< Ufunuo 20 >
1 Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, akiwa ameshika ufunguo wa lile Shimo na mnyororo mkubwa mkononi mwake. (Abyssos )
I saw an angel coming down from heaven. He had the key to the deep dark pit, and he was carrying a large chain in his hand. (Abyssos )
2 Akalishika lile joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ndiye ibilisi au Shetani, naye akamfunga kwa muda wa miaka 1,000.
He seized the dragon. That dragon is the ancient serpent, the devil, that is, Satan. The angel bound him with the chain. That chain could not be loosed {[No one could loose] that chain} for 1,000 years.
3 Akamtupa katika lile Shimo, akamfunga humo na kulitia lakiri, ili kumzuia asiendelee kudanganya mataifa mpaka hiyo miaka 1,000 itimie. Baada ya hayo lazima afunguliwe kwa muda mfupi. (Abyssos )
The angel threw him into the deep dark pit. He shut [the door of the pit], locked it, and sealed it [to prevent anyone from opening it]. He did that in order that Satan might no longer deceive [the people of the] nations [MTY], until those 1,000 years are ended. After that [time], Satan must be released {[God/God’s angel] must release Satan} for a short time [in order that he can do what God has planned]. (Abyssos )
4 Kisha nikaona viti vya enzi vilivyokuwa vimekaliwa na hao waliopewa mamlaka ya kuhukumu, na nikaona roho za wale waliokatwa vichwa kwa sababu ya ushuhuda wa Yesu na kwa sababu ya neno la Mungu. Hawakuwa wamemsujudu huyo mnyama wala sanamu yake wala hawakupokea ile chapa yake kwenye vipaji vya nyuso zao au kwenye mikono yao. Wakawa hai na kutawala pamoja na Kristo miaka 1,000.
I saw thrones on which people were sitting. [They were given] {[God] gave those people} [authority] to judge [other people]. I also saw the souls [of people] whose heads had been {whose heads [others] had} cut off because of [their telling people about] Jesus and declaring God’s message. They were people who refused to worship the beast or its image, and who did not allow [the beast’s agents] to put the beast’s mark on them, either on their foreheads or on their hands. They became alive again, and they ruled with Christ [during those] 1,000 years.
5 (Wafu waliosalia hawakufufuka mpaka ilipotimia hiyo miaka 1,000.) Huu ndio ufufuo wa kwanza.
They were the ones who lived again the first time [that God caused dead people] to live again. The rest of [the believers who] had died did not live again until after those 1,000 years.
6 Waliobarikiwa na walio watakatifu ni wale walio na sehemu katika ufufuo wa kwanza. Hao mauti ya pili haina nguvu juu yao, bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala pamoja naye kwa muda wa miaka 1,000.
([God] will be pleased with/[How] happy will be) those who live again that first time. God will [consider] them holy. They will not die [PRS] a second time. Instead, they will be priests [who serve] God and Christ, and they will rule with [Christ] during those 1,000 years.
7 Hiyo miaka 1,000 itakapotimia, Shetani atafunguliwa kutoka kifungoni mwake,
When the 1,000 years are ended, Satan will be released {[God’s angel] will release Satan} from [the deep pit] in which he was imprisoned.
8 naye atatoka ili kuyadanganya mataifa yaliyopo katika pembe nne za dunia, yaani, Gogu na Magogu apate kuwakusanya tayari kwa vita. Idadi yao ni kama mchanga ulioko pwani.
He will go out to deceive [rebellious] people in nations [IDM] all over the earth. [These are the nations that the prophet Ezekiel called] Gog and Magog. Satan will gather them to fight against [God’s people]. There will be [so many of them fighting against God’s people that no one will be able to count them] [SIM], just like [no one can count the grains of] sand on the ocean shore.
9 Nao walitembea katika eneo lote la dunia, wakaizunguka kambi ya watakatifu na ule mji unaopendwa. Lakini moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza.
They will march over the whole earth and surround the camp of God’s people [in Jerusalem], the city that [God] loves. Then [God will send] fire down from heaven, and it will burn them up.
10 Naye ibilisi aliyewadanganya akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti walikokuwa wametupwa yule mnyama na yule nabii wa uongo. Watateswa humo usiku na mchana, milele na milele. (aiōn , Limnē Pyr )
The devil, who had deceived those people, will be thrown {[God’s angel] will throw the devil, who had deceived those people} into the lake of burning sulfur. [This is the same lake] into which both the beast and the false prophet had been [thrown] {[he] had [thrown] both the beast and the false prophet}. [As a result], they will continually suffer severely forever. (aiōn , Limnē Pyr )
11 Kisha nikaona kiti kikubwa cheupe cha enzi pamoja na yeye aliyeketi juu yake. Dunia na mbingu zikaukimbia uso wake wala mahali pao hapakuonekana.
Then I saw a huge white throne on which [God] was sitting. He [was so awesome that] the earth and the sky disappeared from his presence completely; they were completely destroyed {[God] completely destroyed them}.
12 Nami nikawaona wafu wakubwa na wadogo, wakiwa wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi na vitabu vikafunguliwa. Pia kitabu kingine kikafunguliwa ambacho ni kitabu cha uzima. Hao wafu wakahukumiwa sawasawa na matendo yao kama yalivyoandikwa ndani ya hivyo vitabu.
I saw that the people who had died [but now lived again] were standing in front of the throne. [They included people of] every social status! The books [in which God records what people do] were opened {[God/God’s angel] opened the books [in which God records what people do]}. Another book was opened {[He] opened another book}, which is [called the Book] of Life, [in which God has written the names of people who have eternal life]. [God] judged the people who had died [and now lived again] according to what they had done, just like [he] had recorded it in the books.
13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake, nayo mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Kila mtu akahukumiwa kulingana na yale aliyoyatenda. (Hadēs )
[The people whose bodies were buried in the] sea [became alive again in order to stand before God’s throne]. Everyone who had been buried on the land (OR, Every person who was waiting in the place where dead people stay) [became alive again, in order to stand before the throne]. [God] judged each one of them according to what each one had done. (Hadēs )
14 Kisha mauti na Kuzimu zikatupwa katika ziwa la moto. Hii ndio mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. (Hadēs , Limnē Pyr )
All the unbelievers [PRS, MTY] —those who had been in the place where they waited after they died— [were thrown into the burning lake]. The burning lake is [the place in which people] die the second time. (Hadēs , Limnē Pyr )
15 Iwapo mtu jina lake halikuonekana katika kile kitabu cha uzima, alitupwa ndani ya lile ziwa la moto. (Limnē Pyr )
The people whose [names] [MTY] are not in the book, the one [where God] has written [the names of people who] have [eternal] life, [were also thrown] {([God/God’s angel]) threw them also} [into the lake] of fire. (Limnē Pyr )