< Ufunuo 19 >

1 Baada ya haya nikasikia sauti kama ya umati mkubwa mbinguni wakipiga kelele wakisema: “Haleluya! Wokovu na utukufu na uweza ni vya Mungu wetu,
After these things I heard as it were the really loud voice of a great multitude in heaven saying: “Hallelujah! The salvation and power and glory of our God!
2 kwa maana hukumu zake ni za kweli na za haki. Amemhukumu yule kahaba mkuu aliyeuharibu ulimwengu kwa uzinzi wake. Mungu amemlipiza kisasi kwa ajili ya damu ya watumishi wake.”
Because His judgments are true and just, because He has judged the great whore who corrupted the earth with her fornication, and has avenged the blood of His slaves by her hand.”
3 Wakasema tena kwa nguvu: “Haleluya! Moshi wake huyo kahaba unapanda juu milele na milele.” (aiōn g165)
And a second voice said, “Hallelujah! Her smoke goes up for ever and ever!” (aiōn g165)
4 Wale wazee ishirini na wanne pamoja na wale viumbe wanne wenye uhai wakaanguka kifudifudi, wakamwabudu Mungu, aliyekuwa ameketi kwenye kile kiti cha enzi. Wakasema kwa sauti kuu: “Amen, Haleluya!”
And the twenty-four elders and the four living beings fell down and worshiped God, who sits on the throne, saying, “Amen, Hallelujah!”
5 Kisha sauti ikatoka katika kile kiti cha enzi, ikisema: “Msifuni Mungu wetu, ninyi watumishi wake wote, ninyi nyote mnaomcha, wadogo kwa wakubwa!”
And a voice came from the Throne saying, “Praise our God, all you His slaves and those who fear Him, small and great!”
6 Kisha nikasikia sauti kama ya umati mkubwa, kama sauti ya maji mengi yaendayo kasi na kama ngurumo kubwa ya radi wakipiga kelele wakisema: “Haleluya! Kwa maana Bwana Mungu wetu Mwenyezi anatawala.
And I heard as it were the voice of a great multitude like the sound of many waters and like the sound of mighty thunderings saying: “Hallelujah! Because the Lord our God reigns, the Almighty!
7 Tufurahi, tushangilie na kumpa utukufu! Kwa maana arusi ya Mwana-Kondoo imewadia na bibi arusi wake amejiweka tayari.
Let us rejoice and exult and give Him the glory, because the wedding of the Lamb has come, and His wife has prepared herself.”
8 Akapewa kitani safi, nyeupe inayongʼaa, ili avae.” (Hiyo kitani safi inawakilisha matendo ya haki ya watakatifu.)
And it was granted to her to be dressed in fine linen, bright and pure, for the fine linen is the righteous deeds of the saints.
9 Ndipo malaika akaniambia, “Andika: ‘Wamebarikiwa wale walioalikwa kwenye karamu ya arusi ya Mwana-Kondoo!’” Naye akaongeza kusema, “Haya ndiyo maneno ya kweli ya Mungu.”
And he says to me, “Write: ‘Blessed are those who are invited to the wedding banquet of the Lamb.’” And he says to me, “These are the true words of God.”
10 Ndipo nikaanguka kifudifudi miguuni pake ili kumwabudu, lakini yeye akaniambia, “Usifanye hivyo! Mimi pia ni mtumishi mwenzako pamoja na ndugu zako walio na ushuhuda wa Yesu. Mwabudu Mungu! Maana ushuhuda wa Yesu ndio roho ya unabii.”
And I fell at his feet to worship him, but he says to me: “Don't! I am your fellow slave and among your brothers who hold the testimony of Jesus. Worship God! For the testimony of Jesus is the spirit of prophecy.”
11 Kisha nikaona mbingu imefunguka na hapo mbele yangu akiwepo farasi mweupe, ambaye yeye aliyempanda aliitwa Mwaminifu na Kweli. Yeye huhukumu kwa haki na kufanya vita.
I saw the heaven opened, and wow, a white horse! And the One who sits on it, called Faithful and True, both judges and makes war with righteousness.
12 Macho yake ni kama miali ya moto na juu ya kichwa chake kuna taji nyingi. Ana jina lililoandikwa ambalo hakuna mtu yeyote anayelijua isipokuwa yeye mwenyewe.
Now His eyes were a flame of fire and on His head were many diadems, having names written, besides a written name that no one knows except Himself;
13 Amevaa joho lililochoviwa katika damu, na Jina lake ni “Neno la Mungu.”
and He was clothed with a robe that had been dipped in blood, and His name is called The Word of God.
14 Majeshi ya mbinguni walikuwa wakimfuata, wakiwa wamepanda farasi weupe, hali wamevaa mavazi ya kitani safi, nyeupe na nzuri.
And the armies in heaven, clothed in fine linen, white, clean, followed Him on white horses.
15 Kinywani mwake hutoka upanga mkali ambao kwa huo atayaangusha mataifa. “Atayatawala kwa fimbo yake ya utawala ya chuma.” Hulikanyaga shinikizo la mvinyo wa ghadhabu ya Mungu Mwenyezi.
And out of His mouth goes a sharp, two-edged sword, so that with it He may strike the nations. And He Himself will shepherd them with a rod of iron. And He Himself treads the winepress of the fury of the wrath of God, the Almighty.
16 Kwenye joho lake na paja lake pameandikwa jina hili: Mfalme wa wafalme, na Bwana wa mabwana.
And He has a name written on His robe and on His thigh, King of kings and Lord of lords!
17 Nami nikamwona malaika amesimama ndani kwenye jua, akaita ndege wote warukao angani kwa sauti kuu, “Njooni, kusanyikeni kwa ajili ya karamu kubwa ya Mungu,
And I saw an angel standing in the sun; and he cried out with a loud voice, saying to all the birds that fly in midheaven, “Come, gather together to the great dinner of God,
18 ili mpate kula nyama ya wafalme na ya majemadari, ya mashujaa, ya farasi na ya wapanda farasi, nyama ya wanadamu, wote walio huru na watumwa, wadogo na wakubwa.”
so that you may eat flesh of kings and flesh of commanders and flesh of the mighty and flesh of horses along with their riders, even the flesh of all, both free and slave, both small and great.”
19 Kisha nikamwona yule mnyama na wafalme wa dunia pamoja na majeshi yao wakiwa wamekusanyika pamoja ili kufanya vita dhidi ya yule aliyempanda farasi pamoja na jeshi lake.
And I saw the Beast and the kings of the earth and their armies gathered together to make war against the One riding the horse and against His army.
20 Lakini yule mnyama akakamatwa pamoja na huyo nabii wa uongo ambaye alikuwa amefanya ishara kwa niaba ya huyo mnyama, ambaye kwa ishara hizi aliwadanganya wale waliopokea chapa ya huyo mnyama na kuiabudu sanamu yake. Hawa wawili wakatupwa wakiwa hai ndani ya ziwa la moto liwakalo kwa kiberiti. (Limnē Pyr g3041 g4442)
So the Beast was captured, and with him the False prophet, the one who performed signs in his presence (by which he had deceived those who had received the mark of the Beast and those who worshiped his image). The two were thrown alive into the Lake of Fire that burns with brimstone. (Limnē Pyr g3041 g4442)
21 Wale waliosalia waliuawa kwa upanga uliotoka kinywani mwa yule aliyekuwa amempanda farasi nao ndege wote wakajishibisha kwa nyama yao.
And the rest were killed by the sword that proceeds from the mouth of the One riding the horse. And all the birds were filled with their flesh.

< Ufunuo 19 >