< Ufunuo 21 >
1 Kisha nikaona mbingu mpya na nchi mpya, kwa maana mbingu za kwanza na nchi ya kwanza vimekwisha kupita, wala hapakuwepo na bahari tena.
And I saw a new heaven and a new earth, for the first heaven and the first earth passed away, and the sea is no more;
2 Nikaona Mji Mtakatifu, Yerusalemu mpya, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu, ukiwa umeandaliwa kama bibi arusi aliyepambwa kwa ajili ya mumewe.
and I saw the holy city, New Jerusalem, coming down from God out of Heaven, made ready as a bride adorned for her husband;
3 Nami nikasikia sauti kubwa kutoka kile kiti cha enzi ikisema, “Sasa makao ya Mungu ni pamoja na wanadamu, naye atakaa pamoja nao. Yeye atakuwa Mungu wao nao watakuwa watu wake, naye Mungu mwenyewe atakuwa pamoja nao.
and I heard a great voice out of Heaven, saying, “Behold, the dwelling place of God [is] with men, and He will dwell with them, and they will be His peoples, and God Himself will be with them [as] their God,
4 Atafuta kila chozi kutoka macho yao. Mauti haitakuwepo tena, wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu, kwa maana mambo ya kwanza yamekwisha kupita.”
and God will wipe away every tear from their eyes, and there will be no more death, nor sorrow, nor crying, nor will there be anymore pain, because the first things passed away.”
5 Naye yule aliyeketi juu ya kile kiti cha enzi akasema, “Tazama, nayafanya mambo yote kuwa mapya!” Kisha akasema, “Andika haya, maana maneno haya ni ya kuaminika tena ni kweli.”
And He who is sitting on the throne said, “Behold, I make all things new”; and He says to me, “Write, because these words are true and steadfast”;
6 Akaniambia, “Imekwisha kuwa. Mimi ni Alfa na Omega, Mwanzo na Mwisho. Yeye aonaye kiu nitampa kunywa kutoka chemchemi ya maji ya uzima bila gharama yoyote.
and He said to me, “It is done! I am the Alpha and the Omega, the Beginning and the End. To him who is thirsting, I will give of the fountain of the water of life freely.
7 Yeye ashindaye atayarithi haya yote, nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa mwanangu.
The [one] who is overcoming will inherit all things, and I will be his God, and he will be My son.
8 Lakini waoga, wasioamini, wachafu, wauaji, wazinzi, wachawi, waabudu sanamu, pamoja na waongo wote, mahali pao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.” (Limnē Pyr )
But to fearful, and unsteadfast, and abominable, and murderers, and whoremongers, and sorcerers, and idolaters, and all the liars, their part [is] in the lake that is burning with fire and brimstone, which is the second death.” (Limnē Pyr )
9 Mmoja wa wale malaika saba waliokuwa na yale mabakuli saba ya hayo mapigo saba ya mwisho akaja akaniambia, “Njoo, nami nitakuonyesha bibi arusi, yaani, mke wa Mwana-Kondoo.”
And one of the seven messengers, having the seven bowls that are full of the seven last plagues, came and spoke with me, saying, “Come, I will show you the bride, the wife of the Lamb,”
10 Naye akanichukua katika Roho hadi kwenye mlima mkubwa na mrefu, akanionyesha ule Mji Mtakatifu, Yerusalemu, ukishuka kutoka mbinguni kwa Mungu.
and he carried me away in the Spirit to a mountain great and high, and showed me the great city, the holy Jerusalem, coming down out of Heaven from God,
11 Ulikuwa ukingʼaa kwa utukufu wa Mungu kama kito chenye thamani sana, kama yaspi, safi kama kioo.
having the glory of God, and her light—like a most precious stone, as a jasper stone clear as crystal,
12 Ulikuwa na ukuta mkubwa, mrefu wenye malango kumi na mawili, pakiwa na malaika kumi na wawili kwenye hayo malango. Kwenye malango hayo yaliandikwa majina ya yale makabila kumi na mawili ya Israeli.
also having a great and high wall, having twelve gates, and at the gates twelve messengers, and names written thereon, which are [those] of the twelve tribes of the sons of Israel—
13 Kulikuwa na malango matatu upande wa mashariki, matatu upande wa kaskazini, matatu upande wa kusini na matatu upande wa magharibi.
at the east three gates, at the north three gates, at the south three gates, at the west three gates;
14 Ukuta wa huo mji ulikuwa na misingi kumi na miwili, na juu yake yaliandikwa majina ya wale mitume kumi na wawili wa Mwana-Kondoo.
and the wall of the city had twelve foundations, and on them names of the twelve apostles of the Lamb.
15 Huyo malaika aliyesema nami alikuwa na ufito wa dhahabu wa kupimia huo mji, malango yake na kuta zake.
And he who is speaking with me had a golden reed, that he may measure the city, and its gates, and its wall;
16 Mji huo ulikuwa mraba, urefu wake ulikuwa sawa na upana wake. Akaupima huo mji kwa huo ufito akakuta una kama kilomita 2,200; urefu wake na upana wake na kwenda juu kwake vilikuwa sawa.
and the city lies square, and the length of it is as great as the breadth; and he measured the city with the reed—twelve thousand stadia; the length, and the breadth, and the height of it are equal.
17 Akaupima ukuta wake, ulikuwa na unene wa dhiraa 144 kwa kipimo cha kibinadamu ambacho huyo malaika alikuwa akikitumia.
And he measured its wall—one hundred forty-four cubits, the measure of a man, that is, of the messenger;
18 Ukuta huo ulijengwa kwa yaspi hali mji wenyewe ulijengwa kwa dhahabu safi, ikingʼaa kama kioo.
and the building of its wall was jasper, and the city [is] pure gold—like to pure glass.
19 Misingi ya kuta za mji huo zilipambwa kwa kila aina ya kito cha thamani. Msingi wa kwanza ulikuwa wa yaspi, wa pili yakuti samawi, wa tatu kalkedoni, wa nne zumaridi,
And the foundations of the wall of the city have been adorned with every precious stone: the first foundation jasper, the second sapphire, the third chalcedony, the fourth emerald,
20 wa tano sardoniki, wa sita akiki, wa saba krisolitho, wa nane zabarajadi, wa tisa yakuti manjano, wa kumi krisopraso, wa kumi na moja hiakintho, wa kumi na mbili amethisto.
the fifth sardonyx, the sixth sardius, the seventh chrysolite, the eighth beryl, the ninth topaz, the tenth chrysoprase, the eleventh jacinth, the twelfth amethyst.
21 Yale malango kumi na mbili yalikuwa ni lulu kumi na mbili, kila lango lilikuwa limetengenezwa kwa lulu moja. Barabara kuu ya mji huo ilikuwa ya dhahabu safi ingʼaayo kama kioo.
And the twelve gates [are] twelve pearls, each one of the gates respectively was of one pearl; and the street of the city [is] pure gold—as transparent glass.
22 Sikuona Hekalu ndani ya huo mji kwa sababu Bwana Mungu Mwenyezi na Mwana-Kondoo ndio hekalu lake.
And I did not see a temple in it, for the LORD God, the Almighty, and the Lamb, are its temple.
23 Ule mji hauhitaji jua wala mwezi kuuangazia, kwa sababu utukufu wa Mungu ndio nuru yake na Mwana-Kondoo ndiye taa yake.
And the city has no need of the sun, nor of the moon, that they may shine in it; for the glory of God lightens it, and the lamp of it—the Lamb;
24 Mataifa yatatembea yakiangaziwa na nuru yake na wafalme wa duniani wataleta fahari yao ndani yake.
and the nations will walk by its light, and the kings of the earth bring their glory and honor into it,
25 Malango yake hayatafungwa kamwe, kwa maana hakutakuwa na usiku humo.
and its gates will never be shut by day, for night will not be there;
26 Utukufu na heshima za mataifa zitaletwa humo.
and they will bring the glory and the honor of the nations into it;
27 Lakini kitu kichafu hakitaingia humo kamwe, wala mtu yeyote atendaye mambo ya aibu au ya udanganyifu. Bali watakaoingia humo ni wale tu ambao majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo.
and there may never enter into it anything defiling and doing abomination, and a lie, if not those written in the Lamb’s Scroll of Life.