< Ufunuo 2 >
1 “Kwa malaika wa kanisa lililoko Efeso andika: “Haya ndiyo maneno ya yule aliyezishika zile nyota saba katika mkono wake wa kuume na ambaye hutembea kati ya vile vinara saba vya taa vya dhahabu.
By the messenger of the congregation in Ephesus, write: These things, says he who holds the seven stars in his right hand, who walks in the midst of the seven golden lamps:
2 Nayajua matendo yako, bidii yako na saburi yako. Najua kuwa huwezi kuvumiliana na watu waovu na ya kwamba umewajaribu wale wanaojifanya kuwa mitume na kumbe sio, nawe umewatambua kuwa ni waongo.
I know your works, and your labor, and your pateince; and that you can not bear those who are evil: and you have tried those who say they are Apostles, and are not, and have found them liars;
3 Umevumilia na kustahimili taabu kwa ajili ya Jina langu, wala hukuchoka.
and you have patience; and have borne for my name's sake, and have not fainted.
4 “Lakini nina neno dhidi yako: Umeuacha upendo wako wa kwanza.
Nevertheless, I have against you that you have lost your first love.
5 Kumbuka basi ni wapi ulikoangukia! Tubu na ukafanye matendo yale ya kwanza. Kama usipotubu, nitakuja kwako na kukiondoa kinara chako cha taa kutoka mahali pake.
Remember, therefore, from what you are fallen, and reform, and do the first works, otherwise I will come to you quickly, and take away your lamp out of its place, unless you reform.
6 Lakini una jambo hili kwa upande wako: Unayachukia matendo ya Wanikolai, ambayo nami pia nayachukia.
Yet you have this, that you hate the works of the Nicolaitans, which I also hate.
7 “Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa haki ya kula matunda toka kwa mti wa uzima, ambao uko katika paradisoya Mungu.
Whoever has an ear, let him hear what the Spirit says to the congregations. To him who conquers, I will give to eat of the tree of life, which is in the midst of the paradise of God.
8 “Kwa malaika wa kanisa lililoko Smirna andika: “Haya ndiyo maneno yake yeye aliye wa Kwanza na wa Mwisho, aliyekufa kisha akafufuka.
And by the messenger of the congregation in Symrna, write: These things, says the First and the Last, who was dead, and is alive:
9 Naijua dhiki yako na umaskini wako, lakini wewe ni tajiri! Nayajua masingizio ya wale wasemao kuwa ni Wayahudi lakini sio, bali wao ni sinagogi la Shetani.
I know your works, and tribulation, and poverty, (but you are rich, ) and I know the slander of those who say they are Jews, and are not; but are the assembly of Satan.
10 Usiogope mateso yatakayokupata. Nakuambia ibilisi atawatia baadhi yenu gerezani ili kuwajaribu, nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.
Fear none of the things which you shall suffer; behold, the devil will cast some of you into prison, that you may be tried; and you shall have tribulation ten days: be you faithful until death, and I will give you a crown of life.
11 “Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye hatadhuriwa kamwe na mauti ya pili.
Whoever has an ear, let him hear what the Spirit says to the congregations. The conqueror shall not be injured by the second death.
12 “Kwa malaika wa Kanisa lililoko Pergamo andika: “Haya ndiyo maneno yake yeye aliye na upanga mkali wenye makali kuwili.
And by the messenger of the congregation which is in Pergamos, write: These things says he who has the sharp two-edged sword:
13 Ninajua unakoishi, ni kule ambako Shetani ana kiti chake cha enzi. Lakini umelishika Jina langu. Wala hukuikana imani yako kwangu hata katika siku za shahidi wangu mwaminifu Antipa, ambaye aliuawa katika mji mkuu wenu, ambako ndiko anakoishi Shetani.
I know your works, and where you dwell; even where the throne of Satan is: and you hold fast my name, and have not denied my faith, even in those days in which Antipas was my faithful witness, who was slain among you, where Satan dwells.
14 “Hata hivyo, nina mambo machache dhidi yako: Unao watu wafuatao mafundisho ya Balaamu, yule aliyemfundisha Balaki kuwashawishi Waisraeli watende dhambi kwa kula vitu vilivyotolewa kafara kwa sanamu na kufanya uasherati.
Nevertheless, I have a few things against you, that you have there, them who hold the doctrine of Balaam, who taught Balak to cast a stumbling block before the children of Israel, to eat things sacrificed to idols, and to commit fornication.
15 Vivyo hivyo unao wale wayashikayo mafundisho ya Wanikolai.
You, in like manner, have those that hold the doctrine of the Nicolaitans, which I hate.
16 Basi tubu! Ama sivyo, nitakuja kwako upesi na kupigana na watu hao kwa upanga wa kinywa changu.
Reform, or otherwise, I will come to you quickly, and I will fight against them with the sword of my mouth.
17 “Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa. Nitampa pia jiwe jeupe ambalo juu yake limeandikwa jina jipya asilolijua mtu, isipokuwa yule anayelipokea.
Whoever has an ear, let him hear what the Spirit says to the congregations: To the conqueror I will give of the hidden mann; and I will give him a white stone, and in the stone a new name written, which no man knows except he who receives it.
18 “Kwa malaika wa kanisa lililoko Thiatira andika: “Haya ndiyo maneno ya Mwana wa Mungu, ambaye macho yake ni kama mwali wa moto na ambaye miguu yake ni kama shaba iliyosuguliwa sana.
And by the messenger of the congregation in Thyatira, write: These things says the Son of God, who has his eyes as a flame of fire, and his feet like fine brass:
19 Nayajua matendo yako, upendo wako na imani yako, huduma na saburi yako na kwamba matendo yako ya sasa yamezidi yale ya kwanza.
I know your works, and love, and service, and faith, and your patience, and that your last works are more than the first.
20 “Hata hivyo, nina neno dhidi yako: Unamvumilia yule mwanamke Yezebeli ambaye anajiita nabii, lakini anawafundisha na kuwapotosha watumishi wangu ili wafanye uasherati na kula vyakula vilivyotolewa kafara kwa sanamu.
Nevertheless, I have against you, that you permit that woman Jezabel, who says that she is a prophetess, to teach and to seduce my servants to commit fornication, and to eat things sacrificed to idols.
21 Nimempa muda ili atubu kwa ajili ya uasherati wake, lakini hataki.
And I have given her time to reform from her fornication, and she reforms not.
22 Kwa hiyo nitamtupa kwenye kitanda cha mateso, na nitawafanya hao wanaozini naye kupata mateso makali wasipotubia njia zake.
Behold, I will cast her into a bed, and those who commit adultery with her, into great tribulation, unless they reform from their works;
23 Nami nitawaua watoto wake. Nayo makanisa yote yatajua kwamba Mimi ndiye nichunguzaye mioyo na nia, na kwamba nitamlipa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake.
and I will say her children with death; and all the congregations shall know that I am he who search the reins and the heart; and I will give to every one of you according to your works.
24 Basi nawaambia ninyi wengine mlioko Thiatira, ninyi ambao hamyafuati mafundisho ya Yezebeli, wala hamkujifunza hayo yanayoitwa mambo ya ndani sana ya Shetani (sitaweka mzigo mwingine wowote juu yenu):
But I say to you, even to the rest in Thyatira, as many as do not hold this doctrine, and who have not known the depths of Satan, as they speak; I will lay upon you no other burden.
25 Lakini shikeni sana mlicho nacho, mpaka nitakapokuja.
Nevertheless, what you have, hold fast till I come.
26 “Atakayeshinda na kutenda mapenzi yangu mpaka mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa:
And as for him that conquers, and keeps my works to the end, I will give him power over the nations:
27 “‘Atawatawala kwa fimbo ya chuma, atawavunja vipande vipande kama chombo cha udongo’: kama vile mimi nilivyopokea mamlaka kutoka kwa Baba yangu.
and he shall rule them with a rod of iron, they shall be dashed in pieces like a potter's vessel: as I have also received of my Father.
28 Nami nitampa pia ile nyota ya asubuhi.
And I will give him the morning star.
29 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa.
Whoever has an ear, let him hear what the Spirit says to the congregations.