< Ufunuo 16 >

1 Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mle Hekaluni ikiwaambia wale malaika saba, “Nendeni, mkayamwage duniani hayo mabakuli saba ya ghadhabu ya Mungu.”
Then I heard a loud voice from the sanctuary say to the seven angels, "Go and pour on to the earth the seven bowls of the anger of God."
2 Malaika wa kwanza akaenda akalimwaga hilo bakuli lake juu ya nchi. Majipu mabaya yenye maumivu makali yakawapata wale watu wote waliokuwa na chapa ya yule mnyama na walioabudu sanamu yake.
So the first angel went away and poured his bowl on to the earth; and it brought a bad and painful sore upon the men who had on them the mark of the Wild Beast and worshipped his statue.
3 Malaika wa pili akalimwaga bakuli lake baharini, nayo ikabadilika kuwa damu kama ya mtu aliyekufa na kila kiumbe hai kilichokuwa ndani ya bahari kikafa.
The second angel poured his bowl into the sea, and it became blood, like a dead man's blood, and every living creature in the sea died.
4 Malaika wa tatu akalimwaga bakuli lake katika mito na chemchemi za maji, nazo zikawa damu.
The third angel poured his bowl into the rivers and springs of water, and they became blood.
5 Ndipo nikamsikia malaika msimamizi wa maji akisema: “Wewe una haki katika hukumu hizi ulizotoa, wewe uliyeko, uliyekuwako, Uliye Mtakatifu, kwa sababu umehukumu hivyo;
And I heard the angel of the waters say, "Righteous art Thou, who art and wast, the holy One, because Thou hast thus taken vengeance.
6 kwa kuwa walimwaga damu ya watakatifu wako na manabii wako, nawe umewapa damu wanywe kama walivyostahili.”
For they poured out the blood of Thy people and of the Prophets, and in return Thou hast given them blood to drink. And this they deserved."
7 Nikasikia madhabahu ikiitikia, “Naam, Bwana Mungu Mwenyezi, hukumu zako ni kweli na haki.”
And I heard a voice from the altar say, "Even so, O Lord God, the Ruler of all, true and righteous are Thy judgments."
8 Malaika wa nne akamimina bakuli lake kwenye jua, nalo likapewa nguvu za kuwaunguza watu kwa moto.
Then the fourth angel poured his bowl on to the sun, and power was given to it to scorch men with fire.
9 Watu wakaunguzwa na hilo joto kali, wakalaani Jina la Mungu, aliyekuwa na uwezo juu ya mapigo haya, tena wakakataa kutubu na kumtukuza Mungu.
And the men were severely burned; and yet they spoke evil of God who had power over the plagues, and they did not repent so as to give Him glory.
10 Malaika wa tano akamimina bakuli lake kwenye kiti cha enzi cha yule mnyama, nao ufalme wake ukagubikwa na giza. Watu wakatafuna ndimi zao kwa ajili ya maumivu,
The fifth angel poured his bowl on to the throne of the Wild Beast; and his kingdom became darkened. People gnawed their tongues because of the pain,
11 wakamlaani Mungu wa mbinguni kwa sababu ya maumivu na majeraha yao, wala hawakutubu kwa ajili ya matendo yao maovu.
and they spoke evil of the God in Heaven because of their pains and their sores, and did not repent of their misconduct.
12 Malaika wa sita akamimina bakuli lake kwenye mto mkubwa Frati, maji yake yakakauka ili kutayarisha njia kwa ajili ya wafalme watokao Mashariki.
The sixth angel poured his bowl into that great river, the Euphrates; and its stream was dried up in order to clear the way for the kings who are to come from the east.
13 Kisha nikaona roho wachafu watatu waliofanana na vyura wakitoka katika kinywa cha lile joka na katika kinywa cha yule mnyama na katika kinywa cha yule nabii wa uongo.
Then I saw three foul spirits, resembling frogs, issue from the mouth of the Dragon, from the mouth of the Wild Beast, and from the mouth of the false Prophet.
14 Hizo ndizo roho za pepo wachafu zitendazo miujiza. Nazo huwaendea wafalme wa ulimwengu wote na kuwakusanya tayari kwa ajili ya vita katika siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.
For they are the spirits of demons working marvels--spirits that go out to control the kings of the whole earth, to assemble them for the battle which is to take place on the great day of God, the Ruler of all.
15 “Tazama, naja kama mwizi! Amebarikiwa yeye akeshaye na kuziweka tayari nguo zake ili asiende uchi na kuonekana aibu yake.”
("I am coming like a thief. Blessed is the man who keeps awake and guards his raiment for fear he walk about ill-clad, and his uncomeliness become manifest.")
16 Ndipo wakawakusanya wafalme pamoja mahali paitwapo Armagedoni kwa Kiebrania.
And assemble them they did at the place called in Hebrew 'Har-Magedon.'
17 Malaika wa saba akamimina bakuli lake angani na sauti kubwa ikatoka mle hekaluni katika kile kiti cha enzi, ikisema, “Imekwisha kuwa!”
Then the seventh angel poured his bowl into the air; and a loud voice came out of the sanctuary from the throne, saying, "Everything is now ready."
18 Kukawa na mianga ya umeme wa radi, ngurumo, radi na tetemeko kubwa la ardhi. Hapajawa kamwe na tetemeko la ardhi kama hilo tangu mwanadamu awepo duniani, hivyo lilikuwa tetemeko kubwa ajabu.
Flashes of lightning followed, and voices, and peals of thunder, and an earthquake more dreadful than there had ever been since there was a man upon the earth--so terrible was it, and so great!
19 Ule mji mkubwa ukagawanyika katika sehemu tatu, nayo miji ya mataifa ikaanguka. Mungu akaukumbuka Babeli Mkuu na kumpa kikombe kilichojaa mvinyo wa ghadhabu ya hasira yake.
The great city was split into three parts; the cities of the nations fell; and great Babylon came into remembrance before God, for Him to make her drink from the wine-cup of His fierce anger.
20 Kila kisiwa kikatoweka wala milima haikuonekana.
Every island fled away, and there was not a mountain anywhere to be seen.
21 Mvua kubwa ya mawe yenye uzito wa talanta moja ikashuka kutoka mbinguni, ikawaangukia wanadamu. Nao wanadamu wakamlaani Mungu kwa ajili ya hayo mapigo ya mvua ya mawe, kwa sababu pigo hilo lilikuwa la kutisha.
And heavy hail, that seemed to be a talent in weight, fell from the sky upon the people; and they spoke evil of God on account of the plague of the hail--because the plague of it was exceedingly severe.

< Ufunuo 16 >