< Ufunuo 14 >

1 Kisha nikatazama na hapo mbele yangu alikuwepo Mwana-Kondoo, akiwa amesimama juu ya Mlima Sayuni. Pamoja naye walikuwa wale 144,000 wenye Jina la Mwana-Kondoo na Jina la Baba yake likiwa limeandikwa kwenye vipaji vya nyuso zao.
I looked and saw the Lamb standing on Mount Zion. With him were 144,000 who had his name and his Father's name written on their foreheads.
2 Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni kama sauti ya maji mengi yaendayo kwa kasi na sauti kama ngurumo ya radi. Sauti hiyo niliyoisikia ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi wakipiga vinubi vyao.
I heard a voice from heaven sounding like a roar of many waters and loud thunder. The sound I heard was also like harpists playing their harps.
3 Nao wakaimba wimbo mpya mbele ya hicho kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe wanne wenye uhai na wale wazee. Hakuna mtu yeyote aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao 144,000 waliokuwa wamekombolewa kutoka duniani.
They sang a new song before the throne and before the four living creatures and the elders. No one could learn the song except for the 144,000 who had been bought from the earth.
4 Hawa ndio wale ambao hawakujitia unajisi kwa wanawake, kwa kuwa wao ni bikira. Wao humfuata Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamekombolewa kutoka miongoni mwa wanadamu wakawa malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.
These are the ones that have not defiled themselves with women, for they have kept themselves sexually pure. It is these who follow the Lamb wherever he goes. These were bought out of mankind as firstfruits for God and for the Lamb.
5 Vinywani mwao hapakuonekana uongo, wala hawakuwa na hatia yoyote.
No lie was found in their mouth; they are blameless.
6 Kisha nikamwona malaika mwingine akiruka juu angani, naye alikuwa na Injili ya milele ya kuwatangazia wale waishio duniani, yaani, kwa kila taifa, kabila, lugha na jamaa. (aiōnios g166)
I saw another angel flying in midair, who had the eternal message of good news to proclaim to those who live on the earth—to every nation, tribe, language, and people. (aiōnios g166)
7 Akasema kwa sauti kubwa, “Mcheni Mungu na kumpa utukufu, kwa maana saa ya hukumu yake imewadia. Mwabuduni yeye aliyeziumba mbingu, dunia, bahari na chemchemi za maji.”
He called out with a loud voice, “Fear God and give him glory. For the hour of his judgment has come. Worship him, the one who made the heaven, the earth, the sea, and the springs of water.”
8 Malaika wa pili akafuata akisema, “Umeanguka! Umeanguka Babeli Mkuu, ule uliyafanya mataifa yote kulewa kwa mvinyo wa ghadhabu ya uasherati wake.”
Another angel—a second angel—followed, saying, “Fallen, fallen is Babylon the great, who persuaded all the nations to drink the wine of her immoral passion.”
9 Malaika wa tatu akawafuata hao wawili akisema kwa sauti kubwa, “Kama mtu yeyote anamwabudu huyo mnyama na sanamu yake na kutiwa chapa yake kwenye kipaji chake cha uso au kwenye mkono wake,
Another angel—a third angel—followed them, saying with a loud voice, “If anyone worships the beast and his image, and receives a mark on his forehead or on his hand,
10 yeye pia atakunywa mvinyo wa hasira kali ya Mungu ambayo imemiminwa katika kikombe cha ghadhabu yake pasipo kuchanganywa na maji. Naye atateswa kwa moto uwakao na kiberiti mbele ya malaika watakatifu na mbele za Mwana-Kondoo.
he will also drink some of the wine of God's wrath, the wine that has been poured undiluted into the cup of his anger. The person who drinks it will be tormented with fire and sulfur before God's holy angels and before the Lamb.
11 Nao moshi wa mateso yao hupanda juu milele na milele. Hakuna mapumziko, mchana wala usiku, kwa wale wamwabuduo huyo mnyama na sanamu yake, au kwa yeyote anayepokea chapa ya jina lake.” (aiōn g165)
The smoke from their torment goes up forever and ever, and they have no rest day or night—these worshipers of the beast and his image, and everyone who receives the mark of his name. (aiōn g165)
12 Hapa ndipo penye wito wa subira na uvumilivu wa watakatifu; wale wanaozishika amri za Mungu na kudumu katika uaminifu kwa Yesu.
Here is a call for the patient endurance of the saints, those who obey the commandments of God and faith in Jesus.”
13 Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika: Wamebarikiwa wafu wafao katika Bwana tangu sasa.” “Naam,” asema Roho, “watapumzika kutoka taabu zao, kwa kuwa matendo yao yatawafuata.”
I heard a voice from heaven say, “Write this: Blessed are the dead who die in the Lord.” “Yes,” says the Spirit, “so that they may rest from their labors, for their deeds will follow them.”
14 Nikatazama, hapo mbele yangu palikuwa na wingu jeupe, na aliyekuwa ameketi juu ya hilo wingu alikuwa “kama Mwana wa Adamu” mwenye taji ya dhahabu kichwani mwake na mundu mkali mkononi mwake.
I looked, and there was a white cloud. Seated on the cloud was one like a son of man. He had a golden crown on his head and a sharp sickle in his hand.
15 Kisha malaika mwingine akaja kutoka hekaluni naye akamwita kwa sauti kubwa yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akasema, “Chukua mundu wako ukavune kwa kuwa wakati wa mavuno umewadia, kwa maana mavuno ya dunia yamekomaa.”
Then another angel came out of the temple and called with a loud voice to the one sitting on the cloud: “Take your sickle and start to reap. For the time to reap has come, since the harvest of the earth is ripe.”
16 Hivyo yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akauzungusha mundu wake duniani, nayo dunia ikavunwa.
Then the one who was sitting on the cloud swung his sickle over the earth, and the earth was harvested.
17 Malaika mwingine akatoka katika hekalu lililoko mbinguni, naye pia alikuwa na mundu mkali.
Another angel came out from the temple in heaven; he also had a sharp sickle.
18 Kisha malaika mwingine, aliyekuwa na mamlaka juu ya moto, akatoka kwenye madhabahu, naye akamwita yule malaika mwenye mundu mkali kwa sauti kubwa, akisema, “Chukua mundu wako mkali ukakusanye vichala vya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva.”
Still another angel came out from the incense altar, who had authority over the fire. He called out with a loud voice to the one who had the sharp sickle, “Take your sharp sickle and gather in the clusters of grapes from the vines of the earth, for their grapes are now ripe.”
19 Hivyo yule malaika akauzungusha mundu wake duniani na kukusanya zabibu za dunia na kuzitupa kwenye shinikizo kubwa la ghadhabu ya Mungu.
The angel swung his sickle to the earth and gathered the grape harvest of the earth. He threw it into the great wine vat of God's wrath.
20 Lile shinikizo likakanyagwa nje ya mji, nayo damu ikatiririka kama mafuriko kutoka hilo shinikizo kufikia kimo cha hatamu za farasi, kwa umbali wa maili 200.
The winepress was stomped outside the city, and blood poured out from it up to the height of a horse's bridle, for 1,600 stadia.

< Ufunuo 14 >