< Ufunuo 15 >

1 Ndipo nikaona ishara nyingine kubwa ya ajabu mbinguni: malaika saba wenye yale mapigo saba ya mwisho, kwa sababu kwa mapigo hayo ghadhabu ya Mungu ilikuwa imekamilika.
אחר כך ראיתי בשמים חזיון מסתורי נוסף: שבעה מלאכים נושאים שבע מגפות. אלה הן המכות האחרונות, כי יחד איתן בא הקץ לזעמו של אלוהים.
2 Nikaona kile kilichoonekana kama bahari ya kioo iliyochanganyikana na moto. Kando ya hiyo bahari, walikuwa wamesimama wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake pamoja na tarakimu ya jina lake. Mikononi mwao walikuwa wameshika vinubi walivyopewa na Mungu.
ראיתי מולי מעין ים זכוכית ואש, ועליו עומדים כל אלה שהתגברו על החיה הרעה, על פסלה, על סימן החותם שלה ועל מספרה. כולם החזיקו בידיהם את כינורות האלוהים,
3 Nao wakaimba wimbo wa Mose, mtumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema: “Bwana Mungu Mwenyezi, matendo yako ni makuu na ya ajabu. Njia zako wewe ni za haki na za kweli, Mfalme wa nyakati zote!
ושרו את שירת משה עבד אלוהים ואת שירת השה:”גדולים ונפלאים מעשיך, ה׳ אלוהי צבאות. צדק ואמת דרכיך, ה׳ מלך הגויים. מי לא ירא מפניך, ה׳? ומי לא ייתן כבוד לשמך? כי אתה לבדך קדוש. כל העמים יבואו וישתחוו לפניך, כי נגלו מעשיך הצודקים.“
4 Ni nani ambaye hatakuogopa wewe Bwana na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako ndiwe mtakatifu. Mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako, kwa kuwa matendo yako ya haki yamedhihirishwa.”
5 Baada ya haya nikatazama, nalo hekalu, la hema la Ushuhuda, lilikuwa limefunguliwa mbinguni.
אחרי כן ראיתי את קודש הקודשים בהיכל השמים נפתח לרווחה,
6 Ndani ya lile hekalu wakatoka malaika saba wakiwa na mapigo saba. Walikuwa wamevaa nguo safi za kitani ingʼaayo na kufungwa mikanda ya dhahabu vifuani mwao.
ומתוכו יצאו שבעת המלאכים שנשאו את שבע המכות. הם לבשו גלימות לבנות, צחורות וטהורות, ועל החזה חגרו חגורות זהב.
7 Ndipo mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai akawapa wale malaika saba mabakuli saba ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, yeye aishiye milele na milele. (aiōn g165)
אחת מארבע החיות הגישה לכל אחד מהשבעה קערת זהב מלאה בזעם האלוהים החי לנצח. (aiōn g165)
8 Nalo lile hekalu lilijawa na moshi uliotokana na utukufu wa Mungu na uweza wake, wala hakuna yeyote aliyeweza kuingia mle hekaluni mpaka yale mapigo saba ya wale malaika saba yalipomalizika.
ההיכל נמלא עשן מגבורתו של אלוהים ומכבודו, ואיש לא יכול היה להיכנס לתוכו עד שסיימו שבעת המלאכים להכות את הארץ בשבע המגפות.

< Ufunuo 15 >