< Ufunuo 6 >

1 Kisha nikaangalia wakati Mwana-Kondoo akivunja ile lakiri ya kwanza miongoni mwa zile saba. Ndipo nikasikia mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai akisema kwa sauti kama ya radi: “Njoo!”
And I saw when the Lamb opened one of the seals, and I heard one of the four living creatures saying, as it were a voice of thunder, “Come and behold!”
2 Nikatazama, na hapo mbele yangu alikuwepo farasi mweupe! Yeye aliyempanda alikuwa na upinde, naye akapewa taji, akampanda akatoka akiwa kama mshindi aelekeaye katika kushinda.
And I saw, and behold, a white horse, and he who is sitting on it is having a bow, and there was given to him a garland, and he went forth overcoming, and that he may overcome.
3 Alipoivunja ile lakiri ya pili, nikamsikia yule kiumbe wa pili mwenye uhai akisema, “Njoo!”
And when He opened the second seal, I heard the second living creature saying, “Come and behold!”
4 Ndipo akatokea farasi mwingine mwekundu sana. Yeye aliyempanda akapewa uwezo wa kuondoa amani duniani na kuwafanya watu wauane. Yeye akapewa upanga mkubwa.
And there went forth another horse—fire-colored, and to him who is sitting on it, there was given to him to take peace from the earth, and that they may slay one another, and there was given to him a great sword.
5 Mwana-kondoo alipoivunja ile lakiri ya tatu, nikamsikia yule kiumbe wa tatu mwenye uhai akisema, “Njoo!” Nikatazama, na mbele yangu alikuwepo farasi mweusi! Yeye aliyempanda alikuwa na mizani mkononi mwake.
And when He opened the third seal, I heard the third living creature saying, “Come and behold!” And I saw, and behold, a black horse, and he who is sitting on it is having a balance in his hand,
6 Ndipo nikasikia kile kilichokuwa kama sauti katikati ya wale viumbe wanne wenye uhai ikisema, “Kipimo kimoja cha ngano kwa mshahara wa kibarua wa siku moja, na vipimo vitatu vya shayiri kwa mshahara wa kibarua cha siku moja. Lakini usiharibu mafuta wala divai!”
and I heard a voice in the midst of the four living creatures saying, “A measure of wheat for a denarius, and three measures of barley for a denarius, and you may not injure the oil and the wine.”
7 Alipovunja ile lakiri ya nne, nikasikia sauti ya yule kiumbe wa nne mwenye uhai ikisema, “Njoo!”
And when He opened the fourth seal, I heard the voice of the fourth living creature saying, “Come and behold!”
8 Nikatazama, na hapo mbele yangu alikuwepo farasi mwenye rangi ya kijivujivu! Yeye aliyempanda aliitwa Mauti, naye Kuzimu alikuwa akimfuata nyuma yake kwa karibu. Wakapewa mamlaka juu ya robo ya dunia, kuua kwa upanga, njaa, tauni na kwa wanyama wakali wa dunia. (Hadēs g86)
And I saw, and behold, a pale horse, and he who is sitting on him—his name is Death, and Hades follows with him, and there was given to them authority to kill over the fourth part of the earth with sword, and with hunger, and with death, and by the beasts of the earth. (Hadēs g86)
9 Mwana-kondoo alipoivunja ile lakiri ya tano, nikaona chini ya madhabahu, roho za wale waliochinjwa kwa ajili ya neno la Mungu na kwa ajili ya ushuhuda walioutunza.
And when He opened the fifth seal, I saw under the altar the souls of those slain because of the word of God, and because of the testimony that they held,
10 Wakalia kwa sauti kuu, wakisema, “Hata lini, Ee Bwana Mwenyezi, uliye mtakatifu na mwaminifu, hutawahukumu na kulipiza kisasi juu ya watu waishio duniani kwa ajili ya damu yetu?”
and they were crying with a great voice, saying, “Until when, O Master, the Holy and the True, do You not judge and take vengeance of our blood from those dwelling on the earth?”
11 Kisha kila mmoja wao akapewa joho jeupe na wakaambiwa wangoje kwa muda kidogo zaidi, mpaka idadi ya ndugu zao na watumishi wenzao watakaouawa kama wao walivyouawa, itakapotimia.
And there was given to each one a white robe, and it was said to them that they may rest themselves yet a short time, until may also be fulfilled their fellow-servants and their brothers, who are about to be killed—even as they.
12 Nikatazama akiivunja ile lakiri ya sita. Pakatokea tetemeko kuu la nchi, na jua likawa jeusi kama nguo ya gunia iliyotengenezwa kwa singa za mbuzi, na mwezi wote ukawa mwekundu kama damu.
And I saw when He opened the sixth seal, and behold, a great earthquake came, and the sun became black as sackcloth of hair, and the moon became as blood,
13 Nyota zilizo angani zikaanguka ardhini kama vile matunda ya mtini yasiyokomaa yaangukavyo wakati mti wake unapotikiswa na upepo mkali.
and the stars of Heaven fell to the earth—as a fig tree casts her unripe figs, being shaken by a great wind—
14 Anga ikatoweka kama vile karatasi isokotwavyo, na kila mlima na kila kisiwa kikaondolewa mahali pake.
and the sky departed as a scroll rolled up, and every mountain and island were moved out of their places;
15 Ndipo wafalme wa dunia, wakuu wote, majemadari, matajiri, wenye nguvu na kila mtu, mtumwa na mtu huru, wakajificha katika mapango na kwenye miamba ya milima.
and the kings of the earth, and the great men, and the rich, and the chiefs of thousands, and the mighty, and every servant, and every freeman, hid themselves in the dens, and in the rocks of the mountains,
16 Wakaiita milima na miamba wakisema, “Tuangukieni, mkatufiche na uso wake yeye aketiye kwenye kiti cha enzi, na mkatuepushe na ghadhabu ya Mwana-Kondoo!
and they say to the mountains and to the rocks, “Fall on us, and hide us from the face of Him who is sitting on the throne, and from the anger of the Lamb,”
17 Kwa maana siku ile kuu ya ghadhabu yao imewadia. Je, ni nani awezaye kustahimili?”
because the great day of His anger has come, and who is able to stand?

< Ufunuo 6 >