< Ufunuo 9 >
1 Malaika wa tano akaipiga tarumbeta yake, nami nikaona nyota iliyokuwa imeanguka toka angani hadi ardhini. Nyota hiyo ilipewa ufunguo wa lile Shimo. (Abyssos )
O quinto anjo tocou a sua trombeta. Eu vi uma estrela vinda do céu cair na terra. Ela recebeu a chave que abria o Abismo. (Abyssos )
2 Alipolifungua hilo Shimo, moshi ukapanda kutoka humo kama moshi wa tanuru kubwa sana. Jua na anga vikatiwa giza na ule moshi uliotoka katika hilo Shimo. (Abyssos )
Ela abriu a porta de entrada do Abismo e, de lá, saiu fumaça como a de uma imensa fornalha. O sol e o céu ficaram na mais completa escuridão, por causa da fumaça que tinha saído do Abismo. (Abyssos )
3 Ndipo katika ule moshi wakatoka nzige wakaenda juu ya nchi, nao wakapewa nguvu kama zile za nge wa duniani.
Da fumaça surgiram gafanhotos, que se espalharam pela terra e que receberam poder semelhante ao de escorpiões.
4 Wakaambiwa wasidhuru nyasi ya nchi, wala mmea wala mti wowote, bali wawadhuru tu wale watu ambao hawana muhuri wa Mungu kwenye vipaji vya nyuso zao.
Foi dito para que eles não danificassem a relva, as árvores ou qualquer outro tipo de vegetação. Eles tinham ordem de ferir apenas as pessoas que não tivessem a marca do selo de Deus em suas testas.
5 Wakaruhusiwa kuwatesa kwa muda wa miezi mitano, lakini wasiwaue. Uchungu wa kuuma kwao ulikuwa kama ule wa mtu aumwapo na nge.
Eles não podiam matar, mas poderiam torturar essas pessoas durante cinco meses. A dor dessa tortura era como a de uma picada de escorpião.
6 Katika siku hizo watu watatafuta kifo lakini hawatakiona, watatamani kufa, lakini kifo kitawakimbia.
Durante esse período de cinco meses, as pessoas irão buscar a morte, mas não a encontrarão. Elas irão desejar morrer, mas a morte irá fugir delas!
7 Wale nzige walikuwa na umbo kama la farasi waliotayarishwa kwa ajili ya vita. Kwenye vichwa vyao kulikuwa na kitu kama taji za dhahabu na nyuso zao zilikuwa kama za binadamu.
Os gafanhotos pareciam cavalos de guerra. Eles usavam o que parecia ser coroas douradas sobre a cabeça, e seus rostos pareciam com os de seres humanos.
8 Walikuwa na nywele kama za wanawake, na meno yao yalikuwa kama ya simba.
Eles tinham cabelos compridos como os de mulheres e dentes como os de leões.
9 Walikuwa na dirii kama za chuma, na sauti za mabawa yao zilikuwa kama ngurumo za farasi wengi na magari mengi yakikimbilia vitani.
As suas couraças pareciam como se fossem feitas de ferro, e o barulho que faziam ao bater as suas asas era como o de carros sendo puxados por muitos cavalos, indo para uma batalha.
10 Walikuwa na mikia yenye miiba ya kuumia kama nge. Nguvu yao ya kutesa watu kwa huo muda wa miezi mitano ilikuwa katika hiyo mikia yao.
Eles tinham rabos e ferrões como os de escorpiões. Tinham o poder de machucar as pessoas durante cinco meses com os seus rabos.
11 Walikuwa na mfalme wao, ambaye ni malaika wa lile Shimo, ambaye jina lake kwa Kiebrania ni Abadoni, na kwa Kiyunani ni Apolioni. (Abyssos )
O rei que os governava era o anjo do Abismo, chamado Abadom, em hebraico, e Apolião, em grego. (Abyssos )
12 Ole ya kwanza imepita, bado nyingine mbili zinakuja.
O primeiro Ai foi cumprido, mas ainda havia mais dois por vir.
13 Malaika wa sita akaipiga tarumbeta yake, nami nikasikia sauti ikitoka katika zile pembe za madhabahu ya dhahabu iliyoko mbele za Mungu.
O sexto anjo tocou a sua trombeta. Eu ouvi uma voz que vinha dos cantos do altar dourado, que está diante do trono de Deus,
14 Ile sauti ikamwambia yule malaika wa sita mwenye tarumbeta, “Wafungulie wale malaika wanne waliofungwa kwenye ule mto mkubwa Frati.”
falando para o sexto anjo que tinha a trombeta: “Liberte os quatro anjos que estão presos perto do grande rio Eufrates!”
15 Basi wale malaika wanne, waliokuwa wamewekwa tayari kwa ajili ya saa hiyo, na siku hiyo, na mwezi huo, na mwaka huo ili wawaue theluthi ya wanadamu wakafunguliwa.
Os quatro anjos que estavam preparados para essa hora, dia, mês e ano específicos foram soltos para matar um terço da humanidade.
16 Idadi ya majeshi wapanda farasi ilikuwa 200,000,000. Nilisikia idadi yao.
E me disseram que o número de soldados a cavalo desse exército somava duzentos milhões.
17 Hivi ndivyo nilivyowaona hao farasi na wapanda farasi katika maono yangu: Wapanda farasi walivaa dirii vifuani zenye rangi nyekundu sana kama ya moto na yakuti samawi na kiberiti. Vichwa vya hao farasi vilikuwa kama vichwa vya simba, na moto, moshi na kiberiti vilitoka vinywani mwao.
Em minha visão, eu vi os cavalos e os seus cavaleiros usando couraças vermelhas como o fogo e, também, azul-escuras e amarelas. As cabeças dos cavalos pareciam como as de leões e de suas bocas saíam fogo, fumaça e enxofre.
18 Theluthi ya wanadamu wakauawa kwa mapigo hayo matatu, yaani, huo moto, moshi na kiberiti, vilivyotoka kwenye vinywa vya hao farasi.
A terça parte da humanidade foi morta por essas três pragas: o fogo, a fumaça e o enxofre que saíam das bocas dos cavalos.
19 Nguvu za hao farasi zilikuwa katika vinywa vyao na kwenye mikia yao, kwa sababu mikia yao ilikuwa kama nyoka, yenye vichwa ambayo waliitumia kudhuru.
O poder dos cavalos estava em seus rabos, assim como, em suas bocas, pois os rabos eram como cabeças de serpentes que eles usavam para ferir as pessoas.
20 Wanadamu waliosalia, ambao hawakuuawa katika mapigo hayo, bado walikataa kutubia kazi za mikono yao na hawakuacha kuabudu mashetani na sanamu za dhahabu, za fedha, za shaba, za mawe na za miti, ambazo haziwezi kuona, kusikia wala kutembea.
Mas, nem mesmo assim, o restante da humanidade, que não morreu por causa dessas pragas, arrependeu-se dos pecados que cometia. Eles não pararam de adorar demônios e ídolos de ouro, prata, bronze e pedra, os quais não podem ver, ouvir ou andar.
21 Wala hawakutubu na kuacha matendo yao ya uuaji, uchawi, uasherati wala wizi wao.
Eles não se arrependeram dos assassinatos, da feitiçaria, da imoralidade sexual ou dos roubos que cometiam.