< Ufunuo 21 >
1 Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya, kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza vimekwisha kupita, wala hapakuwepo na bahari tena.
Then I saw a new heaven and a new earth, for the first heaven and the first earth had passed away, and the sea was no more.
2 Nikaona Mji Mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, ukiwa umeandaliwa kama bibi arusi aliyepambwa kwa ajili ya mumewe.
I also saw the holy city, new Jerusalem, coming down out of heaven from God, prepared like a bride adorned for her husband.
3 Nami nikasikia sauti kubwa kutoka kile kiti cha enzi ikisema, “Sasa makao ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atakaa pamoja nao. Yeye atakuwa Mungu wao nao watakuwa watu wake, naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.
And I heard a loud voice from heaven saying, “Behold, the tabernacle of God is with men. He will dwell with them, and they will be his people, and God himself will be with them.
4 Atafuta kila chozi kutoka macho yao. Mauti haitakuwepo tena, wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu, kwa maana mambo ya kwanza yamekwisha kupita.”
He will wipe away every tear from their eyes. Death will be no more, and there will no longer be mourning, crying, or pain, for the former things have passed away.”
5 Naye yule aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi akasema, “Tazama, nayafanya mambo yote kuwa mapya!” Kisha akasema, “Andika haya, maana maneno haya ni ya kuaminika tena ni kweli.”
Then he who sits on the throne said, “Behold, I am making all things new.” And he said to me, “Write this down, for these words are true and trustworthy.”
6 Akaniambia, “Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Yeye aonaye kiu nitampa kunywa kutoka chemchemi ya maji ya uzima bila gharama yoyote.
He also said to me, “I am the Alpha and the Omega, the beginning and the end. To him who thirsts I will freely give from the spring of the water of life.
7 Yeye ashindaye atayarithi haya yote, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.
He who overcomes will inherit these things; I will be his God, and he will be my son.
8 Lakini waoga, wasioamini, wachafu, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, pamoja na waongo wote, mahali pao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.” (Limnē Pyr )
But as for the cowardly, the faithless, the sinful, the detestable, the murderers, the fornicators, the sorcerers, the idolaters, and all liars, their portion is in the lake that burns with fire and sulfur, which is the second death.” (Limnē Pyr )
9 Mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na yale mabakuli saba ya hayo mapigo saba ya mwisho akaja akaniambia, “Njoo, nami nitakuonyesha bibi arusi, yaani, mke wa Mwana-Kondoo.”
Then one of the seven angels who had the seven bowls full of the seven final plagues came and said to me, “Come, I will show yoʋ the wife, the bride of the Lamb.”
10 Naye akanichukua katika Roho hadi kwenye mlima mkubwa na mrefu, akanionyesha ule Mji Mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu.
And he carried me away in the Spirit to a great and high mountain and showed me the great city, the holy Jerusalem, coming down out of heaven from God.
11 Ulikuwa ukingʼaa kwa utukufu wa Mungu kama kito chenye thamani sana, kama yaspi, safi kama kioo.
The city shone with the glory of God, and its radiance was like a very precious stone, like a jasper stone, clear as crystal.
12 Ulikuwa na ukuta mkubwa, mrefu wenye malango kumi na mawili, pakiwa na malaika kumi na wawili kwenye hayo malango. Kwenye malango hayo yaliandikwa majina ya yale makabila kumi na mawili ya Israeli.
It had a great, high wall with twelve gates. Twelve angels were at the gates, and on the gates were written the names of the twelve tribes of the sons of Israel.
13 Kulikuwa na malango matatu upande wa mashariki, matatu upande wa kaskazini, matatu upande wa kusini na matatu upande wa magharibi.
There were three gates on the east, three gates on the north, three gates on the south, and three gates on the west.
14 Ukuta wa huo mji ulikuwa na misingi kumi na miwili, na juu yake yaliandikwa majina ya wale mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo.
The wall of the city had twelve foundations, and on them were the twelve names of the twelve apostles of the Lamb.
15 Huyo malaika aliyesema nami alikuwa na ufito wa dhahabu wa kupimia huo mji, malango yake na kuta zake.
The angel who spoke to me had a golden measuring rod to measure the city and its gates.
16 Mji huo ulikuwa mraba, urefu wake ulikuwa sawa na upana wake. Akaupima huo mji kwa huo ufito akakuta una kama kilomita 2,200; urefu wake na upana wake na kwenda juu kwake vilikuwa sawa.
The city is laid out as a square; its length is the same as its width. The angel measured the city with the rod and found it to be twelve thousand stadia. (The length, width, and height were all equal, each measuring twelve thousand stadia.)
17 Akaupima ukuta wake, ulikuwa na unene wa dhiraa 144 kwa kipimo cha kibinadamu ambacho huyo malaika alikuwa akikitumia.
Its wall was one hundred forty-four cubits according to human measurement, which the angel was using.
18 Ukuta huo ulijengwa kwa yaspi hali mji wenyewe ulijengwa kwa dhahabu safi, ikingʼaa kama kioo.
The wall was made of jasper, while the city was pure gold, like clear glass.
19 Misingi ya kuta za mji huo zilipambwa kwa kila aina ya kito cha thamani. Msingi wa kwanza ulikuwa wa yaspi, wa pili yakuti samawi, wa tatu kalkedoni, wa nne zumaridi,
The foundations of the city wall were adorned with every kind of precious stone. The first foundation stone was jasper; the second, sapphire; the third, agate; the fourth, emerald;
20 wa tano sardoniki, wa sita akiki, wa saba krisolitho, wa nane zabarajadi, wa tisa yakuti manjano, wa kumi krisopraso, wa kumi na moja hiakintho, wa kumi na mbili amethisto.
the fifth, sardonyx; the sixth, carnelian; the seventh, chrysolite; the eighth, beryl; the ninth, topaz; the tenth, chrysoprase; the eleventh, jacinth; and the twelfth, amethyst.
21 Yale malango kumi na mbili yalikuwa ni lulu kumi na mbili, kila lango lilikuwa limetengenezwa kwa lulu moja. Barabara kuu ya mji huo ilikuwa ya dhahabu safi ingʼaayo kama kioo.
The twelve gates were twelve pearls, each one of the gates was made of a single pearl, and the street of the city was pure gold, like transparent glass.
22 Sikuona Hekalu ndani ya huo mji kwa sababu Bwana Mungu Mwenyezi na Mwana-Kondoo ndio hekalu lake.
I did not see a temple in the city, for the Lord God Almighty is its temple, and so is the Lamb.
23 Ule mji hauhitaji jua wala mwezi kuuangazia, kwa sababu utukufu wa Mungu ndio nuru yake na Mwana-Kondoo ndiye taa yake.
The city has no need of sun or moon to shine upon it, for the glory of God gives it light, and its lamp is the Lamb.
24 Mataifa yatatembea yakiangaziwa na nuru yake na wafalme wa duniani wataleta fahari yao ndani yake.
The nations will walk by its light, and the kings of the earth will bring the glory and honor of the nations into the city to present to God.
25 Malango yake hayatafungwa kamwe, kwa maana hakutakuwa na usiku humo.
Its gates will never be shut at the end of the day, for there will be no night there.
26 Utukufu na heshima za mataifa zitaletwa humo.
They will bring the glory and honor of the nations into the city.
27 Lakini kitu kichafu hakitaingia humo kamwe, wala mtu yeyote atendaye mambo ya aibu au ya udanganyifu. Bali watakaoingia humo ni wale tu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.
But no unclean thing and no one who causes an abomination or a lie will ever enter it, but only those whose names are written in the Lamb's book of life.