< Ufunuo 5 >
1 Kisha nikaona katika mkono wake wa kuume wa yule aliyeketi kwenye kile kiti cha enzi, kitabu kilichoandikwa ndani na upande wa nje, kikiwa kimefungwa kwa lakiri saba.
And I saw upon the right hand of the one sitting upon the throne a book having been written within and without, having been sealed with seven seals.
2 Nami nikamwona malaika mwenye nguvu akitangaza kwa sauti kuu, akisema, “Ni nani anayestahili kuzivunja hizo lakiri na kukifungua kitabu?”
And I saw a mighty angel crying with a great voice, Who is able to open the book, and to loose its seals?
3 Lakini hapakuwa na yeyote mbinguni wala duniani au chini ya dunia aliyeweza kukifungua hicho kitabu wala hata kutazama ndani yake.
And no one in the heaven, nor upon the earth, nor beneath the earth, was able to open the book, and to look into it.
4 Nikalia sana sana kwa sababu hakuonekana yeyote anayestahili kukifungua hicho kitabu wala kutazama ndani yake.
And I was weeping much, because no one was found worthy to open the book, or to look into it.
5 Kisha, mmoja wa wale wazee akaniambia, “Usilie! Tazama, Simba wa kabila la Yuda, wa Uzao wa Daudi, ameshinda. Yeye ndiye anayeweza kukifungua hicho kitabu na kuvunja hizo lakiri zake saba.”
And one of the elders says to me; Weep not: behold, the Lion of the tribe of Judah, the Root of David, has conquered to open the book, and the seven seals.
6 Ndipo nikaona katikati ya kile kiti cha enzi na wale viumbe wenye uhai wanne na miongoni mwa wale wazee, Mwana-Kondoo amesimama, akiwa kama amechinjwa. Alikuwa na pembe saba na macho saba, ambazo ndizo zile Roho saba za Mungu zilizotumwa duniani pote.
And I saw, in the midst of the throne and the four living creatures, and in the midst of the elders, the Lamb standing as having been slain, having seven horns and seven eyes, which are the seven Spirits of God having been sent into all the earth.
7 Huyo Mwana-Kondoo akaja na kukitwaa kile kitabu kutoka kwenye mkono wa kuume wa yule aliyeketi kwenye kile kiti cha enzi.
And he came and took the book out of the right hand of the one sitting upon the throne.
8 Alipokwisha kukitwaa kile kitabu, wale viumbe wenye uhai wanne pamoja na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele ya yule Mwana-Kondoo. Kila mmoja wao alikuwa na kinubi, nao walikuwa wameshika mabakuli ya dhahabu yaliyojaa uvumba, ambayo ni maombi ya watakatifu.
And when he took the book, the four living creatures and the twenty-four elders fell down before the Lamb, having each a harp, and golden bowls filled with incense, which are the prayers of the saints.
9 Nao wakaimba wimbo mpya, wakisema: “Wewe unastahili kukitwaa kitabu na kuzivunja lakiri zake, kwa sababu ulichinjwa na kwa damu yako ukamnunulia Mungu watu kutoka kila kabila, kila lugha, kila jamaa na kila taifa.
And they sing a new song, saying, Thou art worthy to receive the book, and to open its seals: because thou wast slain, and didst with thy blood redeem unto God out of every tribe, and tongue, and people, and nation;
10 Wewe umewafanya hawa wawe ufalme na makuhani wa kumtumikia Mungu wetu, nao watatawala duniani.”
and didst make them a kingdom and priests unto our God: and they shall reign on the earth.
11 Kisha nikatazama, nikasikia sauti za malaika wengi wakiwa wamekizunguka kile kiti cha enzi, pamoja na wale viumbe wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne. Idadi yao ilikuwa kumi elfu mara kumi elfu na maelfu ya maelfu.
And I saw, and I heard as it were a voice of many angels round about the throne, and the living creatures, and the elders: and their number was myriads of myriads, and thousands of thousands;
12 Nao waliimba kwa sauti kuu, wakisema: “Anastahili Mwana-Kondoo, yeye aliyechinjwa, kupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na sifa!”
saying with a great voice; Worthy is the Lamb that was slain to receive power, and riches, and wisdom, and might, and honor, and glory, and blessing.
13 Kisha nikasikia kila kiumbe mbinguni na duniani, chini ya nchi na baharini na vyote vilivyomo ndani yake vikiimba: “Sifa na heshima na utukufu na uweza ni vyake yeye aketiye juu ya hicho kiti cha enzi na kwa Mwana-Kondoo, milele na milele!” (aiōn )
And I heard all creation, which is in the heaven, and upon the earth, and beneath the earth, and in the sea, and all things which are in them, indeed saying, to the one sitting upon the throne, and to the Lamb, blessing, and honor, and glory, and dominion, unto the ages of the ages. (aiōn )
14 Wale viumbe wenye uhai wanne wakasema, “Amen!” Nao wale wazee ishirini na wanne wakaanguka kifudifudi wakaabudu.
And the four living creatures continued to say, Amen. And the elders fell and worshiped.