< Ufunuo 16 >
1 Kisha nikasikia sauti kubwa kutoka mle Hekaluni ikiwaambia wale malaika saba, “Nendeni, mkayamwage duniani hayo mabakuli saba ya ghadhabu ya Mungu.”
聽見由殿裏發出一個大聲音,向那七位天使說:「你們去,把那滿盛天主義怒的七個盂倒在地上!」
2 Malaika wa kwanza akaenda akalimwaga hilo bakuli lake juu ya nchi. Majipu mabaya yenye maumivu makali yakawapata wale watu wote waliokuwa na chapa ya yule mnyama na walioabudu sanamu yake.
第一位天使便去,把他的盂倒在地上,遂在那些帶有獸印和朝拜獸像的人身上,生出了一種惡毒而劇痛的瘡。
3 Malaika wa pili akalimwaga bakuli lake baharini, nayo ikabadilika kuwa damu kama ya mtu aliyekufa na kila kiumbe hai kilichokuwa ndani ya bahari kikafa.
第二位天使把他的盂倒在海裏,海水就變成好似死人的血,因而海中的一切活物都死了。
4 Malaika wa tatu akalimwaga bakuli lake katika mito na chemchemi za maji, nazo zikawa damu.
第三位天使把他的盂倒在河流和水泉上,水就變成了血。
5 Ndipo nikamsikia malaika msimamizi wa maji akisema: “Wewe una haki katika hukumu hizi ulizotoa, wewe uliyeko, uliyekuwako, Uliye Mtakatifu, kwa sababu umehukumu hivyo;
那時,我聽見掌管水的天使說:「今在和昔在的聖善者,你這樣懲罰,真是公義,
6 kwa kuwa walimwaga damu ya watakatifu wako na manabii wako, nawe umewapa damu wanywe kama walivyostahili.”
因為他們曾傾流了聖徒和先知們的血,你如今給他們血喝,這是他們應得的。」
7 Nikasikia madhabahu ikiitikia, “Naam, Bwana Mungu Mwenyezi, hukumu zako ni kweli na haki.”
我又聽見從祭壇有聲音說:「是的,上主,全能的天主!你的懲罰,真實而公義。」
8 Malaika wa nne akamimina bakuli lake kwenye jua, nalo likapewa nguvu za kuwaunguza watu kwa moto.
第四位天使把他的盂倒在太陽上,致使太陽以烈火炙烤世人。
9 Watu wakaunguzwa na hilo joto kali, wakalaani Jina la Mungu, aliyekuwa na uwezo juu ya mapigo haya, tena wakakataa kutubu na kumtukuza Mungu.
世人因被劇熱所炙烤,便褻瀆掌管這些災禍的天主的名號,沒有悔改將光榮歸於天主。
10 Malaika wa tano akamimina bakuli lake kwenye kiti cha enzi cha yule mnyama, nao ufalme wake ukagubikwa na giza. Watu wakatafuna ndimi zao kwa ajili ya maumivu,
第五位天使把他的盂倒在那獸座上,牠的王國就陷入黑暗,人痛苦的咬自己的舌頭;
11 wakamlaani Mungu wa mbinguni kwa sababu ya maumivu na majeraha yao, wala hawakutubu kwa ajili ya matendo yao maovu.
他們因自己的痛苦和瘡痍,便褻瀆天上的天主,沒有悔改自己的行為。
12 Malaika wa sita akamimina bakuli lake kwenye mto mkubwa Frati, maji yake yakakauka ili kutayarisha njia kwa ajili ya wafalme watokao Mashariki.
第六位天使把他的盂倒在幼發拉的大河中,河水就乾涸了,為給那些由日出之地要來的諸王,準備了一條道路。
13 Kisha nikaona roho wachafu watatu waliofanana na vyura wakitoka katika kinywa cha lile joka na katika kinywa cha yule mnyama na katika kinywa cha yule nabii wa uongo.
我又看見從龍口、獸口和假先知口中出來了三個不潔的神,狀如青蛙;
14 Hizo ndizo roho za pepo wachafu zitendazo miujiza. Nazo huwaendea wafalme wa ulimwengu wote na kuwakusanya tayari kwa ajili ya vita katika siku ile kuu ya Mungu Mwenyezi.
他們是邪魔之神,施行奇蹟,往全世界的諸王那裏去,召集他們,為在全能天主的那偉大日子上交戰。「
15 “Tazama, naja kama mwizi! Amebarikiwa yeye akeshaye na kuziweka tayari nguo zake ili asiende uchi na kuonekana aibu yake.”
看,我來有如盜賊一樣;那醒著並保持自己的衣服,不至於赤身行走,而叫人看見自己的恥辱的,纔是有福的!」
16 Ndipo wakawakusanya wafalme pamoja mahali paitwapo Armagedoni kwa Kiebrania.
那三個神就把諸王聚集到一個地方,那地方希伯來文叫「阿瑪革冬。」
17 Malaika wa saba akamimina bakuli lake angani na sauti kubwa ikatoka mle hekaluni katika kile kiti cha enzi, ikisema, “Imekwisha kuwa!”
第七位天使把他的盂倒在空氣中,於是就由【天上的】殿裏,從寶座那裏發出了一個巨大聲音說:「成了!」
18 Kukawa na mianga ya umeme wa radi, ngurumo, radi na tetemeko kubwa la ardhi. Hapajawa kamwe na tetemeko la ardhi kama hilo tangu mwanadamu awepo duniani, hivyo lilikuwa tetemeko kubwa ajabu.
遂有閃電、響聲和雷霆,又發生了大地震,是自從在地上有人類以來,從未有過這樣大的地震。
19 Ule mji mkubwa ukagawanyika katika sehemu tatu, nayo miji ya mataifa ikaanguka. Mungu akaukumbuka Babeli Mkuu na kumpa kikombe kilichojaa mvinyo wa ghadhabu ya hasira yake.
那大城分裂為三段,異民的城也都傾覆了;天主想起了那偉大的巴比倫,遂遞給她那盛滿天主烈怒的酒杯。
20 Kila kisiwa kikatoweka wala milima haikuonekana.
各島嶼都消失了,諸山嶺也不見了。
21 Mvua kubwa ya mawe yenye uzito wa talanta moja ikashuka kutoka mbinguni, ikawaangukia wanadamu. Nao wanadamu wakamlaani Mungu kwa ajili ya hayo mapigo ya mvua ya mawe, kwa sababu pigo hilo lilikuwa la kutisha.
又有像「塔冷通」般的大冰雹,從天上落在世人的身上;世人因冰雹的災禍便褻瀆天主,因為那災禍太慘重了。