< Ufunuo 1 >
1 Ufunuo wa Yesu Kristo aliopewa na Mungu ili awaonyeshe watumishi wake mambo ambayo ni lazima yatukie hivi karibuni. Alijulisha mambo haya kwa kumtuma malaika wake kwa Yohana mtumishi wake,
This is the Revelation of Jesus Christ, which God gave him to show his servants what will happen soon. He sent his angel to reveal it to his servant John
2 ambaye anashuhudia kuhusu kila kitu alichokiona, yaani, Neno la Mungu na ushuhuda wa Yesu Kristo.
who confirmed everything he saw concerning the word of God and the testimony of Jesus Christ.
3 Amebarikiwa yeye asomaye maneno ya unabii huu, na wamebarikiwa wale wanaoyasikia na kuyatia moyoni yale yaliyoandikwa humo, kwa sababu wakati umekaribia.
Anyone who reads this is blessed, as are those who hear these prophetic words and pay attention to what's written, because the time is near.
4 Yohana, kwa makanisa saba yaliyoko Asia: Neema na amani iwe kwenu kutoka kwake aliyeko, aliyekuwako na atakayekuja, na kutoka kwa wale roho saba walioko mbele ya kiti chake cha enzi,
This letter comes from John and is sent to the seven churches in the province of Asia. May you have grace and peace from the one who was, who is, and who is to come, and from the seven Spirits before his throne,
5 na kutoka kwa Yesu Kristo ambaye ni yule shahidi mwaminifu, mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu, mtawala wa wafalme wa dunia. Kwake yeye anayetupenda na ambaye ametuweka huru kutoka dhambi zetu kwa damu yake,
and from Jesus Christ the trustworthy witness, the firstborn from the dead, the ruler of earthly kings. To Jesus who loves us and freed us from our sins by his blood,
6 akatufanya sisi kuwa ufalme na makuhani, tumtumikie Mungu wake ambaye ni Baba yake. Utukufu na uwezo ni vyake milele na milele! Amen. (aiōn )
who made us into his kingdom, priests to his God and Father—to Jesus be glory and authority for ever and ever. Amen. (aiōn )
7 Tazama! Anakuja na mawingu, na kila jicho litamwona, hata wale waliomchoma; na makabila yote duniani yataomboleza kwa sababu yake. Naam, ndivyo itakavyokuwa! Amen.
Look, he is coming surrounded by clouds, and everybody shall see him, even those who killed him. All the peoples of the earth will weep because of him. May it be so! Amen.
8 “Mimi ni Alfa na Omega,” asema Bwana Mungu, “aliyeko, aliyekuwako na atakayekuja, Mwenyezi.”
“I am the Beginning and the End,” says the All-powerful Lord God, who was, who is, and who is to come.
9 Mimi, Yohana, ndugu yenu ninayeshiriki pamoja nanyi mateso katika Yesu na katika ufalme na uvumilivu katika saburi, nilikuwa katika kisiwa cha Patmo kwa ajili ya neno la Mungu na ushuhuda wa Yesu.
I am John, your brother who shares with you in the suffering and in the kingdom and in the patient waiting that are our experience in Jesus. I was detained on the island of Patmos for sharing the word of God and the truth as revealed by Jesus.
10 Katika siku ya Bwana, nilikuwa katika Roho na nikasikia sauti kubwa kama ya baragumu nyuma yangu
I was filled by the Spirit on the Lord's day, and I heard a loud voice behind me that sounded like a trumpet.
11 ikisema, “Andika kwenye kitabu haya yote unayoyaona, kisha uyapeleke kwa makanisa saba, yaani: Efeso, Smirna, Pergamo, Thiatira, Sardi, Filadelfia na Laodikia.”
It told me, “Write down in a book what you see and send it to the seven churches: Ephesus, Smyrna, Pergamum, Thyatira, Sardis, Philadelphia, and Laodicea.”
12 Ndipo nikageuka ili nione ni sauti ya nani iliyokuwa ikisema nami. Nami nilipogeuka, nikaona vinara saba vya taa vya dhahabu,
I turned round to see who was speaking to me. When I turned I saw seven golden candlesticks,
13 na katikati ya vile vinara vya taa, alikuwamo mtu kama Mwana wa Adamu, akiwa amevaa joho refu, na mkanda wa dhahabu ukiwa umefungwa kifuani mwake.
and standing among the candlesticks was someone who looked like a Son of man. He was wearing a robe that reached down to his feet with a golden sash across his chest.
14 Kichwa chake na nywele zake zilikuwa nyeupe kama sufu, nyeupe kama theluji, nayo macho yake yalikuwa kama mwali wa moto.
His hair looked like white wool, and his eyes like flaming fire.
15 Nyayo zake zilikuwa kama shaba inayongʼaa, katika tanuru ya moto, nayo sauti yake ilikuwa kama mugurumo ya maji mengi.
His feet looked like polished brass that had been refined in a furnace. His voice sounded like a thundering waterfall.
16 Katika mkono wake wa kuume alishika nyota saba, na kinywani mwake ulitoka upanga mkali wenye makali kuwili. Uso wake ulikuwa kama jua likingʼaa kwa nguvu zake zote.
He was holding seven stars in his right hand, and a sharp double-edged sword came out of his mouth. His face shone like the sun at its brightest.
17 Nilipomwona, nilianguka miguuni pake kama aliyekufa. Ndipo akauweka mkono wake wa kuume juu yangu na kusema: “Usiogope, Mimi ndiye wa Kwanza na wa Mwisho.
When I saw him I fell down at his feet as if I were dead. But he touched me with his right hand and said, “Don't be afraid, I am the first and the last,
18 Mimi ni Yeye Aliye Hai, niliyekuwa nimekufa, na tazama, ni hai milele na milele! Nami ninazo funguo za mauti na kuzimu. (aiōn , Hadēs )
the living one. I was dead, but look! Now I am alive for ever and ever, and I hold the keys of death and the grave. (aiōn , Hadēs )
19 “Basi andika mambo uliyoyaona, yaliyopo na yale yatakayotukia baada ya haya.
So write down what you've seen—what's happening in the present and what will happen in the future.
20 Kuhusu siri ya zile nyota saba ulizoziona katika mkono wangu wa kuume na vile vinara saba vya taa vya dhahabu ni hii: Zile nyota saba ni malaika wa yale makanisa saba, navyo vile vinara saba ni hayo makanisa saba.
The meaning of the seven stars that you saw me holding in my right hand and the seven golden candlesticks is this: the seven stars are the angels of the seven churches and the seven candlesticks are the seven churches.”