< Ufunuo 15 >
1 Ndipo nikaona ishara nyingine kubwa ya ajabu mbinguni: malaika saba wenye yale mapigo saba ya mwisho, kwa sababu kwa mapigo hayo ghadhabu ya Mungu ilikuwa imekamilika.
And I saw another sign in heaven, great and wonderful: seven angels having the seven last plagues. For in them is filled up the wrath of God.
2 Nikaona kile kilichoonekana kama bahari ya kioo iliyochanganyikana na moto. Kando ya hiyo bahari, walikuwa wamesimama wale watu waliomshinda yule mnyama na sanamu yake pamoja na tarakimu ya jina lake. Mikononi mwao walikuwa wameshika vinubi walivyopewa na Mungu.
And I saw as it were a sea of glass mingled with fire, and them that had overcome the beast, and his image, and the number of his name, standing on the sea of glass, having the harps of God:
3 Nao wakaimba wimbo wa Mose, mtumishi wa Mungu, na wimbo wa Mwana-Kondoo, wakisema: “Bwana Mungu Mwenyezi, matendo yako ni makuu na ya ajabu. Njia zako wewe ni za haki na za kweli, Mfalme wa nyakati zote!
And singing the canticle of Moses, the servant of God, and the canticle of the Lamb, saying: Great and wonderful are thy works, O Lord God Almighty; just and true are thy ways, O King of ages.
4 Ni nani ambaye hatakuogopa wewe Bwana na kulitukuza jina lako? Kwa kuwa wewe peke yako ndiwe mtakatifu. Mataifa yote yatakuja na kuabudu mbele zako, kwa kuwa matendo yako ya haki yamedhihirishwa.”
Who shall not fear thee, O Lord, and magnify thy name? For thou only art holy: for all nations shall come, and shall adore in thy sight, because thy judgments are manifest.
5 Baada ya haya nikatazama, nalo hekalu, la hema la Ushuhuda, lilikuwa limefunguliwa mbinguni.
And after these things I looked; and behold, the temple of the tabernacle of the testimony in heaven was opened:
6 Ndani ya lile hekalu wakatoka malaika saba wakiwa na mapigo saba. Walikuwa wamevaa nguo safi za kitani ingʼaayo na kufungwa mikanda ya dhahabu vifuani mwao.
And the seven angels came out of the temple, having the seven plagues, clothed with clean and white linen, and girt about the breasts with golden girdles.
7 Ndipo mmoja wa wale viumbe wanne wenye uhai akawapa wale malaika saba mabakuli saba ya dhahabu yaliyojaa ghadhabu ya Mungu, yeye aishiye milele na milele. (aiōn )
And one of the four living creatures gave to the seven angels seven golden vials, full of the wrath of God, who liveth for ever and ever. (aiōn )
8 Nalo lile hekalu lilijawa na moshi uliotokana na utukufu wa Mungu na uweza wake, wala hakuna yeyote aliyeweza kuingia mle hekaluni mpaka yale mapigo saba ya wale malaika saba yalipomalizika.
And the temple was filled with smoke from the majesty of God, and from his power; and no man was able to enter into the temple, till the seven plagues of the seven angels were fulfilled.