< Ufunuo 15 >

1 Ndipo nikaona ishara nyingine kubwa ya ajabu mbinguni: malaika saba wenye yale mapigo saba ya mwisho, kwa sababu kwa mapigo hayo ghadhabu ya Mungu ilikuwa imekamilika.
Och jag såg ett annat tecken i himmelen, stort och underbart; sju änglar med de sju plågor som bliva de sista, ty med dem är Guds vredesdom fullbordad.
2 Nikaona kile kilichoonekana kama bahari ya kioo iliyochanganyikana na moto. Kando ya hiyo bahari, walikuwa wamesimama wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake pamoja na tarakimu ya jina lake. Mikononi mwao walikuwa wameshika vinubi walivyopewa na Mungu.
Och jag fick se något som såg ut såsom ett glashav, blandat med eld. Och jag såg dem som hade vunnit seger över vilddjuret, med dess bild och dess namns tal, stå vid glashavet, med Guds harpor i sina händer.
3 Nao wakaimba wimbo wa Mose, mtumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema: “Bwana Mungu Mwenyezi, matendo yako ni makuu na ya ajabu. Njia zako wewe ni za haki na za kweli, Mfalme wa nyakati zote!
Och de sjöngo Moses', Guds tjänares, sång och Lammets sång: de sjöngo: »Stora och underbara äro dina verk, Herre Gud, du Allsmäktige; rättfärdiga och rätta äro dina vägar, du folkens konung.
4 Ni nani ambaye hatakuogopa wewe Bwana na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako ndiwe mtakatifu. Mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako, kwa kuwa matendo yako ya haki yamedhihirishwa.”
Vem skulle icke frukta dig, Herre, och prisa ditt namn? Du allena är helig, och alla folk skola komma och tillbedja inför dig. Ty dina domar hava blivit uppenbara.»
5 Baada ya haya nikatazama, nalo hekalu, la hema la Ushuhuda, lilikuwa limefunguliwa mbinguni.
Sedan såg jag att vittnesbördets tabernakels tempel i himmelen öppnades.
6 Ndani ya lile hekalu wakatoka malaika saba wakiwa na mapigo saba. Walikuwa wamevaa nguo safi za kitani ingʼaayo na kufungwa mikanda ya dhahabu vifuani mwao.
Och de sju änglarna med de sju plågorna kommo ut ur templet, klädda i rent, skinande linne, och omgjordade kring bröstet med gyllene bälten.
7 Ndipo mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai akawapa wale malaika saba mabakuli saba ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, yeye aishiye milele na milele. (aiōn g165)
Och ett av de fyra väsendena gav de sju änglarna sju gyllene skålar, fulla av Guds vrede, hans som lever i evigheternas evigheter. (aiōn g165)
8 Nalo lile hekalu lilijawa na moshi uliotokana na utukufu wa Mungu na uweza wake, wala hakuna yeyote aliyeweza kuingia mle hekaluni mpaka yale mapigo saba ya wale malaika saba yalipomalizika.
Och templet blev uppfyllt av rök från Guds härlighet och från hans makt, och ingen kunde gå in i templet, förrän de sju änglarnas sju plågor hade fått sin fullbordan.

< Ufunuo 15 >