< Ufunuo 19 >

1 Baada ya haya nikasikia sauti kama ya umati mkubwa mbinguni wakipiga kelele wakisema: “Haleluya! Wokovu na utukufu na uweza ni vya Mungu wetu,
After these things I heard as it were a great voice of a vast multitude in the heaven, saying, Hallelujah! Salvation, and glary, and power, belong to our God:
2 kwa maana hukumu zake ni za kweli na za haki. Amemhukumu yule kahaba mkuu aliyeuharibu ulimwengu kwa uzinzi wake. Mungu amemlipiza kisasi kwa ajili ya damu ya watumishi wake.”
because his judgments are true and righteous; because he has judged the great harlot, who corrupted the earth by her fornication, and he has avenged the blood of his servants from her hand.
3 Wakasema tena kwa nguvu: “Haleluya! Moshi wake huyo kahaba unapanda juu milele na milele.” (aiōn g165)
And a second time they said, Hallelujah! and her smoke is going up unto the ages of the ages. (aiōn g165)
4 Wale wazee ishirini na wanne pamoja na wale viumbe wanne wenye uhai wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu, aliyekuwa ameketi kwenye kile kiti cha enzi. Wakasema kwa sauti kuu: “Amen, Haleluya!”
And the twenty-four elders and the four living creatures fell down and worshiped God who sitteth upon the throne, saying Amen; Hallelujah!
5 Kisha sauti ikatoka katika kile kiti cha enzi, ikisema: “Msifuni Mungu wetu, ninyi watumishi wake wote, ninyi nyote mnaomcha, wadogo kwa wakubwa!”
And a voice came out from the throne, saying, Praise our God, all ye his servants, ye who fear him, small and great.
6 Kisha nikasikia sauti kama ya umati mkubwa, kama sauti ya maji mengi yaendayo kasi na kama ngurumo kubwa ya radi wakipiga kelele wakisema: “Haleluya! Kwa maana Bwana Mungu wetu Mwenyezi anatawala.
And I heard as it were the voice of a great multitude, and as the sound of many waters, and as the sound of mighty thunders, saying, Hallelujah! because the Lord our God Omnipotent reigned.
7 Tufurahi, tushangilie na kumpa utukufu! Kwa maana arusi ya Mwana-Kondoo imewadia na bibi arusi wake amejiweka tayari.
Let us rejoice and be glad, and give glory to him! because the marriage of the Lamb has come, and his wife has made herself ready.
8 Akapewa kitani safi, nyeupe inayongʼaa, ili avae.” (Hiyo kitani safi inawakilisha matendo ya haki ya watakatifu.)
And it was given unto her that she should be clothed in linen, bright and clean. For the linen is the righteous acts of the saints.
9 Ndipo malaika akaniambia, “Andika: ‘Wamebarikiwa wale walioalikwa kwenye karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo!’” Naye akaongeza kusema, “Haya ndiyo maneno ya kweli ya Mungu.”
And he says to me, Write, Blessed are they who have been called to the marriage supper of the Lamb. And He says to me, These are the true words of God.
10 Ndipo nikaanguka kifudifudi miguuni pake ili kumwabudu, lakini yeye akaniambia, “Usifanye hivyo! Mimi pia ni mtumishi mwenzako pamoja na ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Mwabudu Mungu! Maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii.”
And I fell down before his feet to worship him. And he says to me; See that you do it not: I am your fellow-servant, and one of your brethren who have the testimony of Jesus; worship God. For the testimony of Jesus is the spirit of prophecy.
11 Kisha nikaona mbingu imefunguka na hapo mbele yangu akiwepo farasi mweupe, ambaye yeye aliyempanda aliitwa Mwaminifu na Kweli. Yeye huhukumu kwa haki na kufanya vita.
And I saw the heaven open, and behold a white horse; and one sitting on him called, Faithful and True, in righteousness he both judges and wages war.
12 Macho yake ni kama miali ya moto na juu ya kichwa chake kuna taji nyingi. Ana jina lililoandikwa ambalo hakuna mtu yeyote anayelijua isipokuwa yeye mwenyewe.
And his eyes are a flame of fire, and upon his head are many diadems; having a name written, which no one knows, but himself,
13 Amevaa joho lililochoviwa katika damu, na Jina lake ni “Neno la Mungu.”
and being clothed with a garment sprinkled with blood: and his name has been called, The Word of God.
14 Majeshi ya mbinguni walikuwa wakimfuata, wakiwa wamepanda farasi weupe, hali wamevaa mavazi ya kitani safi, nyeupe na nzuri.
Armies in the heaven follow him on white horses, clothed in linen, white and clean.
15 Kinywani mwake hutoka upanga mkali ambao kwa huo atayaangusha mataifa. “Atayatawala kwa fimbo yake ya utawala ya chuma.” Hulikanyaga shinikizo la mvinyo wa ghadhabu ya Mungu Mwenyezi.
And out of his mouth goes forth a sharp sword, that with it he may smite the nations; and he will shepherdize them with an iron rod: and he treads the winepress of the wrath of the indignation of God Almighty.
16 Kwenye joho lake na paja lake pameandikwa jina hili: Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana.
And he has on his vesture and on his thigh a name written, King of kings, and Lord of lords.
17 Nami nikamwona malaika amesimama ndani kwenye jua, akaita ndege wote warukao angani kwa sauti kuu, “Njooni, kusanyikeni kwa ajili ya karamu kubwa ya Mungu,
And I saw one angel standing on the sun; and he cried with a great voice, saying to all the birds which fly in the midst of heaven, Come, gather yourselves to the great banquet of God;
18 ili mpate kula nyama ya wafalme na ya majemadari, ya mashujaa, ya farasi na ya wapanda farasi, nyama ya wanadamu, wote walio huru na watumwa, wadogo na wakubwa.”
in order that you may eat the flesh of kings, and the flesh of chiliarchs, and the flesh of mighty men, and the flesh of horses and of those sitting on them, and the flesh of all free men and slaves also, both small and great.
19 Kisha nikamwona yule mnyama na wafalme wa dunia pamoja na majeshi yao wakiwa wamekusanyika pamoja ili kufanya vita dhidi ya yule aliyempanda farasi pamoja na jeshi lake.
And I saw the beast, and the kings of the earth, and their armies, assembled to make war with the one sitting on the horse, and with his army.
20 Lakini yule mnyama akakamatwa pamoja na huyo nabii wa uongo ambaye alikuwa amefanya ishara kwa niaba ya huyo mnyama, ambaye kwa ishara hizi aliwadanganya wale waliopokea chapa ya huyo mnyama na kuiabudu sanamu yake. Hawa wawili wakatupwa wakiwa hai ndani ya ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti. (Limnē Pyr g3041 g4442)
And the beast, and the false prophet along with him, who wrought miracles in his presence, by which he deceived those having received the mark of the beast, and those worshiping his image; and the two were cast alive into the lake of fire which burns with brimstone. (Limnē Pyr g3041 g4442)
21 Wale waliosalia waliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa yule aliyekuwa amempanda farasi nao ndege wote wakajishibisha kwa nyama yao.
And the rest were slain with the sword proceeding out from the mouth of him, the one sitting on the horse: and all the birds were filled with their flesh.

< Ufunuo 19 >