< Ufunuo 19 >

1 Baada ya haya nikasikia sauti kama ya umati mkubwa mbinguni wakipiga kelele wakisema: “Haleluya! Wokovu na utukufu na uweza ni vya Mungu wetu,
After these things I heard as it were a loud voice of a great multitude in heaven, saying, Hallelujah I The salvation, and the glory, and the power, belong to our God;
2 kwa maana hukumu zake ni za kweli na za haki. Amemhukumu yule kahaba mkuu aliyeuharibu ulimwengu kwa uzinzi wake. Mungu amemlipiza kisasi kwa ajili ya damu ya watumishi wake.”
for true and righteous are his judgments; for he hath judged the great harlot, who corrupted the earth with her fornication, and hath avenged the blood of his servants at her hand.
3 Wakasema tena kwa nguvu: “Haleluya! Moshi wake huyo kahaba unapanda juu milele na milele.” (aiōn g165)
And a second time they said, Hallelujah! and her smoke goeth up for ever and ever. (aiōn g165)
4 Wale wazee ishirini na wanne pamoja na wale viumbe wanne wenye uhai wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu, aliyekuwa ameketi kwenye kile kiti cha enzi. Wakasema kwa sauti kuu: “Amen, Haleluya!”
And the twenty-four elders and the four living creatures fell down and worshipped God that sat on the throne, saying, Amen, hallelujah!
5 Kisha sauti ikatoka katika kile kiti cha enzi, ikisema: “Msifuni Mungu wetu, ninyi watumishi wake wote, ninyi nyote mnaomcha, wadogo kwa wakubwa!”
And a voice came forth from the throne, saying, Praise our God, all ye his servants, and ye that fear him, the small and the great.
6 Kisha nikasikia sauti kama ya umati mkubwa, kama sauti ya maji mengi yaendayo kasi na kama ngurumo kubwa ya radi wakipiga kelele wakisema: “Haleluya! Kwa maana Bwana Mungu wetu Mwenyezi anatawala.
And I heard as it were the voice of a great multitude, and as the voice of many waters, and as the voice of mighty thunders, saying, Hallelujah! for the Lord our God the Almighty reigneth.
7 Tufurahi, tushangilie na kumpa utukufu! Kwa maana arusi ya Mwana-Kondoo imewadia na bibi arusi wake amejiweka tayari.
Let us rejoice and exult, and we will give to him the glory; for the marriage of the Lamb is come, and his wife hath made herself ready;
8 Akapewa kitani safi, nyeupe inayongʼaa, ili avae.” (Hiyo kitani safi inawakilisha matendo ya haki ya watakatifu.)
and it was given to her that she should be clothed in fine linen, shining and pure. For the fine linen is the righteousness of the saints.
9 Ndipo malaika akaniambia, “Andika: ‘Wamebarikiwa wale walioalikwa kwenye karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo!’” Naye akaongeza kusema, “Haya ndiyo maneno ya kweli ya Mungu.”
And he saith to me, Write, Blessed are they who are called to the marriage-supper of the Lamb. And he saith to me, These are the true words of God.
10 Ndipo nikaanguka kifudifudi miguuni pake ili kumwabudu, lakini yeye akaniambia, “Usifanye hivyo! Mimi pia ni mtumishi mwenzako pamoja na ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Mwabudu Mungu! Maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii.”
And I fell at his feet to worship him; and he saith to me, See thou do it not; I am a fellow-servant of thee, and of thy brethren who maintain the testimony to Jesus; worship God. For the testimony to Jesus is the spirit of prophecy.
11 Kisha nikaona mbingu imefunguka na hapo mbele yangu akiwepo farasi mweupe, ambaye yeye aliyempanda aliitwa Mwaminifu na Kweli. Yeye huhukumu kwa haki na kufanya vita.
And I saw heaven opened, and behold, a white horse, and he who sat upon him was called Faithful and True, and in righteousness he doth judge and make war.
12 Macho yake ni kama miali ya moto na juu ya kichwa chake kuna taji nyingi. Ana jina lililoandikwa ambalo hakuna mtu yeyote anayelijua isipokuwa yeye mwenyewe.
His eyes were a flame of fire, and on his head were many diadems; and he had names written, and a name written which no one knoweth but he himself;
13 Amevaa joho lililochoviwa katika damu, na Jina lake ni “Neno la Mungu.”
and he was clothed with a garment dipped in blood; and his name is called, The Word of God.
14 Majeshi ya mbinguni walikuwa wakimfuata, wakiwa wamepanda farasi weupe, hali wamevaa mavazi ya kitani safi, nyeupe na nzuri.
And the armies which are in heaven followed him upon white horses, clothed in fine linen, white and pure.
15 Kinywani mwake hutoka upanga mkali ambao kwa huo atayaangusha mataifa. “Atayatawala kwa fimbo yake ya utawala ya chuma.” Hulikanyaga shinikizo la mvinyo wa ghadhabu ya Mungu Mwenyezi.
And out of his mouth goeth a sharp sword, that with it he may smite the nations; and he will rule them with a rod of iron; and he treadeth the wine-press of the fierceness of the wrath of God Almighty.
16 Kwenye joho lake na paja lake pameandikwa jina hili: Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana.
And he hath on his garment and on his thigh a name written: KING OF KINGS, AND LORD OF LORDS.
17 Nami nikamwona malaika amesimama ndani kwenye jua, akaita ndege wote warukao angani kwa sauti kuu, “Njooni, kusanyikeni kwa ajili ya karamu kubwa ya Mungu,
And I saw an angel standing in the sun; and he cried with a loud voice, saying to all the birds that fly in mid-heaven, Come, gather yourselves together to the great supper of God;
18 ili mpate kula nyama ya wafalme na ya majemadari, ya mashujaa, ya farasi na ya wapanda farasi, nyama ya wanadamu, wote walio huru na watumwa, wadogo na wakubwa.”
that ye may eat the flesh of kings, and the flesh of captains, and the flesh of mighty men, and the flesh of horses, and of those who sit on them, and the flesh of all men, both free and bond, lieth small and great.
19 Kisha nikamwona yule mnyama na wafalme wa dunia pamoja na majeshi yao wakiwa wamekusanyika pamoja ili kufanya vita dhidi ya yule aliyempanda farasi pamoja na jeshi lake.
And I saw the beast, and the kings of the earth, and their armies, gathered together to make war against him who sat on the horse, and against his army.
20 Lakini yule mnyama akakamatwa pamoja na huyo nabii wa uongo ambaye alikuwa amefanya ishara kwa niaba ya huyo mnyama, ambaye kwa ishara hizi aliwadanganya wale waliopokea chapa ya huyo mnyama na kuiabudu sanamu yake. Hawa wawili wakatupwa wakiwa hai ndani ya ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti. (Limnē Pyr g3041 g4442)
And the beast was seized and he who was with him, the false prophet who wrought the signs in his presence, with which he deceived those who received the mark of the beast, and who worshipped his image; the two were cast alive into the lake of fire burning with brimstone. (Limnē Pyr g3041 g4442)
21 Wale waliosalia waliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa yule aliyekuwa amempanda farasi nao ndege wote wakajishibisha kwa nyama yao.
And the rest were slain with the sword of him who sat upon the horse, the sword which proceeded out of his mouth; and all the birds were glutted with their flesh.

< Ufunuo 19 >