< Ufunuo 3 >
1 “Kwa malaika wa kanisa lililoko Sardi andika: “Haya ndiyo maneno ya aliye na zile Roho sabaza Mungu na zile nyota saba. Nayajua matendo yako, kwamba una sifa ya kuwa hai, lakini umekufa.
And by the messenger of the congregation in Sardis, write: These things says he who has the seven spirits of God, and the seven stars: I know your works, that you have a name that you live, but are dead.
2 Amka! Nawe uyaimarishe yale yaliyosalia na yaliyo karibu kufa, kwa maana sikuona kwamba kazi zako zimekamilika machoni pa Mungu wangu.
Be watchful, and strengthen the things which remain, which are ready to die: for I have not found your works filled up in the sight of God.
3 Kumbuka basi yale uliyoyapokea na kuyasikia, yatii na ukatubu. Lakini usipoamka, nitakuja kama mwizi wala hutajua saa nitakayokuja kwako.
Remember, therefore, how you have received and heard, and hold fast, and reform: therefore, unless you are watchful, I will come upon you as thief, and you shall not know what hour I will come upon you.
4 “Lakini bado una watu wachache katika Sardi ambao hawajayachafua mavazi yao. Wao wataenda pamoja nami, wakiwa wamevaa mavazi meupe, kwa maana wanastahili.
But you have a few names in Sardis, who have not polluted their garments: and they shall walk with me in white, for they are worthy.
5 Yeye ashindaye atavikwa vazi jeupe kama wao. Sitafuta jina lake kutoka kitabu cha uzima, bali nitalikiri jina lake mbele za Baba yangu na mbele za malaika wake.
As for the conqueror, he shall be clothed in white apparel; and I will not blot out his name from the book of life; but I will confess his name before my Father, and before his angels.
6 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa.
Whoever has an ear, let him hear what the Spirit says to the congregations.
7 “Kwa malaika wa kanisa lililoko Filadelfia andika: “Haya ndiyo maneno yake yeye aliye mtakatifu na wa kweli, yeye aliye na ufunguo wa Daudi. Anachokifungua hakuna awezaye kukifunga, wala anachokifunga hakuna awezaye kukifungua.
And by the messenger of the congregation in Philadelphia, write: These things says the Holy One, the True One; who has the key, the Son of David; he who opens and no man shuts; and shuts, and no man opens:
8 Nayajua matendo yako. Tazama, nimeweka mbele yako mlango uliofunguliwa, wala hakuna awezaye kuufunga. Ninajua kwamba una nguvu kidogo lakini umelishika neno langu wala hukulikana Jina langu.
I know your works: behold, I have set before you an open door, and no man can shut it; because you have little strength, and have kept my word, and have not denied my name.
9 Nitawafanya wale wa sinagogi la Shetani, wale ambao husema kuwa ni Wayahudi lakini sio, bali ni waongo, nitawafanya waje wapige magoti miguuni pako, na wakiri ya kwamba nimekupenda.
Behold, I will give of those--who are of the assembly of Satan; who say they are Jews, and are not, but do lie; behold--I will make them to come and worship before your feet; and they shall know that I have loved you.
10 Kwa kuwa umeshika amri yangu ya kuvumilia katika saburi, nitakulinda katika saa ya kujaribiwa inayokuja ulimwenguni pote, ili kuwajaribu wote wakaao duniani.
Because you have kept the word of my patience, I will also keep you from the hour of temptation, which shall come upon all the world, to try the inhabitants of the earth.
11 “Ninakuja upesi. Shika sana ulicho nacho, ili mtu asije akaichukua taji yako.
I come quickly: keep that which you have, that no man take your crown.
12 Yeye ashindaye nitamfanya kuwa nguzo katika hekalu la Mungu wangu, wala hatatoka humo kamwe. Nitaandika juu yake Jina la Mungu wangu na jina la mji mkubwa wa Mungu wangu, Yerusalemu mpya, ambao unashuka kutoka mbinguni kwa Mungu wangu. Nami pia nitaandika juu yake Jina langu jipya.
As for the conqueror, I will make him a pillar in the temple of my God, and he shall go out no more: and I will inscribe upon him the name of my God, and the name of the city of my God, the New Jerusalem, which is to come down from heaven, from my God; and my new name.
13 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa.
Whoever has an ear, let him hear what the Spirit says to the congregations.
14 “Kwa malaika wa kanisa lililoko Laodikia andika: “Haya ndiyo maneno yake yeye aliye Amen, shahidi mwaminifu na wa kweli, mtawala wa uumbaji wote wa Mungu.
And by the messenger of the congregation in Laodicea, write: These things says the AMEN, the Faithful and true Witness, the Beginning of the creation of God:
15 Nayajua matendo yako, ya kwamba wewe si baridi wala si moto. Afadhali ungelikuwa moja au lingine.
I know your works, that you are neither cold nor hot: I wish you were either cold or hot.
16 Hivyo kwa kuwa u vuguvugu, si baridi wala moto, nitakutapika utoke kinywani mwangu.
Therefore, because you are lukewarm, and neither cold nor hot, I will vomit you out of my mouth.
17 Kwa maana unasema: ‘Mimi ni tajiri, nimejilimbikizia mali, wala sihitaji kitu chochote.’ Lakini hutambui ya kwamba wewe ni mnyonge, wa kuhurumiwa, maskini, kipofu, tena uliye uchi.
Because you say, I am wealthy, and have enriched myself, and have need of nothing; and do not know that you are wreatched and miserable, and poor, and blind, and naked.
18 Nakushauri ununue kutoka kwangu dhahabu iliyosafishwa kwa moto, ili upate kuwa tajiri, na mavazi meupe ili uyavae upate kuficha aibu ya uchi wako, na mafuta ya kupaka macho yako ili upate kuona.
I counsel you to buy of me gold tried in the fire, that you may be rich; and white apparel, that you may be clothed, and that the shame of your nakedness may not appear; and anoint your eyes with eye-salve, that you may see.
19 “Wale niwapendao, ninawakemea na kuwaadibisha. Hivyo uwe na bidii ukatubu.
As many as I love, I reprove and correct; therefore, be zealous, and reform.
20 Tazama! Nasimama mlangoni nabisha. Kama mtu yeyote akisikia sauti yangu na kufungua mlango, nitaingia ndani na kula pamoja naye, naye pamoja nami.
Behold, I stand at the door and knock: if any one hear my voice, and open the door, I will enter into his house, and will sup with him, and he with me.
21 “Yeye ashindaye nitampa haki ya kuketi pamoja nami kwenye kiti changu cha enzi, kama vile mimi nilivyoshinda na nikaketi pamoja na Baba yangu kwenye kiti chake cha enzi.
As for the conqueror, I will give him to sit down with me upon my throne; as I also have conquered, and sat down with my Father upon his throne.
22 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa.”
Whoever has an ear, let him hear what the Spirit says to the congregations.