< Ufunuo 5 >

1 Kisha nikaona katika mkono wake wa kuume wa yule aliyeketi kwenye kile kiti cha enzi, kitabu kilichoandikwa ndani na upande wa nje, kikiwa kimefungwa kwa lakiri saba.
Rêngsukmuna ânsung ngâipu kut changtieng han lekhazuot ku mua; maha kângnika ânziek mohôr sari ngei mohôr ânnam leta ânthom ani.
2 Nami nikamwona malaika mwenye nguvu akitangaza kwa sauti kuu, akisema, “Ni nani anayestahili kuzivunja hizo lakiri na kukifungua kitabu?”
Vântîrton râttak ku mua, rôl inringtakin, “Tu mo aminpipna mo-onga, lekhazuot ha aphar thei rang ni zoi?” tiin tânghâi ku mu sa.
3 Lakini hapakuwa na yeyote mbinguni wala duniani au chini ya dunia aliyeweza kukifungua hicho kitabu wala hata kutazama ndani yake.
Aniatachu invâna, pilchunga aninônchu rammuol nuoia khom tute lekhazuot mo-onga asûnga a en thei rang reng om mak ngei.
4 Nikalia sana sana kwa sababu hakuonekana yeyote anayestahili kukifungua hicho kitabu wala kutazama ndani yake.
Lekhazuot hah a mo-onga, asûnga a en theiruo tute an om loi sikin ka chap ngungûia.
5 Kisha, mmoja wa wale wazee akaniambia, “Usilie! Tazama, Simba wa kabila la Yuda, wa Uzao wa Daudi, ameshinda. Yeye ndiye anayeweza kukifungua hicho kitabu na kuvunja hizo lakiri zake saba.”
Hanchu upangei lâia inkhatin ko kôm, “Chap no roh. En roh! Juda jâta ikeibaknei, David richisuonpâra roiinpui han, a menea, male ama han aminpipna sari ngei hah akheka lekhazuot hah a mo-ong thei zoi,” a tia.
6 Ndipo nikaona katikati ya kile kiti cha enzi na wale viumbe wenye uhai wanne na miongoni mwa wale wazee, Mwana-Kondoo amesimama, akiwa kama amechinjwa. Alikuwa na pembe saba na macho saba, ambazo ndizo zile Roho saba za Mungu zilizotumwa duniani pote.
Hanchu Belrite hah rêngsukmun alâitak han ânding ku mua, iring parân minli ngei le upangei hah arihîla an om ani. Belrite that sai anghan ânlanga. Maha rikingei sari le mitngei sari a dôna, ma ngei hah Pathien ratha sari ngei pilchung pumpuia tîra om ngei hah an ni.
7 Huyo Mwana-Kondoo akaja na kukitwaa kile kitabu kutoka kwenye mkono wa kuume wa yule aliyeketi kwenye kile kiti cha enzi.
Belrite hah a sea male rêngsukmuna ânsung ngâipu kut changtieng renga lekhazuot hah ava lâk zoia.
8 Alipokwisha kukitwaa kile kitabu, wale viumbe wenye uhai wanne pamoja na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele ya yule Mwana-Kondoo. Kila mmoja wao alikuwa na kinubi, nao walikuwa wameshika mabakuli ya dhahabu yaliyojaa uvumba, ambayo ni maombi ya watakatifu.
Ma anghan a thoa anîn chu, iring parân minli ngei le upa sômnikleiminli ngei han serânda le rângkachak khuriâingei mirimhoia sip chôi pakin Belrite makunga han an inboka, ma ngei hah Pathien mingei chubaithonangei ani.
9 Nao wakaimba wimbo mpya, wakisema: “Wewe unastahili kukitwaa kitabu na kuzivunja lakiri zake, kwa sababu ulichinjwa na kwa damu yako ukamnunulia Mungu watu kutoka kila kabila, kila lugha, kila jamaa na kila taifa.
Anni ngei han lâ thar an thoa: “Nangma chu lekhazuot lâk theiruo le a minpipnangei kheka mo-ong thei ni ni. Thatin no oma, male thina nên pêkna han Pathien ta rangin jâttina mingei, chongtina mingei, namtina mingei le ruitina mingei no rochôk zoi.
10 Wewe umewafanya hawa wawe ufalme na makuhani wa kumtumikia Mungu wetu, nao watatawala duniani.”
Kin Pathien sintho rangin rêngrama ochaingei ni sin ngei zoi ani, male anni ngei han pilchunga roijêk an tih.”
11 Kisha nikatazama, nikasikia sauti za malaika wengi wakiwa wamekizunguka kile kiti cha enzi, pamoja na wale viumbe wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne. Idadi yao ilikuwa kumi elfu mara kumi elfu na maelfu ya maelfu.
Ko hong en nôka, male vântîrtonngei rôl ki rieta, isâng tamtak le isângrazasôm tamtak an ni! rêngsukmun rihîla han an indinga, iring parân minli ngei le upangei khom an om sa,
12 Nao waliimba kwa sauti kuu, wakisema: “Anastahili Mwana-Kondoo, yeye aliyechinjwa, kupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na sifa!”
male rôl inringtakin lâ an thoa: “Belrite thata omsai hih sinthotheina, neinunsampâr, vârna le râtna, miritna, roiinpuina le minpâkna man theiruo piel ani!”
13 Kisha nikasikia kila kiumbe mbinguni na duniani, chini ya nchi na baharini na vyote vilivyomo ndani yake vikiimba: “Sifa na heshima na utukufu na uweza ni vyake yeye aketiye juu ya hicho kiti cha enzi na kwa Mwana-Kondoo, milele na milele!” (aiōn g165)
Male invâna, pilchunga, rammuol nuoia, le tuikhanglien sûnga iring parânngei murdi vânnuoia iring murdi ngei le lâ an thoa: “Rêngsukmuna ânsung ngâipu le Belrite kôm han, minpâkna le miritna, roiinpuina le sinthotheina ngei, tuonsôt tuonsôtin om rese!” (aiōn g165)
14 Wale viumbe wenye uhai wanne wakasema, “Amen!” Nao wale wazee ishirini na wanne wakaanguka kifudifudi wakaabudu.
Iring parân minli ngei han, “Amen!” tiin an thuona, male upangei han inbokin chubai an mûk zoi.

< Ufunuo 5 >