< Ufunuo 7 >
1 Baada ya hili nikaona malaika wanne wakiwa wamesimama katika pembe nne za dunia, wakizuia hizo pepo nne za dunia, ili kwamba pasiwe na upepo utakaovuma juu ya nchi au juu ya bahari au juu ya mti wowote.
Potem zobaczyłem czterech aniołów stojących na czterech krańcach ziemi, trzymających cztery wiatry ziemi, aby wiatr nie wiał na ziemię ani na morze, ani na żadne drzewo.
2 Nikaona malaika mwingine akipanda kutoka mawio ya jua akiwa na muhuri wa Mungu aliye hai. Akawaita kwa sauti kubwa wale malaika wanne waliokuwa wamepewa mamlaka ya kuidhuru nchi na bahari, akisema,
I zobaczyłem innego anioła wstępującego od wschodu słońca, który miał pieczęć Boga żywego i zawołał donośnym głosem do czterech aniołów, którym pozwolono wyrządzać szkodę ziemi i morzu:
3 “Msiidhuru nchi wala bahari, wala miti, hadi tuwe tumetia muhuri kwenye vipaji vya nyuso za watumishi wa Mungu wetu.”
Nie wyrządzajcie szkody ziemi ani morzu, ani drzewom, dopóki nie opieczętujemy sług naszego Boga na ich czołach.
4 Ndipo nikasikia idadi ya wale waliotiwa muhuri: yaani 144,000 kutoka makabila yote ya Israeli.
I usłyszałem liczbę opieczętowanych: sto czterdzieści cztery tysiące opieczętowanych ze wszystkich pokoleń synów Izraela:
5 Kutoka kabila la Yuda 12,000 walitiwa muhuri, kutoka kabila la Reubeni 12,000, kutoka kabila la Gadi 12,000,
Z pokolenia Judy dwanaście tysięcy opieczętowanych, z pokolenia Rubena dwanaście tysięcy opieczętowanych, z pokolenia Gada dwanaście tysięcy opieczętowanych;
6 kutoka kabila la Asheri 12,000, kutoka kabila la Naftali 12,000, kutoka kabila la Manase 12,000,
Z pokolenia Asera dwanaście tysięcy opieczętowanych, z pokolenia Neftalego dwanaście tysięcy opieczętowanych, z pokolenia Manassesa dwanaście tysięcy opieczętowanych;
7 kutoka kabila la Simeoni 12,000, kutoka kabila la Lawi 12,000, kutoka kabila la Isakari 12,000,
Z pokolenia Symeona dwanaście tysięcy opieczętowanych, z pokolenia Lewiego dwanaście tysięcy opieczętowanych, z pokolenia Issachara dwanaście tysięcy opieczętowanych;
8 kutoka kabila la Zabuloni 12,000, kutoka kabila la Yosefu 12,000, na kutoka kabila la Benyamini 12,000.
Z pokolenia Zabulona dwanaście tysięcy opieczętowanych, z pokolenia Józefa dwanaście tysięcy opieczętowanych, z pokolenia Beniamina dwanaście tysięcy opieczętowanych.
9 Baada ya hili nikatazama na hapo mbele yangu palikuwa na umati mkubwa wa watu ambao hakuna yeyote awezaye kuuhesabu, kutoka kila taifa, kila kabila, kila jamaa na kila lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi na mbele ya Mwana-Kondoo. Walikuwa wamevaa mavazi meupe na wakiwa wameshika matawi ya mitende mikononi mwao.
Potem zobaczyłem, a oto wielki tłum, którego nikt nie mógł policzyć, z każdego narodu, plemienia, ludu i języka, który stał przed tronem i przed Barankiem ubrani w białe szaty, a palmy w ich rękach.
10 Nao walikuwa wakipiga kelele kwa sauti kubwa wakisema: “Wokovu una Mungu wetu, yeye aketiye kwenye kiti cha enzi, na Mwana-Kondoo!”
I wołali donośnym głosem: Zbawienie należy do naszego Boga zasiadającego na tronie i do Baranka.
11 Malaika wote walikuwa wamesimama kukizunguka kile kiti cha enzi na wale wazee ishirini na wanne na wale viumbe wanne wenye uhai. Wakaanguka kifudifudi mbele ya hicho kiti cha enzi na kumwabudu Mungu,
A wszyscy aniołowie stali dokoła tronu i starszych, i czterech stworzeń, i upadli przed tronem na twarze, i oddali pokłon Bogu;
12 wakisema: “Amen! Sifa na utukufu na hekima na shukrani na heshima na uweza na nguvu viwe kwa Mungu wetu milele na milele. Amen!” (aiōn )
Mówiąc: Amen. Błogosławieństwo i chwała, i mądrość, i dziękczynienie, i cześć, i moc, i siła naszemu Bogu na wieki wieków. Amen. (aiōn )
13 Kisha mmoja wa wale wazee ishirini na wanne akaniuliza, “Ni nani hawa waliovaa mavazi meupe, nao wametoka wapi?”
A jeden ze starszych odezwał się do mnie tymi słowy: Kim są ci, którzy są ubrani w białe szaty i skąd przybyli?
14 Nikamjibu, “Bwana, wewe wajua.” Naye akasema, “Hawa ni wale waliotoka katika ile dhiki kuu, nao wamefua mavazi yao katika damu ya Mwana-Kondoo na kuyafanya meupe kabisa.
Odpowiedziałem mu: Panie, ty wiesz. I powiedział do mnie: To są ci, którzy przyszli z wielkiego ucisku i wyprali swoje szaty, i wybielili je we krwi Baranka.
15 Kwa hiyo, “Wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu na kumtumikia usiku na mchana katika hekalu lake; naye aketiye katika kile kiti cha enzi atatanda hema yake juu yao.
Dlatego są przed tronem Boga i służą mu we dnie i w nocy w jego świątyni, a zasiadający na tronie osłoni ich [sobą] jak namiotem.
16 Kamwe hawataona njaa wala kiu tena. Jua halitawapiga wala joto lolote liunguzalo.
Nie zaznają już głodu ani pragnienia, nie porazi ich słońce ani żaden upał;
17 Kwa maana Mwana-Kondoo aliyeko katikati ya kile kiti cha enzi atakuwa Mchungaji wao; naye atawaongoza kwenda kwenye chemchemi za maji yaliyo hai. Naye Mungu atafuta kila chozi kutoka macho yao.”
Ponieważ Baranek, który jest pośrodku tronu, będzie ich pasł i poprowadzi ich do żywych źródeł wód, i otrze Bóg wszelką łzę z ich oczu.