< Ufunuo 7 >
1 Baada ya hili nikaona malaika wanne wakiwa wamesimama katika pembe nne za dunia, wakizuia hizo pepo nne za dunia, ili kwamba pasiwe na upepo utakaovuma juu ya nchi au juu ya bahari au juu ya mti wowote.
Sedan såg jag fyra Änglar stå på fyra jordenes hörn, hållande fyra jordenes väder, att intet väder skulle blåsa på jordena, eller på hafvet, eller på något trä.
2 Nikaona malaika mwingine akipanda kutoka mawio ya jua akiwa na muhuri wa Mungu aliye hai. Akawaita kwa sauti kubwa wale malaika wanne waliokuwa wamepewa mamlaka ya kuidhuru nchi na bahari, akisema,
Och jag såg en annan Ängel uppstiga ifrå solens uppgång; han hade lefvandes Guds insegel, och ropade med höga röst till de fyra Änglar, hvilkom gifvet var skada göra jordene och hafvena;
3 “Msiidhuru nchi wala bahari, wala miti, hadi tuwe tumetia muhuri kwenye vipaji vya nyuso za watumishi wa Mungu wetu.”
Och sade: Görer icke jordene skada, eller hafvena, eller trän, så länge vi med insegel tecknom vår Guds tjenare på deras anlete.
4 Ndipo nikasikia idadi ya wale waliotiwa muhuri: yaani 144,000 kutoka makabila yote ya Israeli.
Och jag hörde talet på dem, som tecknade voro, hundrade fyra och fyratio tusend, som tecknade voro, af all Israels barnas slägter:
5 Kutoka kabila la Yuda 12,000 walitiwa muhuri, kutoka kabila la Reubeni 12,000, kutoka kabila la Gadi 12,000,
Af Juda slägte tolftusend tecknade; af Rubens slägte tolftusend tecknade; af Gads slägte tolftusend tecknade;
6 kutoka kabila la Asheri 12,000, kutoka kabila la Naftali 12,000, kutoka kabila la Manase 12,000,
Af Assers slägte tolftusend tecknade; af Nephthali slägte tolftusend tecknade; af Manasse slägte tolftusend tecknade;
7 kutoka kabila la Simeoni 12,000, kutoka kabila la Lawi 12,000, kutoka kabila la Isakari 12,000,
Af Simeons slägte tolftusend tecknade; af Levi slägte tolftusend tecknade; af Isaschars slägte tolftusend tecknade;
8 kutoka kabila la Zabuloni 12,000, kutoka kabila la Yosefu 12,000, na kutoka kabila la Benyamini 12,000.
Af Zabulons slägte tolftusend tecknade; af Josephs slägte tolftusend tecknade; af BenJamins slägte tolftusend tecknade.
9 Baada ya hili nikatazama na hapo mbele yangu palikuwa na umati mkubwa wa watu ambao hakuna yeyote awezaye kuuhesabu, kutoka kila taifa, kila kabila, kila jamaa na kila lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi na mbele ya Mwana-Kondoo. Walikuwa wamevaa mavazi meupe na wakiwa wameshika matawi ya mitende mikononi mwao.
Sedan såg jag, och si, en stor skare, den ingen räkna kunde, af allom Hedningom, och slägtom, och folkom, och tungomålom, ståndande för stolen, och för Lambena, klädd i sid hvit kläder, och palmer i deras händer;
10 Nao walikuwa wakipiga kelele kwa sauti kubwa wakisema: “Wokovu una Mungu wetu, yeye aketiye kwenye kiti cha enzi, na Mwana-Kondoo!”
Och de ropade med höga röst, och sade: Salighet honom, som sitter på stolen, vårom Gudi och Lambena.
11 Malaika wote walikuwa wamesimama kukizunguka kile kiti cha enzi na wale wazee ishirini na wanne na wale viumbe wanne wenye uhai. Wakaanguka kifudifudi mbele ya hicho kiti cha enzi na kumwabudu Mungu,
Och alle Änglar stodo kringom stolen, och om de äldsta, och om de fyra djuren, och föllo på sin ansigte framför stolen, och tillbådo Gud;
12 wakisema: “Amen! Sifa na utukufu na hekima na shukrani na heshima na uweza na nguvu viwe kwa Mungu wetu milele na milele. Amen!” (aiōn )
Och sade: Amen, lof, och ära, och vishet, och tack, och pris, och kraft, och starkhet vare vårom Gud, ifrån evighet till evighet. Amen. (aiōn )
13 Kisha mmoja wa wale wazee ishirini na wanne akaniuliza, “Ni nani hawa waliovaa mavazi meupe, nao wametoka wapi?”
Och en af de äldsta svarade, och sade till mig: Ho äro desse, som uti de sida hvita kläder klädde äro? Och hvadan äro de komne?
14 Nikamjibu, “Bwana, wewe wajua.” Naye akasema, “Hawa ni wale waliotoka katika ile dhiki kuu, nao wamefua mavazi yao katika damu ya Mwana-Kondoo na kuyafanya meupe kabisa.
Och jag sade till honom: Herre, du vetst det. Och han sade till mig: Desse äro de som komne äro utu stor bedröfvelse, och hafva tvagit sin kläder, och gjort dem hvit i Lambsens blod.
15 Kwa hiyo, “Wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu na kumtumikia usiku na mchana katika hekalu lake; naye aketiye katika kile kiti cha enzi atatanda hema yake juu yao.
Derföre äro de för Guds stol, och tjena honom dag och natt uti hans tempel; och den på stolen sitter, skall bo öfver dem.
16 Kamwe hawataona njaa wala kiu tena. Jua halitawapiga wala joto lolote liunguzalo.
De skola intet mer hungra, eller törsta; icke heller skall solen falla på dem, icke heller någon hette;
17 Kwa maana Mwana-Kondoo aliyeko katikati ya kile kiti cha enzi atakuwa Mchungaji wao; naye atawaongoza kwenda kwenye chemchemi za maji yaliyo hai. Naye Mungu atafuta kila chozi kutoka macho yao.”
Ty Lambet, som midt i stolen är, skall regera dem, och leda dem till lefvande vattukällor; och Gud skall aftorka alla tårar af deras ögon.