< Ufunuo 7 >
1 Baada ya hili nikaona malaika wanne wakiwa wamesimama katika pembe nne za dunia, wakizuia hizo pepo nne za dunia, ili kwamba pasiwe na upepo utakaovuma juu ya nchi au juu ya bahari au juu ya mti wowote.
After this I saw four angels, standing at the four corners of the earth, restraining the four winds from blowing on the earth, or on the sea, or on any tree.
2 Nikaona malaika mwingine akipanda kutoka mawio ya jua akiwa na muhuri wa Mungu aliye hai. Akawaita kwa sauti kubwa wale malaika wanne waliokuwa wamepewa mamlaka ya kuidhuru nchi na bahari, akisema,
And I saw another angel ascend from the sunrising, having a seal of the living God; and he cried with a great voice to the four angels to whom it was given to injure the earth and the sea,
3 “Msiidhuru nchi wala bahari, wala miti, hadi tuwe tumetia muhuri kwenye vipaji vya nyuso za watumishi wa Mungu wetu.”
saying, "Do no harm to the earth, or the sea, or the trees, Until we have sealed the slaves of our God on their foreheads."
4 Ndipo nikasikia idadi ya wale waliotiwa muhuri: yaani 144,000 kutoka makabila yote ya Israeli.
And I heard the number of those who were sealed, a hundred and forty and four thousand, sealed out of every tribe of the children of Israel.
5 Kutoka kabila la Yuda 12,000 walitiwa muhuri, kutoka kabila la Reubeni 12,000, kutoka kabila la Gadi 12,000,
Of the tribe of Judah, twelve thousand were sealed; Of the tribe of Reuben, twelve thousand; Of the tribe of Gad, twelve thousand;
6 kutoka kabila la Asheri 12,000, kutoka kabila la Naftali 12,000, kutoka kabila la Manase 12,000,
Of the tribe of Asher, twelve thousand; Of the tribe of Naphtali, twelve thousand; Of the tribe of Manasseh, twelve thousand;
7 kutoka kabila la Simeoni 12,000, kutoka kabila la Lawi 12,000, kutoka kabila la Isakari 12,000,
Of the tribe of Symeon, twelve thousand; Of the tribe of Levi, twelve thousand; Of the tribe of Issachar, twelve thousand;
8 kutoka kabila la Zabuloni 12,000, kutoka kabila la Yosefu 12,000, na kutoka kabila la Benyamini 12,000.
Of the tribe of Zebulun, twelve thousand; Of the tribe of Joseph, twelve thousand; Of the tribe of Benjamin, twelve thousand;
9 Baada ya hili nikatazama na hapo mbele yangu palikuwa na umati mkubwa wa watu ambao hakuna yeyote awezaye kuuhesabu, kutoka kila taifa, kila kabila, kila jamaa na kila lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi na mbele ya Mwana-Kondoo. Walikuwa wamevaa mavazi meupe na wakiwa wameshika matawi ya mitende mikononi mwao.
After this I looked, and behold a great multitude, whom no man could number, out of every nation and tribe and people and tongue, standing before the throne and before the Lamb, clothed in white robes, with palm branches in their hands;
10 Nao walikuwa wakipiga kelele kwa sauti kubwa wakisema: “Wokovu una Mungu wetu, yeye aketiye kwenye kiti cha enzi, na Mwana-Kondoo!”
and they cried with a loud voice, saying "Salvation to our God, who sits on the throne, And to the Lamb!"
11 Malaika wote walikuwa wamesimama kukizunguka kile kiti cha enzi na wale wazee ishirini na wanne na wale viumbe wanne wenye uhai. Wakaanguka kifudifudi mbele ya hicho kiti cha enzi na kumwabudu Mungu,
And all the angels stood encircling the throne, and the Elders and the Living Creatures; and they fell on their faces before the throne, worshiping God,
12 wakisema: “Amen! Sifa na utukufu na hekima na shukrani na heshima na uweza na nguvu viwe kwa Mungu wetu milele na milele. Amen!” (aiōn )
and crying, "Even so! The blessing and the glory and the wisdom And the thanksgiving and the honor and the power and the might Be to our God forever and ever. Amen." (aiōn )
13 Kisha mmoja wa wale wazee ishirini na wanne akaniuliza, “Ni nani hawa waliovaa mavazi meupe, nao wametoka wapi?”
And one of the Elders spoke to me, saying. "Who are these, clad in white robes? Whence come they?"
14 Nikamjibu, “Bwana, wewe wajua.” Naye akasema, “Hawa ni wale waliotoka katika ile dhiki kuu, nao wamefua mavazi yao katika damu ya Mwana-Kondoo na kuyafanya meupe kabisa.
And I said to him, "You know, my Lord." And he said to me, "These are those who have come out of the great persecution, and have washed their robes and made them white in the blood of the Lamb.
15 Kwa hiyo, “Wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu na kumtumikia usiku na mchana katika hekalu lake; naye aketiye katika kile kiti cha enzi atatanda hema yake juu yao.
For this they are now before the throne of God, and are serving him day and night in his temple. "And He who sits on the throne Will spread his tabernacle over them.
16 Kamwe hawataona njaa wala kiu tena. Jua halitawapiga wala joto lolote liunguzalo.
They hunger no more, Neither thirst any more; Neither will the sun strike upon them, Nor any scorching heat;
17 Kwa maana Mwana-Kondoo aliyeko katikati ya kile kiti cha enzi atakuwa Mchungaji wao; naye atawaongoza kwenda kwenye chemchemi za maji yaliyo hai. Naye Mungu atafuta kila chozi kutoka macho yao.”
For the Lamb in the midst of the throne Will shepherd them, And will lead them to fountains of living water; And God will wipe away every tear from their eyes."