< Ufunuo 5 >

1 Kisha nikaona katika mkono wake wa kuume wa yule aliyeketi kwenye kile kiti cha enzi, kitabu kilichoandikwa ndani na upande wa nje, kikiwa kimefungwa kwa lakiri saba.
Tu jsem uviděl, že onen sedící na trůnu má v pravé ruce svitek popsaný z obou stran, zapečetěný sedmi pečetěmi.
2 Nami nikamwona malaika mwenye nguvu akitangaza kwa sauti kuu, akisema, “Ni nani anayestahili kuzivunja hizo lakiri na kukifungua kitabu?”
Jeden mocný anděl zvolal silným hlasem: „Kdo může rozlomit tyto pečetě a rozvinout ten svitek?“
3 Lakini hapakuwa na yeyote mbinguni wala duniani au chini ya dunia aliyeweza kukifungua hicho kitabu wala hata kutazama ndani yake.
Nikde se však nikdo nenašel, kdo by to mohl učinit a přečíst. To mě zarmoutilo, že jsem až plakal.
4 Nikalia sana sana kwa sababu hakuonekana yeyote anayestahili kukifungua hicho kitabu wala kutazama ndani yake.
5 Kisha, mmoja wa wale wazee akaniambia, “Usilie! Tazama, Simba wa kabila la Yuda, wa Uzao wa Daudi, ameshinda. Yeye ndiye anayeweza kukifungua hicho kitabu na kuvunja hizo lakiri zake saba.”
Ale jeden z těch starců mě potěšil: „Neplač! Ježíš, Lev z Judova kmene, Davidův potomek zvítězil! On proto může rozlomit ty pečetě a svitek rozvinout.“
6 Ndipo nikaona katikati ya kile kiti cha enzi na wale viumbe wenye uhai wanne na miongoni mwa wale wazee, Mwana-Kondoo amesimama, akiwa kama amechinjwa. Alikuwa na pembe saba na macho saba, ambazo ndizo zile Roho saba za Mungu zilizotumwa duniani pote.
Setřel jsem slzy a vidím, že v kruhu starců, mezi čtyřmi bytostmi u trůnu, stojí Beránek, s jizvami po smrtelných ranách. Na hlavě má znamení plnosti síly a vševědoucnosti Božího Ducha.
7 Huyo Mwana-Kondoo akaja na kukitwaa kile kitabu kutoka kwenye mkono wa kuume wa yule aliyeketi kwenye kile kiti cha enzi.
Beránek přistoupil až k sedícímu na trůnu a z jeho pravice přijal ten svitek.
8 Alipokwisha kukitwaa kile kitabu, wale viumbe wenye uhai wanne pamoja na wale wazee ishirini na wanne wakaanguka mbele ya yule Mwana-Kondoo. Kila mmoja wao alikuwa na kinubi, nao walikuwa wameshika mabakuli ya dhahabu yaliyojaa uvumba, ambayo ni maombi ya watakatifu.
Jakmile se to stalo, ty čtyři bytosti a dvacet čtyři starci se mu hluboce uklonili. Každý z nich měl harfu a zlatou nádobu z níž jako vonný dým vystupovaly modlitby věřících.
9 Nao wakaimba wimbo mpya, wakisema: “Wewe unastahili kukitwaa kitabu na kuzivunja lakiri zake, kwa sababu ulichinjwa na kwa damu yako ukamnunulia Mungu watu kutoka kila kabila, kila lugha, kila jamaa na kila taifa.
Začali zpívat novou píseň: „Ty jediný jsi hoden vzít tento zápis a rozlomit pečetě! Vždyť jsi položil svůj život a z otroctví hříchu jsi Bohu vykoupil svou krví lidi všech kmenů, jazyků, tříd i národů.
10 Wewe umewafanya hawa wawe ufalme na makuhani wa kumtumikia Mungu wetu, nao watatawala duniani.”
Udělal jsi je Božími králi a knězi na zemi.“
11 Kisha nikatazama, nikasikia sauti za malaika wengi wakiwa wamekizunguka kile kiti cha enzi, pamoja na wale viumbe wenye uhai wanne na wale wazee ishirini na wanne. Idadi yao ilikuwa kumi elfu mara kumi elfu na maelfu ya maelfu.
Tu se k nim připojil obrovský zástup andělů, kteří obklopovali Boží trůn. Byly jich statisíce.
12 Nao waliimba kwa sauti kuu, wakisema: “Anastahili Mwana-Kondoo, yeye aliyechinjwa, kupokea uweza na utajiri na hekima na nguvu na heshima na utukufu na sifa!”
Volali: „Obětovanému Beránkovi patří všechna moc, bohatství, moudrost i síla, čest, sláva i dík.“
13 Kisha nikasikia kila kiumbe mbinguni na duniani, chini ya nchi na baharini na vyote vilivyomo ndani yake vikiimba: “Sifa na heshima na utukufu na uweza ni vyake yeye aketiye juu ya hicho kiti cha enzi na kwa Mwana-Kondoo, milele na milele!” (aiōn g165)
A všechno tvorstvo v nebi, na zemi, v hlubinách, v mořích – prostě celý vesmír se rozezvučel: „Bohu na trůnu a Beránkovi díky, čest, sláva a moc na věky věků!“ (aiōn g165)
14 Wale viumbe wenye uhai wanne wakasema, “Amen!” Nao wale wazee ishirini na wanne wakaanguka kifudifudi wakaabudu.
Čtyři bytosti kolem trůnu uzavřely chvalozpěvy společným „Amen!“A čtyřiadvacet starců se hluboce poklonilo.

< Ufunuo 5 >