< Ufunuo 14 >

1 Kisha nikatazama na hapo mbele yangu alikuwepo Mwana-Kondoo, akiwa amesimama juu ya Mlima Sayuni. Pamoja naye walikuwa wale 144,000 wenye Jina la Mwana-Kondoo na Jina la Baba yake likiwa limeandikwa kwenye vipaji vya nyuso zao.
And I loked and loo a lambe stode on the mount Syon and with him C. and xliiii. thousande havynge his fathers name written in their forhedes.
2 Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni kama sauti ya maji mengi yaendayo kwa kasi na sauti kama ngurumo ya radi. Sauti hiyo niliyoisikia ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi wakipiga vinubi vyao.
And I herde a voyce from heven as the sounde of many waters and as the voyce of a gret thoundre And I herde the voyce of harpers harpynge with their harpes.
3 Nao wakaimba wimbo mpya mbele ya hicho kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe wanne wenye uhai na wale wazee. Hakuna mtu yeyote aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao 144,000 waliokuwa wamekombolewa kutoka duniani.
And they songe as it were a newe songe before the seate and before the foure beestes and the elders and no man coulde learne that songe but the hondred and xliiii. M. which were redemed from the erth.
4 Hawa ndio wale ambao hawakujitia unajisi kwa wanawake, kwa kuwa wao ni bikira. Wao humfuata Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamekombolewa kutoka miongoni mwa wanadamu wakawa malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.
These are they which were not defyled with wemen for they are virgyns. These folowe the lambe whither soever he goeth. These were redemed from men beynge the fyrste frutes vnto God and to the lambe
5 Vinywani mwao hapakuonekana uongo, wala hawakuwa na hatia yoyote.
and in their mouthes was foude no gyle. For they are with oute spott before the trone of god.
6 Kisha nikamwona malaika mwingine akiruka juu angani, naye alikuwa na Injili ya milele ya kuwatangazia wale waishio duniani, yaani, kwa kila taifa, kabila, lugha na jamaa. (aiōnios g166)
And I sawe an angell flye in the myddes of heven havynge an everlastynge gospell to preache vnto them that sytt and dwell on the erth and to all nacions kinreddes and tonges and people (aiōnios g166)
7 Akasema kwa sauti kubwa, “Mcheni Mungu na kumpa utukufu, kwa maana saa ya hukumu yake imewadia. Mwabuduni yeye aliyeziumba mbingu, dunia, bahari na chemchemi za maji.”
sayinge with a lowde voyce: Feare God and geve honour to him for the houre of his iudgement is come: and worshyppe him that made heven and erth and the see and fountaynes of water.
8 Malaika wa pili akafuata akisema, “Umeanguka! Umeanguka Babeli Mkuu, ule uliyafanya mataifa yote kulewa kwa mvinyo wa ghadhabu ya uasherati wake.”
And there folowed another angell sayinge: Babilon is fallen is fallen that gret cite for she made all nacions drynke of the wyne of hyr fornicacion.
9 Malaika wa tatu akawafuata hao wawili akisema kwa sauti kubwa, “Kama mtu yeyote anamwabudu huyo mnyama na sanamu yake na kutiwa chapa yake kwenye kipaji chake cha uso au kwenye mkono wake,
And the thyrde angell folowed them sayinge with aloude voyce: Yf eny man worshippe the beest and his ymage and receave hie marke in his forhed or on his honde
10 yeye pia atakunywa mvinyo wa hasira kali ya Mungu ambayo imemiminwa katika kikombe cha ghadhabu yake pasipo kuchanganywa na maji. Naye atateswa kwa moto uwakao na kiberiti mbele ya malaika watakatifu na mbele za Mwana-Kondoo.
the same shall drynke of the wyne of the wrath of God which is powred in the cuppe of his wrath. And he shalbe punnysshed in fyre and brymstone before the holy Angels and before the lambe.
11 Nao moshi wa mateso yao hupanda juu milele na milele. Hakuna mapumziko, mchana wala usiku, kwa wale wamwabuduo huyo mnyama na sanamu yake, au kwa yeyote anayepokea chapa ya jina lake.” (aiōn g165)
And the smoke of their turment ascendeth vp evermore. And they have no rest daye ner nyght which worshippe ye beast and his ymage and whosoever receaveth the prynt of his name. (aiōn g165)
12 Hapa ndipo penye wito wa subira na uvumilivu wa watakatifu; wale wanaozishika amri za Mungu na kudumu katika uaminifu kwa Yesu.
Here is the pacience of saynctes. Heare are they that kepe the commaundmentes and the fayth of Iesu.
13 Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika: Wamebarikiwa wafu wafao katika Bwana tangu sasa.” “Naam,” asema Roho, “watapumzika kutoka taabu zao, kwa kuwa matendo yao yatawafuata.”
And I herde a voyce from heven sayinge vnto me: wryte. Blessed are the deed which here after dye in the lorde even soo sayth the sprete: that they maye rest fro their laboures but their workes shall folowe them.
14 Nikatazama, hapo mbele yangu palikuwa na wingu jeupe, na aliyekuwa ameketi juu ya hilo wingu alikuwa “kama Mwana wa Adamu” mwenye taji ya dhahabu kichwani mwake na mundu mkali mkononi mwake.
And I loked and beholde a whyte clowde and apon the clowde one syttynge lyke vnto the sonne of man havynge on his heed a golde crowne and in his honde a sharpe sykle.
15 Kisha malaika mwingine akaja kutoka hekaluni naye akamwita kwa sauti kubwa yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akasema, “Chukua mundu wako ukavune kwa kuwa wakati wa mavuno umewadia, kwa maana mavuno ya dunia yamekomaa.”
And another angell came oute of the temple cryinge with a lowde voyce to him that sate on the clowde. Thruste in thy sycle and repe: for the tyme is come to repe for the corne of the erth is rype.
16 Hivyo yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akauzungusha mundu wake duniani, nayo dunia ikavunwa.
And he that sate on the clowde thrust in his sykle on the erth and the erth was reped.
17 Malaika mwingine akatoka katika hekalu lililoko mbinguni, naye pia alikuwa na mundu mkali.
And another angell came oute of the temple which is in heven havynge also a sharpe sycle.
18 Kisha malaika mwingine, aliyekuwa na mamlaka juu ya moto, akatoka kwenye madhabahu, naye akamwita yule malaika mwenye mundu mkali kwa sauti kubwa, akisema, “Chukua mundu wako mkali ukakusanye vichala vya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva.”
And another angell came oute from yt aultre which had power over fyre and cryed with a lowde crye to him that had the sharpe sykle and sayde: thrust in thy sharpe sykle and gaddre the clusters of the erth for her grapes are rype.
19 Hivyo yule malaika akauzungusha mundu wake duniani na kukusanya zabibu za dunia na kuzitupa kwenye shinikizo kubwa la ghadhabu ya Mungu.
And the angell thrust in his sykle on the erth and cut doune the grapes of the vyneyarde of the erth: and cast them into the gret wynefat of the wrath of god
20 Lile shinikizo likakanyagwa nje ya mji, nayo damu ikatiririka kama mafuriko kutoka hilo shinikizo kufikia kimo cha hatamu za farasi, kwa umbali wa maili 200.
and the wynefat was trodden with out the cite and bloud came oute of the fat eve vnto the hors brydles by the space of a thowsande and. vi. C. furlonges.

< Ufunuo 14 >