< Ufunuo 20 >
1 Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, akiwa ameshika ufunguo wa lile Shimo na mnyororo mkubwa mkononi mwake. (Abyssos )
Og jeg saa en Engel stige ned fra Himmelen, han havde Afgrundens Nøgle og en stor Lænke i sin Haand. (Abyssos )
2 Akalishika lile joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ndiye ibilisi au Shetani, naye akamfunga kwa muda wa miaka 1,000.
Og han greb Dragen, den gamle Slange, som er Djævelen og Satan, og bandt ham for tusinde Aar
3 Akamtupa katika lile Shimo, akamfunga humo na kulitia lakiri, ili kumzuia asiendelee kudanganya mataifa mpaka hiyo miaka 1,000 itimie. Baada ya hayo lazima afunguliwe kwa muda mfupi. (Abyssos )
og kastede ham i Afgrunden og lukkede og forseglede over ham, for at han ikke mere skulde forføre Folkeslagene, førend de tusinde Aar vare til Ende; derefter skal han løses en lille Tid. (Abyssos )
4 Kisha nikaona viti vya enzi vilivyokuwa vimekaliwa na hao waliopewa mamlaka ya kuhukumu, na nikaona roho za wale waliokatwa vichwa kwa sababu ya ushuhuda wa Yesu na kwa sababu ya neno la Mungu. Hawakuwa wamemsujudu huyo mnyama wala sanamu yake wala hawakupokea ile chapa yake kwenye vipaji vya nyuso zao au kwenye mikono yao. Wakawa hai na kutawala pamoja na Kristo miaka 1,000.
Og jeg saa Troner, og de satte sig paa dem, og Dommermagt blev given dem; og jeg saa deres Sjæle, som vare halshuggede for Jesu Vidnesbyrds og for Guds Ords Skyld, og dem, som ikke havde tilbedet Dyret eller dets Billede og ikke havde taget Mærket paa deres Pande og paa deres Haand; og de bleve levende og bleve Konger med Kristus i tusinde Aar.
5 (Wafu waliosalia hawakufufuka mpaka ilipotimia hiyo miaka 1,000.) Huu ndio ufufuo wa kwanza.
De øvrige af de døde bleve ikke levende, førend de tusinde Aar vare til Ende. Dette er den første Opstandelse.
6 Waliobarikiwa na walio watakatifu ni wale walio na sehemu katika ufufuo wa kwanza. Hao mauti ya pili haina nguvu juu yao, bali watakuwa makuhani wa Mungu na wa Kristo, nao watatawala pamoja naye kwa muda wa miaka 1,000.
Salig og hellig er den, som har Del i den første Opstandelse; over disse har den anden Død ikke Magt, men de skulle være Guds og Kristi Præster og skulle være Konger med ham i de tusinde Aar.
7 Hiyo miaka 1,000 itakapotimia, Shetani atafunguliwa kutoka kifungoni mwake,
Og naar de tusinde Aar ere til Ende, skal Satan løses af sit Fængsel.
8 naye atatoka ili kuyadanganya mataifa yaliyopo katika pembe nne za dunia, yaani, Gogu na Magogu apate kuwakusanya tayari kwa vita. Idadi yao ni kama mchanga ulioko pwani.
Og han skal gaa ud for at forføre Folkeslagene ved Jordens fire Hjørner, Gog og Magog, for at samle dem til Krig; deres Tal er som Havets Sand.
9 Nao walitembea katika eneo lote la dunia, wakaizunguka kambi ya watakatifu na ule mji unaopendwa. Lakini moto ukashuka kutoka mbinguni na kuwateketeza.
Og de droge frem over Jordens Flade og omringede de helliges Lejr og den elskede Stad. Og Ild faldt ned fra Himmelen fra Gud og fortærede dem.
10 Naye ibilisi aliyewadanganya akatupwa katika ziwa la moto na kiberiti walikokuwa wametupwa yule mnyama na yule nabii wa uongo. Watateswa humo usiku na mchana, milele na milele. (aiōn , Limnē Pyr )
Og Djævelen, som forførte dem, blev kastet i Ild- og Svovlsøen, hvor ogsaa Dyret og den falske Profet var; og de skulle pines Dag og Nat i Evighedernes Evigheder. (aiōn , Limnē Pyr )
11 Kisha nikaona kiti kikubwa cheupe cha enzi pamoja na yeye aliyeketi juu yake. Dunia na mbingu zikaukimbia uso wake wala mahali pao hapakuonekana.
Og jeg saa en stor, hvid Trone og ham, som sad derpaa; for hans Aasyn flyede Jorden og Himmelen, og der blev ikke fundet Sted for dem.
12 Nami nikawaona wafu wakubwa na wadogo, wakiwa wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi na vitabu vikafunguliwa. Pia kitabu kingine kikafunguliwa ambacho ni kitabu cha uzima. Hao wafu wakahukumiwa sawasawa na matendo yao kama yalivyoandikwa ndani ya hivyo vitabu.
Og jeg saa de døde, de store og de smaa, staaende for Tronen, og Bøger bleve aabnede; og en anden Bog blev aabnet, som er Livets Bog; og de døde bleve dømte efter det, som var skrevet i Bøgerne, efter deres Gerninger.
13 Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake, nayo mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Kila mtu akahukumiwa kulingana na yale aliyoyatenda. (Hadēs )
Og Havet afgav de døde, som vare i det; og Døden og Dødsriget afgave de døde, som vare i dem, og de bleve dømte, hver efter sine Gerninger. (Hadēs )
14 Kisha mauti na Kuzimu zikatupwa katika ziwa la moto. Hii ndio mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. (Hadēs , Limnē Pyr )
Og Døden og Dødsriget bleve kastede i Ildsøen. Dette er den anden Død, Ildsøen. (Hadēs , Limnē Pyr )
15 Iwapo mtu jina lake halikuonekana katika kile kitabu cha uzima, alitupwa ndani ya lile ziwa la moto. (Limnē Pyr )
Og dersom nogen ikke fandtes skreven i Livets Bog, blev han kastet i Ildsøen. (Limnē Pyr )