< Ufunuo 2 >

1 “Kwa malaika wa kanisa lililoko Efeso andika: “Haya ndiyo maneno ya yule aliyezishika zile nyota saba katika mkono wake wa kuume na ambaye hutembea kati ya vile vinara saba vya taa vya dhahabu.
“To the messenger of the Ephesian assembly write: These things says He who is holding the seven stars in His right hand, who is walking in the midst of the seven golden lampstands:
2 Nayajua matendo yako, bidii yako na saburi yako. Najua kuwa huwezi kuvumiliana na watu waovu na ya kwamba umewajaribu wale wanaojifanya kuwa mitume na kumbe sio, nawe umewatambua kuwa ni waongo.
I have known your works, and your labor, and your endurance, and that you are not able to bear evil ones, and that you have tried those saying themselves to be apostles and are not, and have found them liars,
3 Umevumilia na kustahimili taabu kwa ajili ya Jina langu, wala hukuchoka.
and you bore, and have endurance, and have toiled because of My Name, and have not been weary.
4 “Lakini nina neno dhidi yako: Umeuacha upendo wako wa kwanza.
But I have against you that you left your first love!
5 Kumbuka basi ni wapi ulikoangukia! Tubu na ukafanye matendo yale ya kwanza. Kama usipotubu, nitakuja kwako na kukiondoa kinara chako cha taa kutoka mahali pake.
Remember, then, from where you have fallen, and convert, and do the first works; and if not, I come to you quickly, and will remove your lampstand from its place—if you may not convert;
6 Lakini una jambo hili kwa upande wako: Unayachukia matendo ya Wanikolai, ambayo nami pia nayachukia.
but this you have, that you hate the works of the Nicolaitans, that I also hate.
7 “Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye, nitampa haki ya kula matunda toka kwa mti wa uzima, ambao uko katika paradisoya Mungu.
He who is having an ear—let him hear what the Spirit says to the assemblies: To him who is overcoming—I will give to him to eat of the Tree of Life that is in the midst of the paradise of God.
8 “Kwa malaika wa kanisa lililoko Smirna andika: “Haya ndiyo maneno yake yeye aliye wa Kwanza na wa Mwisho, aliyekufa kisha akafufuka.
And to the messenger of the assembly of the Smyrneans write: These things says the First and the Last, who became dead and lived:
9 Naijua dhiki yako na umaskini wako, lakini wewe ni tajiri! Nayajua masingizio ya wale wasemao kuwa ni Wayahudi lakini sio, bali wao ni sinagogi la Shetani.
I have known your works, and tribulation, and poverty—yet you are rich—and the slander of those saying themselves to be Jews, and are not, but [are] a synagogue of Satan.
10 Usiogope mateso yatakayokupata. Nakuambia ibilisi atawatia baadhi yenu gerezani ili kuwajaribu, nanyi mtapata dhiki kwa muda wa siku kumi. Uwe mwaminifu hata kufa, nami nitakupa taji ya uzima.
Do not be afraid of the things that you are about to suffer; behold, the Devil is about to cast [some] of you into prison, that you may be tried, and you will have tribulation ten days; become faithful to death, and I will give to you the garland of life.
11 “Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye hatadhuriwa kamwe na mauti ya pili.
He who is having an ear—let him hear what the Spirit says to the assemblies: He who is overcoming may not be injured of the second death.
12 “Kwa malaika wa Kanisa lililoko Pergamo andika: “Haya ndiyo maneno yake yeye aliye na upanga mkali wenye makali kuwili.
And to the messenger of the assembly in Pergamos write: These things says He who is having the sharp two-edged sword:
13 Ninajua unakoishi, ni kule ambako Shetani ana kiti chake cha enzi. Lakini umelishika Jina langu. Wala hukuikana imani yako kwangu hata katika siku za shahidi wangu mwaminifu Antipa, ambaye aliuawa katika mji mkuu wenu, ambako ndiko anakoishi Shetani.
I have known your works, and where you dwell—where the throne of Satan [is]—and you hold fast My Name, and you did not deny My faith, even in the days in which Antipas [was] My faithful witness, who was put to death beside you, where Satan dwells.
14 “Hata hivyo, nina mambo machache dhidi yako: Unao watu wafuatao mafundisho ya Balaamu, yule aliyemfundisha Balaki kuwashawishi Waisraeli watende dhambi kwa kula vitu vilivyotolewa kafara kwa sanamu na kufanya uasherati.
But I have a few things against you: that you have there those holding the teaching of Balaam, who taught Balak to cast a stumbling-block before the sons of Israel, to eat idol-sacrifices, and to commit whoredom;
15 Vivyo hivyo unao wale wayashikayo mafundisho ya Wanikolai.
so have you, even you, those holding the teaching of the Nicolaitans—which thing I hate.
16 Basi tubu! Ama sivyo, nitakuja kwako upesi na kupigana na watu hao kwa upanga wa kinywa changu.
Convert! And if not, I come to you quickly, and will fight against them with the sword of My mouth.
17 “Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa. Yeye ashindaye nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa. Nitampa pia jiwe jeupe ambalo juu yake limeandikwa jina jipya asilolijua mtu, isipokuwa yule anayelipokea.
He who is having an ear—let him hear what the Spirit says to the assemblies: To him who is overcoming, I will give to him to eat from the hidden manna, and will give to him a white stone, and on the stone a new name written, that no one knew except him who is receiving [it].
18 “Kwa malaika wa kanisa lililoko Thiatira andika: “Haya ndiyo maneno ya Mwana wa Mungu, ambaye macho yake ni kama mwali wa moto na ambaye miguu yake ni kama shaba iliyosuguliwa sana.
And to the messenger of the assembly of Thyatira write: These things says the Son of God, who is having His eyes as a flame of fire, and His feet like to frankincense-colored brass:
19 Nayajua matendo yako, upendo wako na imani yako, huduma na saburi yako na kwamba matendo yako ya sasa yamezidi yale ya kwanza.
I have known your works, and love, and ministry, and faith, and your endurance, and your works—and the last [are] more than the first.
20 “Hata hivyo, nina neno dhidi yako: Unamvumilia yule mwanamke Yezebeli ambaye anajiita nabii, lakini anawafundisha na kuwapotosha watumishi wangu ili wafanye uasherati na kula vyakula vilivyotolewa kafara kwa sanamu.
But I have a few things against you: that you allow the woman Jezebel, who is calling herself a prophetess, to teach, and to lead astray, My servants to commit whoredom, and to eat idol-sacrifices;
21 Nimempa muda ili atubu kwa ajili ya uasherati wake, lakini hataki.
and I gave to her a time that she might convert from her whoredom, and she did not convert;
22 Kwa hiyo nitamtupa kwenye kitanda cha mateso, na nitawafanya hao wanaozini naye kupata mateso makali wasipotubia njia zake.
behold, I will cast her into a bed, and those committing adultery with her into great tribulation—if they may not convert from her works,
23 Nami nitawaua watoto wake. Nayo makanisa yote yatajua kwamba Mimi ndiye nichunguzaye mioyo na nia, na kwamba nitamlipa kila mmoja wenu kwa kadiri ya matendo yake.
and I will kill her children in death, and all the assemblies will know that I am He who is searching affections and hearts; and I will give to you—to each—according to your works.
24 Basi nawaambia ninyi wengine mlioko Thiatira, ninyi ambao hamyafuati mafundisho ya Yezebeli, wala hamkujifunza hayo yanayoitwa mambo ya ndani sana ya Shetani (sitaweka mzigo mwingine wowote juu yenu):
And to you I say, and to the rest who are in Thyatira, as many as do not have this teaching, and who did not know the depths of Satan, as they say—I will not put on you another burden,
25 Lakini shikeni sana mlicho nacho, mpaka nitakapokuja.
but hold that which you have, until I may come;
26 “Atakayeshinda na kutenda mapenzi yangu mpaka mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa:
and he who is overcoming, and who is keeping My works to the end, I will give to him authority over the nations,
27 “‘Atawatawala kwa fimbo ya chuma, atawavunja vipande vipande kama chombo cha udongo’: kama vile mimi nilivyopokea mamlaka kutoka kwa Baba yangu.
and he will rule them with a rod of iron—they will be broken as the vessels of the potter—as I have also received from My Father;
28 Nami nitampa pia ile nyota ya asubuhi.
and I will give to him the morning star.
29 Yeye aliye na sikio na asikie yale ambayo Roho ayaambia makanisa.
He who is having an ear—let him hear what the Spirit says to the assemblies.”

< Ufunuo 2 >