wao kwa wao.
For this reason also God gave them up, in the desires of their hearts, to uncleanness, to dishonor their bodies among themselves;
25 Kwa sababu waliibadili kweli ya Mungu kuwa uongo, wakaabudu na kutumikia kiumbe badala ya Muumba, ahimidiwaye milele! Amen. (aiōn )
who changed the truth of God into the lie, and honored and served the creature rather than the Creator, who is blessed for all ages. Amen. (aiōn )
26 Kwa sababu hii, Mungu aliwaacha wavunjiane heshima kwa kufuata tamaa zao za aibu. Hata wanawake wao wakabadili matumizi ya asili ya miili yao wakaitumia isivyokusudiwa.
Because of this God gave them up to dishonorable affections, for even their females changed the natural use into that against nature;
27 Vivyo hivyo wanaume pia wakiacha matumizi ya asili ya wanawake wakawakiana tamaa wao kwa wao. Wanaume wakafanyiana matendo ya aibu na wanaume wengine nao wakapata katika maisha yao adhabu iliyowastahili kwa ajili ya upotovu wao.
and in like manner also the males having left the natural use of the female, burned in their longing toward one another; males with males working shame, and the repayment of their error that was fit, in themselves receiving.
28 Nao kwa kuwa hawakuona umuhimu wa kudumisha ufahamu wa Mungu, yeye akawaachilia wafuate akili za upotovu, watende mambo yale yasiyostahili kutendwa.
And according as they did not approve of having God in knowledge, God gave them up to a disapproved mind, to do the things not seemly;
29 Wakiwa wamejawa na udhalimu wa kila namna, uasherati, uovu, tamaa mbaya na hila. Wamejawa na husuda, uuaji, ugomvi, udanganyifu, hadaa na nia mbaya. Wao pia ni wasengenyaji,
having been filled with all unrighteousness, whoredom, wickedness, covetousness, malice; full of envy, murder, strife, deceit, evil dispositions; whisperers,
30 wasingiziaji, wanaomchukia Mungu, wajeuri, wenye kiburi na majivuno, wenye hila, wasiotii wazazi wao,
evil-speakers, God-haters, insulting, proud, boasters, inventors of evil things, disobedient to parents,
31 wajinga, wasioamini, wasio na huruma na wakatili.
unintelligent, faithless, without natural affection, implacable, unmerciful;
32 Ingawa wanafahamu sheria ya haki ya Mungu kwamba watu wanaofanya mambo kama hayo wanastahili mauti, si kwamba wanaendelea kutenda hayo tu, bali pia wanakubaliana na wale wanaoyatenda.
who the righteous judgment of God having known—that those practicing such things are worthy of death—not only do them, but also have delight with those practicing them.