< Ufunuo 7 >
1 Baada ya hili nikaona malaika wanne wakiwa wamesimama katika pembe nne za dunia, wakizuia hizo pepo nne za dunia, ili kwamba pasiwe na upepo utakaovuma juu ya nchi au juu ya bahari au juu ya mti wowote.
Potemem widział czterech Aniołów, stojących na czterech węgłach ziemi, trzymających cztery wiatry ziemi, aby nie wiał wiatr na ziemię, ani na morze, ani na żadne drzewo.
2 Nikaona malaika mwingine akipanda kutoka mawio ya jua akiwa na muhuri wa Mungu aliye hai. Akawaita kwa sauti kubwa wale malaika wanne waliokuwa wamepewa mamlaka ya kuidhuru nchi na bahari, akisema,
I widziałem inszego Anioła występującego od wschodu słońca, mającego pieczęć Boga żywego, i zawołał głosem wielkim na onych czterech Aniołów, którym dano, aby szkodzili ziemi i morzu;
3 “Msiidhuru nchi wala bahari, wala miti, hadi tuwe tumetia muhuri kwenye vipaji vya nyuso za watumishi wa Mungu wetu.”
Mówiąc: Nie szkodźcie ziemi ani morzu, ani drzewom, aż popieczętujemy sługi Boga naszego na czołach ich.
4 Ndipo nikasikia idadi ya wale waliotiwa muhuri: yaani 144,000 kutoka makabila yote ya Israeli.
I usłyszałem liczbę popieczętowanych: sto czterdzieści i cztery tysiące jest popieczętowanych ze wszystkich pokoleń synów Izraelskich:
5 Kutoka kabila la Yuda 12,000 walitiwa muhuri, kutoka kabila la Reubeni 12,000, kutoka kabila la Gadi 12,000,
Z pokolenia Judowego dwanaście tysięcy popieczętowanych; z pokolenia Rubenowego dwanaście tysięcy popieczętowanych; z pokolenia Gadowego dwanaście tysięcy popieczętowanych;
6 kutoka kabila la Asheri 12,000, kutoka kabila la Naftali 12,000, kutoka kabila la Manase 12,000,
Z pokolenia Aserowego dwanaście tysięcy popieczętowanych; z pokolenia Neftalimowego dwanaście tysięcy popieczętowanych; z pokolenia Manasesowego dwanaście tysięcy popieczętowanych;
7 kutoka kabila la Simeoni 12,000, kutoka kabila la Lawi 12,000, kutoka kabila la Isakari 12,000,
Z pokolenia Symeonowego dwanaście tysięcy popieczętowanych; z pokolenia Lewiego dwanaście tysięcy popieczętowanych; z pokolenia Isacharowego dwanaście tysięcy popieczętowanych;
8 kutoka kabila la Zabuloni 12,000, kutoka kabila la Yosefu 12,000, na kutoka kabila la Benyamini 12,000.
Z pokolenia Zabulonowego dwanaście tysięcy popieczętowanych; z pokolenia Józefowego dwanaście tysięcy popieczętowanych; z pokolenia Benjaminowego dwanaście tysięcy popieczętowanych.
9 Baada ya hili nikatazama na hapo mbele yangu palikuwa na umati mkubwa wa watu ambao hakuna yeyote awezaye kuuhesabu, kutoka kila taifa, kila kabila, kila jamaa na kila lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi na mbele ya Mwana-Kondoo. Walikuwa wamevaa mavazi meupe na wakiwa wameshika matawi ya mitende mikononi mwao.
Potemem widział, a oto lud wielki, którego nie mógł nikt zliczyć, z każdego narodu i pokolenia, i ludzi, i języków, którzy stali przed stolicą i przed oblicznością Baranka, obleczeni w szaty białe, a palmy były w rękach ich.
10 Nao walikuwa wakipiga kelele kwa sauti kubwa wakisema: “Wokovu una Mungu wetu, yeye aketiye kwenye kiti cha enzi, na Mwana-Kondoo!”
I wołali głosem wielkim, mówiąc: Zbawienie należy Bogu naszemu, siedzącemu na stolicy i Barankowi.
11 Malaika wote walikuwa wamesimama kukizunguka kile kiti cha enzi na wale wazee ishirini na wanne na wale viumbe wanne wenye uhai. Wakaanguka kifudifudi mbele ya hicho kiti cha enzi na kumwabudu Mungu,
A wszyscy Aniołowie stali około stolicy i starców i czworga zwierząt, i upadli przed stolicą na oblicze swoje, i kłaniali się Bogu,
12 wakisema: “Amen! Sifa na utukufu na hekima na shukrani na heshima na uweza na nguvu viwe kwa Mungu wetu milele na milele. Amen!” (aiōn )
Mówiąc: Amen! Błogosławieństwo i chwała, i mądrość, i dziękowanie, i cześć, i moc, i siła Bogu naszemu na wieki wieków. Amen. (aiōn )
13 Kisha mmoja wa wale wazee ishirini na wanne akaniuliza, “Ni nani hawa waliovaa mavazi meupe, nao wametoka wapi?”
I odpowiedział jeden z onych starców i rzekł mi: Ci, którzy są obleczeni w szaty białe, co zacz są? i skąd przyszli?
14 Nikamjibu, “Bwana, wewe wajua.” Naye akasema, “Hawa ni wale waliotoka katika ile dhiki kuu, nao wamefua mavazi yao katika damu ya Mwana-Kondoo na kuyafanya meupe kabisa.
I rzekłem mu: Panie! ty wiesz. I rzekł mi: Cić są, którzy przyszli z ucisku wielkiego i omyli szaty swoje, i wybielili je we krwi Barankowej.
15 Kwa hiyo, “Wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu na kumtumikia usiku na mchana katika hekalu lake; naye aketiye katika kile kiti cha enzi atatanda hema yake juu yao.
Dlatego są przed stolicą Bożą i służą mu we dnie i w nocy w kościele jego, a ten, który siedzi na stolicy, jako namiotem zasłoni ich.
16 Kamwe hawataona njaa wala kiu tena. Jua halitawapiga wala joto lolote liunguzalo.
Nie będą więcej łaknąć i nie będą więcej pragnąć, i nie uderzy na nich słońce, ani żadne gorąco
17 Kwa maana Mwana-Kondoo aliyeko katikati ya kile kiti cha enzi atakuwa Mchungaji wao; naye atawaongoza kwenda kwenye chemchemi za maji yaliyo hai. Naye Mungu atafuta kila chozi kutoka macho yao.”
Albowiem Baranek, który jest w pośrodku stolicy, będzie ich pasł i poprowadzi ich do żywych źródeł wód, i otrze Bóg wszelką łzę z oczów ich.