< Ufunuo 2 >

1 “Kwa malaika wa kanisa lililoko Efeso andika: “Haya ndiyo maneno ya yule aliyezishika zile nyota saba katika mkono wake wa kuume na ambaye hutembea kati ya vile vinara saba vya taa vya dhahabu.
To the angel of the church at Ephesus write, These things saith He that holdeth the seven stars in his right hand, who walketh in the midst of the seven golden candlesticks;
2 Nayajua matendo yako, bidii yako na saburi yako. Najua kuwa huwezi kuvumiliana na watu waovu na ya kwamba umewajaribu wale wanaojifanya kuwa mitume na kumbe sio, nawe umewatambua kuwa ni waongo.
I know thy works, and thy labor, and thy patience, and that thou canst not bear those that are evil: and thou hast tried those who say they are apostles, and are not, and hast found them liars; and hast borne trouble, and hast patience;
3 Umevumilia na kustahimili taabu kwa ajili ya Jina langu, wala hukuchoka.
and for my name's sake thou hast laboured, and hast not fainted.
4 “Lakini nina neno dhidi yako: Umeuacha upendo wako wa kwanza.
Yet I have somewhat against thee; for thou hast left thy first love.
5 Kumbuka basi ni wapi ulikoangukia! Tubu na ukafanye matendo yale ya kwanza. Kama usipotubu, nitakuja kwako na kukiondoa kinara chako cha taa kutoka mahali pake.
Remember therefore from whence thou art fallen, and repent, and do the first works: else I will come unto thee quickly, and will remove thy candlestick out of its place, if thou repent not.
6 Lakini una jambo hili kwa upande wako: Unayachukia matendo ya Wanikolai, ambayo nami pia nayachukia.
But this thou hast, that thou hatest the works of the Nicolaitans, which I also hate.
7 “Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa haki ya kula matunda toka kwa mti wa uzima, ambao uko katika paradisoya Mungu.
Let him, that hath an ear, hear what the Spirit saith unto the churches. To him that overcometh will I give to eat of the tree of life, which is in the midst of the paradise of God.
8 “Kwa malaika wa kanisa lililoko Smirna andika: “Haya ndiyo maneno yake yeye aliye wa Kwanza na wa Mwisho, aliyekufa kisha akafufuka.
And to the angel of the church in Smyrna write, These things saith the First and the Last, who was dead and is alive;
9 Naijua dhiki yako na umaskini wako, lakini wewe ni tajiri! Nayajua masingizio ya wale wasemao kuwa ni Wayahudi lakini sio, bali wao ni sinagogi la Shetani.
I know thy works and affliction and poverty (but thou art rich) and I know the blasphemy of those that say they are Jews, and are not, but are the synagogue of Satan.
10 Usiogope mateso yatakayokupata. Nakuambia ibilisi atawatia baadhi yenu gerezani ili kuwajaribu, nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.
Fear none of the things which thou wilt suffer: behold the devil shall cast some of you into prison, that ye may be tried; and ye shall suffer affliction ten days. Be thou faithful unto death, and I will give thee a crown of life.
11 “Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye hatadhuriwa kamwe na mauti ya pili.
Let him, that hath an ear, hear what the Spirit saith unto the churches. He, that overcometh, shall not be hurt by the second death.
12 “Kwa malaika wa Kanisa lililoko Pergamo andika: “Haya ndiyo maneno yake yeye aliye na upanga mkali wenye makali kuwili.
And to the angel of the church in Pergamos write, These things saith He, who hath the sharp two-edged sword;
13 Ninajua unakoishi, ni kule ambako Shetani ana kiti chake cha enzi. Lakini umelishika Jina langu. Wala hukuikana imani yako kwangu hata katika siku za shahidi wangu mwaminifu Antipa, ambaye aliuawa katika mji mkuu wenu, ambako ndiko anakoishi Shetani.
I know thy works, and where thou dwellest, even where Satan's seat is: and yet thou holdest fast my name, and hast not denied my faith, even in those days wherein Antipas was my faithful martyr; who was slain among you, where Satan dwelleth.
14 “Hata hivyo, nina mambo machache dhidi yako: Unao watu wafuatao mafundisho ya Balaamu, yule aliyemfundisha Balaki kuwashawishi Waisraeli watende dhambi kwa kula vitu vilivyotolewa kafara kwa sanamu na kufanya uasherati.
But I have a few things against thee; for thou hast there those that hold the doctrine of Balaam, who taught Balak to cast a stumbling-block before the children of Israel, to eat things sacrificed to idols, and to commit fornication.
15 Vivyo hivyo unao wale wayashikayo mafundisho ya Wanikolai.
So thou hast also them that hold the like doctrine of the Nicolaitans, which I hate.
16 Basi tubu! Ama sivyo, nitakuja kwako upesi na kupigana na watu hao kwa upanga wa kinywa changu.
Repent therefore---if not, I will come unto thee quickly, and will fight against them with the sword that goeth out of my mouth.
17 “Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa. Nitampa pia jiwe jeupe ambalo juu yake limeandikwa jina jipya asilolijua mtu, isipokuwa yule anayelipokea.
Let him, that hath an ear, hear what the Spirit saith unto the churches. To him that overcometh will I give to eat of the hidden manna: and I will give him a white stone, and on the stone a new name written, which no one knoweth, but He that receiveth it.
18 “Kwa malaika wa kanisa lililoko Thiatira andika: “Haya ndiyo maneno ya Mwana wa Mungu, ambaye macho yake ni kama mwali wa moto na ambaye miguu yake ni kama shaba iliyosuguliwa sana.
And to the angel of the church in Thyatira write, These things saith the Son of God, who hath eyes like a flame of fire, and his feet like fine brass; I know thy works,
19 Nayajua matendo yako, upendo wako na imani yako, huduma na saburi yako na kwamba matendo yako ya sasa yamezidi yale ya kwanza.
and thy love, and thy service, and thy faith, and thy patience, and that thy last works are more than the first.
20 “Hata hivyo, nina neno dhidi yako: Unamvumilia yule mwanamke Yezebeli ambaye anajiita nabii, lakini anawafundisha na kuwapotosha watumishi wangu ili wafanye uasherati na kula vyakula vilivyotolewa kafara kwa sanamu.
But I have a few things against thee; because thou sufferest the woman Jezabel, who saith that she is a prophetess, to teach and to seduce my servants to commit fornication and to eat things sacrificed to idols.
21 Nimempa muda ili atubu kwa ajili ya uasherati wake, lakini hataki.
And I gave her time to repent of her fornication, and she repented not.
22 Kwa hiyo nitamtupa kwenye kitanda cha mateso, na nitawafanya hao wanaozini naye kupata mateso makali wasipotubia njia zake.
Behold I will cast her into a bed, and those that commit whoredom with her, into great tribulation, except they repent of their deeds:
23 Nami nitawaua watoto wake. Nayo makanisa yote yatajua kwamba Mimi ndiye nichunguzaye mioyo na nia, na kwamba nitamlipa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake.
and I will cut off her children by death; and all the churches shall know, that I am He who searcheth the reins and hearts, and I will give unto every one of you according to your works.
24 Basi nawaambia ninyi wengine mlioko Thiatira, ninyi ambao hamyafuati mafundisho ya Yezebeli, wala hamkujifunza hayo yanayoitwa mambo ya ndani sana ya Shetani (sitaweka mzigo mwingine wowote juu yenu):
But to you I say, to the rest in Thyatira, As many as do not hold this doctrine, and who are unacquainted with the depths of Satan, as they speak, I will lay on you no other burden:
25 Lakini shikeni sana mlicho nacho, mpaka nitakapokuja.
but what ye have hold fast till I come.
26 “Atakayeshinda na kutenda mapenzi yangu mpaka mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa:
And to him that overcometh, and keepeth my works unto the end, will I give power over the nations:
27 “‘Atawatawala kwa fimbo ya chuma, atawavunja vipande vipande kama chombo cha udongo’: kama vile mimi nilivyopokea mamlaka kutoka kwa Baba yangu.
and he shall rule them with a rod of iron, as the vessels of a potter shall they be broken in pieces; as I also have received of my Father;
28 Nami nitampa pia ile nyota ya asubuhi.
and I will give him the morning-star.
29 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa.
Let him, that hath an ear, hear what the Spirit saith unto the churches.

< Ufunuo 2 >