< Ufunuo 7 >

1 Baada ya hili nikaona malaika wanne wakiwa wamesimama katika pembe nne za dunia, wakizuia hizo pepo nne za dunia, ili kwamba pasiwe na upepo utakaovuma juu ya nchi au juu ya bahari au juu ya mti wowote.
Og derefter saa jeg fire Engle staa paa Jordens fire Hjørner; de holdt Jordens fire Vinde, for at ingen Vind skulde blæse over Jorden, ej heller over Havet, ej heller over noget Træ.
2 Nikaona malaika mwingine akipanda kutoka mawio ya jua akiwa na muhuri wa Mungu aliye hai. Akawaita kwa sauti kubwa wale malaika wanne waliokuwa wamepewa mamlaka ya kuidhuru nchi na bahari, akisema,
Og jeg saa en anden Engel stige op fra Solens Opgang med den levende Guds Segl; og han raabte med høj Røst til de fire Engle, hvem det var givet at skade Jorden og Havet, og sagde:
3 “Msiidhuru nchi wala bahari, wala miti, hadi tuwe tumetia muhuri kwenye vipaji vya nyuso za watumishi wa Mungu wetu.”
Skader ikke Jorden, ej heller Havet, ej heller Træerne, førend vi have beseglet vor Guds Tjenere paa deres Pander.
4 Ndipo nikasikia idadi ya wale waliotiwa muhuri: yaani 144,000 kutoka makabila yote ya Israeli.
Og jeg hørte Tallet paa de beseglede, hundrede og fire og fyrretyve Tusinde beseglede af alle Israels Børns Stammer:
5 Kutoka kabila la Yuda 12,000 walitiwa muhuri, kutoka kabila la Reubeni 12,000, kutoka kabila la Gadi 12,000,
Af Judas Stamme tolv Tusinde beseglede, af Rubens Stamme tolv Tusinde, af Gads Stamme tolv Tusinde,
6 kutoka kabila la Asheri 12,000, kutoka kabila la Naftali 12,000, kutoka kabila la Manase 12,000,
af Asers Stamme tolv Tusinde, af Nafthalis Stamme tolv Tusinde, af Manasses Stamme tolv Tusinde,
7 kutoka kabila la Simeoni 12,000, kutoka kabila la Lawi 12,000, kutoka kabila la Isakari 12,000,
af Simeons Stamme tolv Tusinde, af Levis Stamme tolv Tusinde, af Isaskars Stamme tolv Tusinde,
8 kutoka kabila la Zabuloni 12,000, kutoka kabila la Yosefu 12,000, na kutoka kabila la Benyamini 12,000.
af Sebulons Stamme tolv Tusinde, af Josefs Stamme tolv Tusinde og af Benjamins Stamme tolv Tusinde beseglede.
9 Baada ya hili nikatazama na hapo mbele yangu palikuwa na umati mkubwa wa watu ambao hakuna yeyote awezaye kuuhesabu, kutoka kila taifa, kila kabila, kila jamaa na kila lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi na mbele ya Mwana-Kondoo. Walikuwa wamevaa mavazi meupe na wakiwa wameshika matawi ya mitende mikononi mwao.
Derefter saa jeg, og se en stor Skare, som ingen kunde tælle, af alle Folkeslag og Stammer og Folk og Tungemaal, som stod for Tronen og for Lammet, iførte lange hvide Klæder og med Palmegrene i deres Hænder;
10 Nao walikuwa wakipiga kelele kwa sauti kubwa wakisema: “Wokovu una Mungu wetu, yeye aketiye kwenye kiti cha enzi, na Mwana-Kondoo!”
og de raabte med høj Røst og sagde: Frelsen tilhører vor Gud, som sidder paa Tronen, og Lammet!
11 Malaika wote walikuwa wamesimama kukizunguka kile kiti cha enzi na wale wazee ishirini na wanne na wale viumbe wanne wenye uhai. Wakaanguka kifudifudi mbele ya hicho kiti cha enzi na kumwabudu Mungu,
Og alle Englene stode rundt om Tronen og om de Ældste og om de fire Væsener og faldt ned for Tronen paa deres Ansigt og tilbade Gud og sagde:
12 wakisema: “Amen! Sifa na utukufu na hekima na shukrani na heshima na uweza na nguvu viwe kwa Mungu wetu milele na milele. Amen!” (aiōn g165)
Amen! Velsignelsen og Prisen og Visdommen og Taksigelsen og Æren og Kraften og Styrken tilhører vor Gud i Evighedernes Evigheder! Amen. (aiōn g165)
13 Kisha mmoja wa wale wazee ishirini na wanne akaniuliza, “Ni nani hawa waliovaa mavazi meupe, nao wametoka wapi?”
Og en af de Ældste tog til Orde og sagde til mig: Disse, som ere iførte de lange hvide Klæder, hvem ere de? og hvorfra ere de komne?
14 Nikamjibu, “Bwana, wewe wajua.” Naye akasema, “Hawa ni wale waliotoka katika ile dhiki kuu, nao wamefua mavazi yao katika damu ya Mwana-Kondoo na kuyafanya meupe kabisa.
Og jeg sagde til ham: Min Herre! du ved det. Og han sagde til mig: Det er dem, som komme ud af den store Trængsel, og de have tvættet deres Klæder og gjort dem hvide i Lammets Blod.
15 Kwa hiyo, “Wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu na kumtumikia usiku na mchana katika hekalu lake; naye aketiye katika kile kiti cha enzi atatanda hema yake juu yao.
Derfor ere de foran Guds Trone og tjene ham Dag og Nat i hans Tempel; og han, som sidder paa Tronen, skal opslaa sit Telt over dem.
16 Kamwe hawataona njaa wala kiu tena. Jua halitawapiga wala joto lolote liunguzalo.
De skulle ikke hungre mere, ej heller tørste mere, ej heller skal Solen eller nogen Hede falde paa dem.
17 Kwa maana Mwana-Kondoo aliyeko katikati ya kile kiti cha enzi atakuwa Mchungaji wao; naye atawaongoza kwenda kwenye chemchemi za maji yaliyo hai. Naye Mungu atafuta kila chozi kutoka macho yao.”
Thi Lammet, som er midt for Tronen, skal vogte dem og lede dem til Livets Vandkilder; og Gud skal aftørre hver Taare af deres Øjne.

< Ufunuo 7 >