< Ufunuo 18 >

1 Baada ya haya nikaona malaika mwingine akishuka kutoka mbinguni, akiwa na mamlaka makuu na dunia ikamulikiwa na mngʼao wake.
And after these things I saw another angel come down from heaven, having great power; and the earth was enlightened with his glory.
2 Naye akalia kwa nguvu kwa sauti kubwa, akisema: “Umeanguka! Umeanguka Babeli Mkuu! Umekuwa makao ya mashetani na makazi ya kila pepo mchafu, makazi ya kila ndege na kila mnyama achukizaye.
And he cried with vehemence, and with a loud voice, saying, Babylon the great is fallen, is fallen, and is become the habitation of demons, a den of impure spirits, and a cage for every unclean and hateful bird.
3 Kwa maana mataifa yote yamekunywa mvinyo wa ghadhabu ya uasherati wake. Nao wafalme wa dunia wamefanya uzinzi nao, nao wafanyabiashara wa dunia wametajirika kutokana na wingi wa utajiri wake.”
For all nations have drunk of the wine of her furious whoredom, and the kings of the earth have committed whoredom with her, and the merchants of the earth are grown rich by the abundance of her luxury.
4 Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni ikisema: “Tokeni katikati yake, enyi watu wangu, ili msije mkashiriki dhambi zake, ili msije mkapatwa na pigo lake lolote;
And I heard another voice from heaven, saying, Come out from her, my people, that ye be not partakers of her sins, and that ye may not suffer by her plagues:
5 kwa kuwa dhambi zake zimelundikana hadi mbinguni, naye Mungu ameukumbuka uhalifu wake.
for her sins have reached unto heaven, and God hath remembered her iniquities.
6 Mtendee kama yeye alivyotenda; umlipe mara mbili kwa ajili ya yale aliyotenda. Katika kikombe chake mchanganyie mara mbili ya kile alichochanganya.
Give to her as she hath given to you, and repay her double according to her works: in the cup, which she hath mixed, mix for her double.
7 Mpatie mateso na huzuni nyingi sawa na utukufu na anasa alizojipatia. Kwa kuwa moyoni mwake hujivuna, akisema, ‘Mimi ninatawala kama malkia; mimi si mjane, wala sitaona huzuni kamwe.’
As much as she hath glorified herself and indulged to luxury, so much torment and sorrow give her; because she saith in her heart, I sit as a queen, I am not a widow, and I shall see no sorrow.
8 Kwa hiyo mapigo yatampata kwa siku moja: mauti, maombolezo na njaa. Naye atateketezwa kwa moto, kwa maana Bwana Mungu amhukumuye ana nguvu.
Therefore in one day shall her plagues come, even death and mourning and famine; and she shall be burnt with fire: for strong is the Lord God who judgeth her.
9 “Wafalme wa dunia waliozini naye na kushiriki anasa zake watakapoona moshi wa kuungua kwake, watamlilia na kumwombolezea.
And the kings of the earth, who have committed lewdness and lived luxuriously with her, shall bemoan her and lament for her, when they see the smoke of her burning;
10 Kwa hofu kubwa ya mateso yake, watasimama mbali na kulia na wakisema: “‘Ole! Ole, ee mji mkubwa, ee Babeli mji wenye nguvu! Hukumu yako imekuja katika saa moja!’
standing afar off for fear of her torment, saying, Alas, alas, the great city Babylon, that powerful city! for in one hour is thy judgement come.
11 “Wafanyabiashara wa dunia watalia na kumwomboleza kwa sababu hakuna anunuaye bidhaa zao tena:
And the merchants of the earth shall bewail and mourn over her, because no one will buy their merchandize any more:
12 Bidhaa za dhahabu, za fedha, za vito vya thamani na vya lulu, kitani safi, nguo za rangi ya zambarau, hariri, nguo nyekundu, aina zote za miti ya udi, na vifaa vyote vya pembe za ndovu, vifaa vyote vya miti yenye thamani kuliko yote, shaba, chuma na marmar,
the lading of gold, and silver, and precious stones, and pearl, and fine linen, and purple, and silk, and all sorts of thyine wood, and vessels of ivory, and of the most precious wood, and of brass, and iron, and marble;
13 bidhaa za mdalasini, vikolezi, za uvumba, manemane, na uvumba wenye harufu nzuri, za divai, na mafuta ya zeituni, za unga mzuri na ngano; ngʼombe na kondoo; farasi na magari; na miili na roho za wanadamu.
and their cinnamon, and perfumes, and sweet ointment, and incense, and wine, and oil, and fine flour, and wheat, and cattle, and sheep, and horses, and chariots, and slaves, yea and the souls of men.
14 “Watasema, ‘Yale matunda ambayo roho yako iliyatamani yamekoma. Utajiri wako wote na fahari yako vimetoweka, wala haviwezi kupatikana tena kamwe!’
And the fruits, which thy soul longed after, are gone from thee, and all thy delicate and splendid things are departed, and thou shalt find them no more.
15 Wale wafanyabiashara waliotajirika kwa bidhaa hizo kutoka kwake watasimama mbali naye kwa hofu kubwa ya mateso yanayompata. Watalia na kuomboleza wakipiga kelele wakisema:
The merchants of these things, who grew rich by their trade with her, shall stand afar off for fear of her torment, weeping and mourning,
16 “‘Ole! Ole, ee mji mkubwa, uliyekuwa umevikwa mavazi ya kitani safi, ya rangi ya zambarau na nyekundu, ukimetameta kwa dhahabu, vito vya thamani na lulu!
and saying, Alas, alas, the great city, that was clothed in fine linen, and purple, and scarlet, and adorned with gold, and precious stones, and pearls!
17 Katika muda wa saa moja utajiri wote mkubwa kama huu umeangamia!’ “Kila nahodha, na wote wasafirio kwa meli, na wote wapatao kipato chao kutokana na bahari, watasimama mbali.
for in one hour is so great wealth laid waste. And every pilot, and all on board the ships, and the mariners, and all that traffic by sea, stood afar off,
18 Watakapouona moshi wa kuungua kwake watalia wakisema, ‘Je, kulipata kuwako mji mkubwa kama huu?’
and cried out, when they saw the smoke of her burning, saying, What city is like to this great city?
19 Nao watajirushia mavumbi vichwani mwao, huku wakilia na kuomboleza, wakisema: “‘Ole! Ole, ee mji mkubwa, mji ambao wote wenye meli baharini walitajirika kupitia kwa mali zake! Katika saa moja tu ameangamizwa!
And they threw dust on their heads, and cried out, weeping and moaning, saying, Alas, alas, that great city, in which all that had ships at sea were enriched by her sumptuous expences! for in one hour she is become desolate.
20 Furahia kwa ajili yake, ee mbingu! Furahini watakatifu, mitume na manabii! Mungu amemhukumu kwa vile alivyowatendea ninyi.’”
Rejoice over her, O heaven, and ye holy apostles and prophets, for God hath avenged you on her.
21 Kisha malaika mmoja mwenye nguvu akainua jiwe kubwa kama la kusagia akalitupa baharini akisema: “Hivyo ndivyo mji mkubwa Babeli utakavyotupwa chini kwa nguvu wala hautaonekana tena.
And a mighty angel took up a stone like a great milstone, and cast it into the sea, saying, Thus shall the great city Babylon be thrown down with violence, and never be found more.
22 Nyimbo za wapiga vinubi na waimbaji, wapiga filimbi na wapiga tarumbeta kamwe hazitasikika tena ndani yako. Ndani yako kamwe hataonekana tena fundi mwenye ujuzi wa aina yoyote. Wala sauti ya jiwe la kusagia kamwe haitasikika tena.
And the voice of harpers, and musicians, and pipers, and trumpeters, shall be heard in thee no more: and no artist of any art whatsoever shall be found in thee any more; and the sound of a milstone shall be heard in thee no more.
23 Mwanga wa taa hautaangaza ndani yako tena. Sauti ya bwana arusi na bibi arusi kamwe haitasikika ndani yako tena. Wafanyabiashara wako walikuwa watu maarufu wa dunia. Mataifa yote yalipotoshwa kwa uchawi wako.
And the light of a candle shall be seen in thee no more; and the voice of the bridegroom and bride shall be heard no more in thee: for thy merchants were the great men of the earth, and by thy sorceries were all nations deceived.
24 Ndani yake ilionekana damu ya manabii na ya watakatifu na wote waliouawa duniani.”
And herein was found the blood of prophets and saints, and of all that were slain upon the earth.

< Ufunuo 18 >