< Ufunuo 4 >
1 Baada ya mambo hayo nilitazama, nami nikaona mbele yangu mlango uliokuwa wazi mbinguni. Nayo ile sauti niliyokuwa nimeisikia hapo mwanzo ikisema nami kama tarumbeta ikasema, “Njoo, huku, nami nitakuonyesha yale ambayo hayana budi kutokea baada ya haya.”
After these things I saw, and behold, a door was opened in heaven; and the first voice which I heard, like the voice of a trumpet speaking with me, said: Come up hither, and I will show you things that must be hereafter.
2 Ghafula nilikuwa katika Roho, na hapo mbele yangu kilikuwepo kiti cha enzi mbinguni, kikiwa kimekaliwa na mtu.
And immediately I was in spirit; and behold, a throne was set in heaven, and one sat on the throne;
3 Aliyekuwa amekikalia alikuwa anaonekana kama yaspi na akiki. Kukizunguka kile kiti cha enzi palikuwa na upinde wa mvua ulioonekana kama zumaridi.
and he that sat was, in appearance, like a jasper and sardine-stone: and there was round about the throne a rainbow, in appearance like an emerald.
4 Kukizunguka hicho kiti cha enzi palikuwa na viti vingine vya enzi ishirini na vinne, na juu ya hivyo viti walikuwa wameketi wazee ishirini na wanne. Walivaa mavazi meupe, na walikuwa na taji za dhahabu vichwani mwao.
And round about the throne were twenty-four thrones; and on the thrones there sat twenty-four elders, clothed in white raiment; and on their heads were crowns of gold.
5 Kwenye kile kiti cha enzi palikuwa panatoka miali ya umeme wa radi, ngurumo na sauti za radi. Mbele ya kiti cha enzi, taa saba zilikuwa zinawaka. Hizi ndizo roho saba za Mungu.
And out of the throne there went lightnings and thunderings and voices; and seven lamps of fire were burning before the throne: these are the seven spirits of God.
6 Pia mbele ya kiti cha enzi palikuwa na kile kilichoonekana kama bahari ya kioo, iliyokuwa angavu kama bilauri. Katikati, kukizunguka kile kiti cha enzi, kulikuwa na viumbe wanne wenye uhai, wakiwa wamejawa na macho mbele na nyuma.
And before the throne there was a sea of glass, like crystal. And in the midst of the throne, and round about the throne, were four living creatures full of eyes before and behind.
7 Kiumbe wa kwanza mwenye uhai alikuwa kama simba, wa pili alikuwa kama ngʼombe dume, wa tatu alikuwa na uso kama wa mwanadamu, na wa nne alikuwa kama tai anayeruka.
And the first living creature was like a lion, and the second living creature was like a calf, and the third living creature had the face of a man, and the fourth living creature was like a flying eagle.
8 Kila mmoja wa hawa viumbe wanne wenye uhai alikuwa na mabawa sita, na kujawa na macho pande zote hadi chini ya mabawa. Usiku na mchana hawaachi kusema:
And the four living creatures had each of them six wings about him; and they are full of eyes within; and they have no rest day and night, saying, Holy, holy, holy is the Lord God, the Almighty, who was, and is, and is to come.
9 Kila mara viumbe hao wanne wenye uhai wanapomtukuza, kumheshimu na kumshukuru yeye aketiye kwenye kile kiti cha enzi, tena aishiye milele na milele, (aiōn )
And when the living creatures give glory and honor and thanks to him that sits on the throne, who lives from age to age, (aiōn )
10 wale wazee ishirini na wanne huanguka mbele zake aketiye kwenye kiti cha enzi na kumwabudu yeye aliye hai milele na milele. Huziweka taji zao mbele ya kiti cha enzi, wakisema: (aiōn )
the twenty-four elders fall down before him that sits on the throne, and worship him that lives from age to age, and throw their crowns before the throne, saying: (aiōn )
11 “Bwana wetu na Mungu wetu, wewe unastahili kupokea utukufu na heshima na uweza, kwa maana ndiwe uliyeviumba vitu vyote, na kwa mapenzi yako viliumbwa na vimekuwako.”
Thou art worthy, O Lord, to receive glory and honor and power: for thou hast created all things, and by thy will they exist, and were created.