< Ufunuo 4 >
1 Baada ya mambo hayo nilitazama, nami nikaona mbele yangu mlango uliokuwa wazi mbinguni. Nayo ile sauti niliyokuwa nimeisikia hapo mwanzo ikisema nami kama tarumbeta ikasema, “Njoo, huku, nami nitakuonyesha yale ambayo hayana budi kutokea baada ya haya.”
After these things I saw, and behold, a door opened in heaven; and the first voice which I heard was as of a trumpet speaking to me; and it said, Come up hither, and I will shew thee things which must come to pass hereafter.
2 Ghafula nilikuwa katika Roho, na hapo mbele yangu kilikuwepo kiti cha enzi mbinguni, kikiwa kimekaliwa na mtu.
And immmediately I was in the Spirit: and behold, a throne was set in heaven, and one sitting on the throne.
3 Aliyekuwa amekikalia alikuwa anaonekana kama yaspi na akiki. Kukizunguka kile kiti cha enzi palikuwa na upinde wa mvua ulioonekana kama zumaridi.
And He that sat upon it, was to look at like a jasper and a sardine stone, and there was a rainbow round the throne like the appearance of an emerald.
4 Kukizunguka hicho kiti cha enzi palikuwa na viti vingine vya enzi ishirini na vinne, na juu ya hivyo viti walikuwa wameketi wazee ishirini na wanne. Walivaa mavazi meupe, na walikuwa na taji za dhahabu vichwani mwao.
And around the throne were four and twenty seats: and upon the seats I saw twenty four elders sitting, clothed in white garments; and they had upon their heads crowns of gold.
5 Kwenye kile kiti cha enzi palikuwa panatoka miali ya umeme wa radi, ngurumo na sauti za radi. Mbele ya kiti cha enzi, taa saba zilikuwa zinawaka. Hizi ndizo roho saba za Mungu.
And out of the throne came lightnings, and thunders, and voices: and there were seven lamps of fire burning before the throne; which are the seven spirits of God.
6 Pia mbele ya kiti cha enzi palikuwa na kile kilichoonekana kama bahari ya kioo, iliyokuwa angavu kama bilauri. Katikati, kukizunguka kile kiti cha enzi, kulikuwa na viumbe wanne wenye uhai, wakiwa wamejawa na macho mbele na nyuma.
And before the throne was a sea of glass, like crystal: and in the middle of the throne, and the circle of it, were four animate beings full of eyes before and behind.
7 Kiumbe wa kwanza mwenye uhai alikuwa kama simba, wa pili alikuwa kama ngʼombe dume, wa tatu alikuwa na uso kama wa mwanadamu, na wa nne alikuwa kama tai anayeruka.
And the first was like a lion, and the second like a calf, and the third had a face like a man, and the fourth was like a flying eagle.
8 Kila mmoja wa hawa viumbe wanne wenye uhai alikuwa na mabawa sita, na kujawa na macho pande zote hadi chini ya mabawa. Usiku na mchana hawaachi kusema:
And the four animals had each of them six wings round about, and within were full of eyes; and they cease not day and night saying, Holy, holy, holy is the Lord God almighty, who was, and who is, and who is to come.
9 Kila mara viumbe hao wanne wenye uhai wanapomtukuza, kumheshimu na kumshukuru yeye aketiye kwenye kile kiti cha enzi, tena aishiye milele na milele, (aiōn )
And when the animals give glory and honor and thanks to Him that sitteth on the throne, who liveth for ever and ever, (aiōn )
10 wale wazee ishirini na wanne huanguka mbele zake aketiye kwenye kiti cha enzi na kumwabudu yeye aliye hai milele na milele. Huziweka taji zao mbele ya kiti cha enzi, wakisema: (aiōn )
the four and twenty elders fall down before Him that sitteth on the throne, and worship Him that liveth for ever and ever, (aiōn )
11 “Bwana wetu na Mungu wetu, wewe unastahili kupokea utukufu na heshima na uweza, kwa maana ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa mapenzi yako viliumbwa na vimekuwako.”
and cast their crowns before the throne, saying, Worthy art thou, O Lord, to receive glory and honor and power; for thou hast created all things, and by thy will they exist, and were created.