< Ufunuo 7 >

1 Baada ya hili nikaona malaika wanne wakiwa wamesimama katika pembe nne za dunia, wakizuia hizo pepo nne za dunia, ili kwamba pasiwe na upepo utakaovuma juu ya nchi au juu ya bahari au juu ya mti wowote.
Potom jsem viděl, jak se čtyři andělé postavili do čtyř světových stran a bránili všem zhoubným vichrům, aby nezuřily na zemi, na moři ani v lesích.
2 Nikaona malaika mwingine akipanda kutoka mawio ya jua akiwa na muhuri wa Mungu aliye hai. Akawaita kwa sauti kubwa wale malaika wanne waliokuwa wamepewa mamlaka ya kuidhuru nchi na bahari, akisema,
Tu se na východě objevil ještě jiný anděl a v ruce držel Boží pečetidlo. Volal na ty čtyři anděly, kteří mohli zadržet nebo rozpoutat všeobecnou zkázu:
3 “Msiidhuru nchi wala bahari, wala miti, hadi tuwe tumetia muhuri kwenye vipaji vya nyuso za watumishi wa Mungu wetu.”
„Neškoďte zemi, moři ani lesům, dokud neoznačíme na čelech všechny, kdo slouží Bohu!“
4 Ndipo nikasikia idadi ya wale waliotiwa muhuri: yaani 144,000 kutoka makabila yote ya Israeli.
A byl oznámen počet těch označených: sto čtyřicet čtyři tisíce ze všech kmenů Izraele, to je po dvanácti tisících z každého z dvanácti kmenů:
5 Kutoka kabila la Yuda 12,000 walitiwa muhuri, kutoka kabila la Reubeni 12,000, kutoka kabila la Gadi 12,000,
Juda, Rúben, Gád, Ašer, Neftalí, Manases, Šimeón, Lévi, Isachar, Zabulón, Josef a Benjamín.
6 kutoka kabila la Asheri 12,000, kutoka kabila la Naftali 12,000, kutoka kabila la Manase 12,000,
7 kutoka kabila la Simeoni 12,000, kutoka kabila la Lawi 12,000, kutoka kabila la Isakari 12,000,
8 kutoka kabila la Zabuloni 12,000, kutoka kabila la Yosefu 12,000, na kutoka kabila la Benyamini 12,000.
9 Baada ya hili nikatazama na hapo mbele yangu palikuwa na umati mkubwa wa watu ambao hakuna yeyote awezaye kuuhesabu, kutoka kila taifa, kila kabila, kila jamaa na kila lugha, wamesimama mbele ya kile kiti cha enzi na mbele ya Mwana-Kondoo. Walikuwa wamevaa mavazi meupe na wakiwa wameshika matawi ya mitende mikononi mwao.
Pak jsem spatřil nesčíslné zástupy lidí všech národů, ras, kmenů i jazyků. Stáli před Božím trůnem a před Beránkem oblečeni do bílých oděvů, s palmovými listy v rukou
10 Nao walikuwa wakipiga kelele kwa sauti kubwa wakisema: “Wokovu una Mungu wetu, yeye aketiye kwenye kiti cha enzi, na Mwana-Kondoo!”
a hlasitě volali: „Sláva našemu zachránci, Bohu Králi a Beránkovi!“
11 Malaika wote walikuwa wamesimama kukizunguka kile kiti cha enzi na wale wazee ishirini na wanne na wale viumbe wanne wenye uhai. Wakaanguka kifudifudi mbele ya hicho kiti cha enzi na kumwabudu Mungu,
Také všichni andělé byli shromážděni kolem trůnu, kolem starců a čtyř bytostí. Poklekli a slavili Boha:
12 wakisema: “Amen! Sifa na utukufu na hekima na shukrani na heshima na uweza na nguvu viwe kwa Mungu wetu milele na milele. Amen!” (aiōn g165)
„Ano. Chvála, sláva a čest našemu Bohu! Dík jemu, moudrému, silnému a mocnému na věky. Amen!“ (aiōn g165)
13 Kisha mmoja wa wale wazee ishirini na wanne akaniuliza, “Ni nani hawa waliovaa mavazi meupe, nao wametoka wapi?”
Jeden z těch čtyřiadvaceti starců se mne zeptal: „Víš, kdo jsou ti lidé v bílých oděvech a odkud přicházejí?“
14 Nikamjibu, “Bwana, wewe wajua.” Naye akasema, “Hawa ni wale waliotoka katika ile dhiki kuu, nao wamefua mavazi yao katika damu ya Mwana-Kondoo na kuyafanya meupe kabisa.
Odpověděl jsem: „Nevím, pane, pověz mi to.“Řekl: „To jsou ti, kteří prošli velikým utrpením pro víru. Očistili se od každé poskvrny hříchu Kristovou krví.
15 Kwa hiyo, “Wako mbele ya kiti cha enzi cha Mungu na kumtumikia usiku na mchana katika hekalu lake; naye aketiye katika kile kiti cha enzi atatanda hema yake juu yao.
Teď stojí před Božím trůnem a slouží Bohu bez překážek dnem i nocí. On je bude chránit,
16 Kamwe hawataona njaa wala kiu tena. Jua halitawapiga wala joto lolote liunguzalo.
nebudou trpět hladem ani žízní, slunce ani jiný žár jim už neublíží.
17 Kwa maana Mwana-Kondoo aliyeko katikati ya kile kiti cha enzi atakuwa Mchungaji wao; naye atawaongoza kwenda kwenye chemchemi za maji yaliyo hai. Naye Mungu atafuta kila chozi kutoka macho yao.”
Beránek je povede, nasytí a napojí z pramenů životodárné vody a Bůh sám jim setře každou slzu z očí.“

< Ufunuo 7 >