< Ufunuo 15 >

1 Ndipo nikaona ishara nyingine kubwa ya ajabu mbinguni: malaika saba wenye yale mapigo saba ya mwisho, kwa sababu kwa mapigo hayo ghadhabu ya Mungu ilikuwa imekamilika.
And I saw another great and wonderful sign in heaven; seven angels, who had the seven last plagues; because in them the wrath of God was to be completed.
2 Nikaona kile kilichoonekana kama bahari ya kioo iliyochanganyikana na moto. Kando ya hiyo bahari, walikuwa wamesimama wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake pamoja na tarakimu ya jina lake. Mikononi mwao walikuwa wameshika vinubi walivyopewa na Mungu.
And I saw, as it were, a sea of glass mingled with fire; and those who overcame the beast, and its image, and its mark, and the number of its name; standing by the sea of glass, having the harps of God.
3 Nao wakaimba wimbo wa Mose, mtumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema: “Bwana Mungu Mwenyezi, matendo yako ni makuu na ya ajabu. Njia zako wewe ni za haki na za kweli, Mfalme wa nyakati zote!
And they sang the song of Moses, the servant of God, and the song of the Lamb; saying, Great and wonderful are thy works, O Lord God Almighty; righteous and true are thy ways, O King of Saints.
4 Ni nani ambaye hatakuogopa wewe Bwana na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako ndiwe mtakatifu. Mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako, kwa kuwa matendo yako ya haki yamedhihirishwa.”
Who should not fear thee, O Lord, and glorify thy name? for thou alone art perfect. Surely all nations shall come and worship before thee, because thy righteous judgments are made manifest.
5 Baada ya haya nikatazama, nalo hekalu, la hema la Ushuhuda, lilikuwa limefunguliwa mbinguni.
And after this I saw, and the temple of the tabernacle of the testimony was opened in heaven;
6 Ndani ya lile hekalu wakatoka malaika saba wakiwa na mapigo saba. Walikuwa wamevaa nguo safi za kitani ingʼaayo na kufungwa mikanda ya dhahabu vifuani mwao.
and the seven angels who had the seven plagues, came out of the temple, clothed with pure shining linen garments; and were girded round the breasts with golden girdles.
7 Ndipo mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai akawapa wale malaika saba mabakuli saba ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, yeye aishiye milele na milele. (aiōn g165)
And one of the four living creatures gave to the seven angels, seven golden vials, full of the wrath of God, who lives for ever and ever. (aiōn g165)
8 Nalo lile hekalu lilijawa na moshi uliotokana na utukufu wa Mungu na uweza wake, wala hakuna yeyote aliyeweza kuingia mle hekaluni mpaka yale mapigo saba ya wale malaika saba yalipomalizika.
And the temple was full of smoke from the glory of God, and from his power. And no one could enter into the temple till the seven plagues of the seven angels were finished.

< Ufunuo 15 >