< Ufunuo 21 >
1 Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya, kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza vimekwisha kupita, wala hapakuwepo na bahari tena.
Then [in the vision] I saw a new heaven and a new earth. The first heaven and the first earth had disappeared, and the oceans no longer existed.
2 Nikaona Mji Mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, ukiwa umeandaliwa kama bibi arusi aliyepambwa kwa ajili ya mumewe.
I saw [God’s] holy city, which is the new [city of] Jerusalem. It was coming down out of heaven from God. [The city] had been prepared [and decorated] {[God] had prepared [and decorated the city]} as [SIM] a bride is decorated {decorates herself} [beautifully in order to marry] her husband.
3 Nami nikasikia sauti kubwa kutoka kile kiti cha enzi ikisema, “Sasa makao ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atakaa pamoja nao. Yeye atakuwa Mungu wao nao watakuwa watu wake, naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.
I heard a loud voice that spoke from the throne [of God]. It said, “Listen to this! Now God will live with people. He will live [right in the midst of] them [DOU]! They will be his people. God himself will be with them, and he will be their God.
4 Atafuta kila chozi kutoka macho yao. Mauti haitakuwepo tena, wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu, kwa maana mambo ya kwanza yamekwisha kupita.”
[As a result], he will [cause them to no longer be sad. It will be as though he will] [MTY] wipe every tear from their eyes. [None of them] will ever again die or mourn or cry [DOU] or suffer pain, because the former things [that make us sad] will have disappeared.”
5 Naye yule aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi akasema, “Tazama, nayafanya mambo yote kuwa mapya!” Kisha akasema, “Andika haya, maana maneno haya ni ya kuaminika tena ni kweli.”
Then [God], who sits on the throne, said, “Listen to this! I am [now] making everything new!” He said [to me]: “Write these things [that I have told you], because you can trust [that I will certainly cause them to happen].”
6 Akaniambia, “Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Yeye aonaye kiu nitampa kunywa kutoka chemchemi ya maji ya uzima bila gharama yoyote.
He said to me, “I have finished [doing all the things I needed to do]. I am the one who began all things [MET] and the one who will cause all things to end [MET]. To everyone who is [spiritually] thirsty [MET], I will (freely give/give as a free gift) water from the spring [that causes people] to live [forever].
7 Yeye ashindaye atayarithi haya yote, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.
I will give this to every person who is victorious over [the evil powers] (OR, [over Satan]). I will be their God, and they will be my children.
8 Lakini waoga, wasioamini, wachafu, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, pamoja na waongo wote, mahali pao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.” (Limnē Pyr )
But those who are cowardly, those who do not believe [in me], those [who do] detestable things, those who are murderers, those who sin sexually, those who commit sorcery, those who worship idols, and every liar, will [all suffer] in the lake that burns with fire and sulfur. [Anyone who suffers in that lake] will be dying the second time.” (Limnē Pyr )
9 Mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na yale mabakuli saba ya hayo mapigo saba ya mwisho akaja akaniambia, “Njoo, nami nitakuonyesha bibi arusi, yaani, mke wa Mwana-Kondoo.”
One of the seven angels who had one of the seven bowls that had been full of [the wine/liquid causing] [MTY] the seven last plagues came and said to me, “Come [with me] and I will show you [the people who have permanently united with Christ, the one who is like a] lamb! They will be [like] [MET] a bride [for him].”
10 Naye akanichukua katika Roho hadi kwenye mlima mkubwa na mrefu, akanionyesha ule Mji Mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu.
Then, while [God’s] Spirit [controlled me], the angel took/carried me to the top of a very high mountain. He showed me [God’s] holy city, [the New] Jerusalem. It was coming down out of heaven from God.
11 Ulikuwa ukingʼaa kwa utukufu wa Mungu kama kito chenye thamani sana, kama yaspi, safi kama kioo.
It was shining with his glory. The city was shining like a very precious jasper stone [shines, and] it was clear like crystal.
12 Ulikuwa na ukuta mkubwa, mrefu wenye malango kumi na mawili, pakiwa na malaika kumi na wawili kwenye hayo malango. Kwenye malango hayo yaliandikwa majina ya yale makabila kumi na mawili ya Israeli.
[Around the city] was a very high wall. The wall had twelve gates. An angel was at each gate. The names of the twelve tribes of Israel were written {[God] had written the names of the twelve tribes of Israel} over the gates. [Each gate had the name of one tribe].
13 Kulikuwa na malango matatu upande wa mashariki, matatu upande wa kaskazini, matatu upande wa kusini na matatu upande wa magharibi.
Three gates were on the east [side], three gates were on the north [side], three gates were on the south [side], and three gates were on the west [side].
14 Ukuta wa huo mji ulikuwa na misingi kumi na miwili, na juu yake yaliandikwa majina ya wale mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo.
The wall of the city had twelve foundation [stones]. On each foundation [stone was] the name of one of the twelve apostles of [Jesus, the one who is like a] lamb.
15 Huyo malaika aliyesema nami alikuwa na ufito wa dhahabu wa kupimia huo mji, malango yake na kuta zake.
The angel who was speaking to me carried a golden measuring rod, in order to measure the city, its gates, and its wall.
16 Mji huo ulikuwa mraba, urefu wake ulikuwa sawa na upana wake. Akaupima huo mji kwa huo ufito akakuta una kama kilomita 2,200; urefu wake na upana wake na kwenda juu kwake vilikuwa sawa.
The city was square [in shape]; it was as long as it was wide. After the angel measured the city with his rod, [he reported that it was] (1,500 miles/2,400 kilometers) long, and that its height was the same as [its length and width].
17 Akaupima ukuta wake, ulikuwa na unene wa dhiraa 144 kwa kipimo cha kibinadamu ambacho huyo malaika alikuwa akikitumia.
He measured its wall [and reported that it was] ([216 ft./70 meters]) [thick] (OR, [high]). The angel used the measure that people [normally use].
18 Ukuta huo ulijengwa kwa yaspi hali mji wenyewe ulijengwa kwa dhahabu safi, ikingʼaa kama kioo.
The [city] wall was made of [something like the green stone that we call] jasper. The city [itself] was [made of something like] pure gold [that looked] like clear glass.
19 Misingi ya kuta za mji huo zilipambwa kwa kila aina ya kito cha thamani. Msingi wa kwanza ulikuwa wa yaspi, wa pili yakuti samawi, wa tatu kalkedoni, wa nne zumaridi,
The foundations of the wall of the city were beautifully made with [wonderful stones that are like] precious stones [on earth]. The first foundation [stone was a crystalline stone like] jasper, the second [foundation stone was a blue stone like] sapphire, the third [foundation stone was a green stone like] agate, the fourth [foundation stone was a green stone like] emerald,
20 wa tano sardoniki, wa sita akiki, wa saba krisolitho, wa nane zabarajadi, wa tisa yakuti manjano, wa kumi krisopraso, wa kumi na moja hiakintho, wa kumi na mbili amethisto.
the fifth [foundation stone was a brown and white layered stone like] sardonyx, the sixth [foundation stone was a red stone like] carnelian, the seventh [foundation stone was a yellow stone like] chrysolite, the eighth [foundation stone was a green stone like] beryl, the ninth [foundation stone was a yellow stone like] topaz, the tenth [foundation stone was a green stone like] chrysoprase, the eleventh [foundation stone was a blue stone like] hyacinth, and the twelfth [foundation stone was a purple stone like] amethyst.
21 Yale malango kumi na mbili yalikuwa ni lulu kumi na mbili, kila lango lilikuwa limetengenezwa kwa lulu moja. Barabara kuu ya mji huo ilikuwa ya dhahabu safi ingʼaayo kama kioo.
The twelve gates [of the city] were [something like huge] pearls. Each gate was like [it was] a single pearl. The [ground of] the main plaza of the city (OR, The streets of the city) [appeared to be] pure gold [that looked] like clear glass.
22 Sikuona Hekalu ndani ya huo mji kwa sababu Bwana Mungu Mwenyezi na Mwana-Kondoo ndio hekalu lake.
There was no temple in the city. The Lord God Almighty [himself], and the [one who is like a] lamb, are [there, so there was no need for] [MET] a temple.
23 Ule mji hauhitaji jua wala mwezi kuuangazia, kwa sababu utukufu wa Mungu ndio nuru yake na Mwana-Kondoo ndiye taa yake.
The city will not need the sun or the moon to light the city, because the glory of God will illuminate the city, and [Jesus, the one who is like a] lamb, will also be its light.
24 Mataifa yatatembea yakiangaziwa na nuru yake na wafalme wa duniani wataleta fahari yao ndani yake.
The people of [MTY] the nations will live with the light of the city [shining upon them]. And the kings of the earth will bring their wealth into the city [to honor God and the one who is like a lamb].
25 Malango yake hayatafungwa kamwe, kwa maana hakutakuwa na usiku humo.
The gates of the city will not be shut {No one will shut the gates of the city} [at the end of each day as they usually are shut], because there will be no night there.
26 Utukufu na heshima za mataifa zitaletwa humo.
The [people of the] world will also bring their wealth into the city to honor [God and the one who is like a lamb].
27 Lakini kitu kichafu hakitaingia humo kamwe, wala mtu yeyote atendaye mambo ya aibu au ya udanganyifu. Bali watakaoingia humo ni wale tu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.
No one who is morally impure, no one who does things [that God considers] detestable, and no one who tells lies, will ever enter that city. Only those people whose names are written in the book of the [one who is like a] lamb {whose [names] the [one who is like a] lamb has written in his book}, [the names] of people who have [eternal] life, will be there.