< Ufunuo 5 >

1 Kisha nikaona katika mkono wake wa kuume wa yule aliyeketi kwenye kile kiti cha enzi, kitabu kilichoandikwa ndani na upande wa nje, kikiwa kimefungwa kwa lakiri saba.
And I saw lying in the right hand of Him who sat on the throne a book written on both sides and closely sealed with seven seals.
2 Nami nikamwona malaika mwenye nguvu akitangaza kwa sauti kuu, akisema, “Ni nani anayestahili kuzivunja hizo lakiri na kukifungua kitabu?”
And I saw a mighty angel who was exclaiming in a loud voice, "Who is worthy to open the book and break its seals?"
3 Lakini hapakuwa na yeyote mbinguni wala duniani au chini ya dunia aliyeweza kukifungua hicho kitabu wala hata kutazama ndani yake.
But no one in Heaven, or on earth, or under the earth, was able to open the book or look into it.
4 Nikalia sana sana kwa sababu hakuonekana yeyote anayestahili kukifungua hicho kitabu wala kutazama ndani yake.
And while I was weeping bitterly, because no one was found worthy to open the book or look into it,
5 Kisha, mmoja wa wale wazee akaniambia, “Usilie! Tazama, Simba wa kabila la Yuda, wa Uzao wa Daudi, ameshinda. Yeye ndiye anayeweza kukifungua hicho kitabu na kuvunja hizo lakiri zake saba.”
one of the Elders said to me, "Do not weep. The Lion which belongs to the tribe of Judah, the Root of David, has triumphed, and will open the book and break its seven seals."
6 Ndipo nikaona katikati ya kile kiti cha enzi na wale viumbe wenye uhai wanne na miongoni mwa wale wazee, Mwana-Kondoo amesimama, akiwa kama amechinjwa. Alikuwa na pembe saba na macho saba, ambazo ndizo zile Roho saba za Mungu zilizotumwa duniani pote.
Then, midway between the throne and the four living creatures, I saw a Lamb standing among the Elders. He looked as if He had been offered in sacrifice, and He had seven horns and seven eyes. The last-named are the seven Spirits of God, and have been sent far and wide into all the earth.
7 Huyo Mwana-Kondoo akaja na kukitwaa kile kitabu kutoka kwenye mkono wa kuume wa yule aliyeketi kwenye kile kiti cha enzi.
So He comes, and now He has taken the book out of the right hand of Him who is seated on the throne.
8 Alipokwisha kukitwaa kile kitabu, wale viumbe wenye uhai wanne pamoja na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele ya yule Mwana-Kondoo. Kila mmoja wao alikuwa na kinubi, nao walikuwa wameshika mabakuli ya dhahabu yaliyojaa uvumba, ambayo ni maombi ya watakatifu.
And when He had taken the book, the four living creatures and the twenty-four Elders fell down before the Lamb, having each of them a harp and bringing golden bowls full of incense, which represent the prayers of God's people.
9 Nao wakaimba wimbo mpya, wakisema: “Wewe unastahili kukitwaa kitabu na kuzivunja lakiri zake, kwa sababu ulichinjwa na kwa damu yako ukamnunulia Mungu watu kutoka kila kabila, kila lugha, kila jamaa na kila taifa.
And now they sing a new song. "It is fitting," they say, "that Thou shouldst be the One to take the book And break its seals; Because Thou hast been offered in sacrifice, And hast purchased for God with Thine own blood Some out of every tribe and language and people and nation,
10 Wewe umewafanya hawa wawe ufalme na makuhani wa kumtumikia Mungu wetu, nao watatawala duniani.”
And hast formed them into a Kingdom to be priests to our God, And they reign over the earth."
11 Kisha nikatazama, nikasikia sauti za malaika wengi wakiwa wamekizunguka kile kiti cha enzi, pamoja na wale viumbe wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne. Idadi yao ilikuwa kumi elfu mara kumi elfu na maelfu ya maelfu.
And I looked, and heard what seemed to be the voices of countless angels on every side of the throne, and of the living creatures and the Elders. Their number was myriads of myriads and thousands of thousands,
12 Nao waliimba kwa sauti kuu, wakisema: “Anastahili Mwana-Kondoo, yeye aliyechinjwa, kupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na sifa!”
and in loud voices they were singing, "It is fitting that the Lamb which has been offered in sacrifice should receive all power and riches and wisdom and might and honor and glory and blessing."
13 Kisha nikasikia kila kiumbe mbinguni na duniani, chini ya nchi na baharini na vyote vilivyomo ndani yake vikiimba: “Sifa na heshima na utukufu na uweza ni vyake yeye aketiye juu ya hicho kiti cha enzi na kwa Mwana-Kondoo, milele na milele!” (aiōn g165)
And as for every created thing in Heaven and on earth and under the earth and on the sea, and everything that was in any of these, I heard them say, "To Him who is seated on the throne, And to the Lamb, Be ascribed all blessing and honor And glory and might, Until the Ages of the Ages!" (aiōn g165)
14 Wale viumbe wenye uhai wanne wakasema, “Amen!” Nao wale wazee ishirini na wanne wakaanguka kifudifudi wakaabudu.
Then the four living creatures said "Amen," and the Elders fell down and worshipped.

< Ufunuo 5 >