< Ufunuo 14 >

1 Kisha nikatazama na hapo mbele yangu alikuwepo Mwana-Kondoo, akiwa amesimama juu ya Mlima Sayuni. Pamoja naye walikuwa wale 144,000 wenye Jina la Mwana-Kondoo na Jina la Baba yake likiwa limeandikwa kwenye vipaji vya nyuso zao.
Tedy pohleděl jsem, a aj, Beránek stál na hoře Sion, a s ním sto čtyřidceti a čtyři tisíců majících jméno Otce jeho napsané na čelích svých.
2 Nami nikasikia sauti kutoka mbinguni kama sauti ya maji mengi yaendayo kwa kasi na sauti kama ngurumo ya radi. Sauti hiyo niliyoisikia ilikuwa kama sauti ya wapiga vinubi wakipiga vinubi vyao.
A slyšel jsem hlas s nebe, jako hlas vod mnohých, a jako hlas hromu velikého. A hlas slyšel jsem, jako těch, kteříž hrají na harfy své.
3 Nao wakaimba wimbo mpya mbele ya hicho kiti cha enzi na mbele ya wale viumbe wanne wenye uhai na wale wazee. Hakuna mtu yeyote aliyeweza kujifunza wimbo huo isipokuwa hao 144,000 waliokuwa wamekombolewa kutoka duniani.
A zpívali jakožto píseň novou, před trůnem, a před čtyřmi zvířaty, a před starci, a žádný nemohl se naučiti té písni, jediné těch sto čtyřidceti a čtyři tisíce, kteříž jsou koupeni z země.
4 Hawa ndio wale ambao hawakujitia unajisi kwa wanawake, kwa kuwa wao ni bikira. Wao humfuata Mwana-Kondoo kila aendako. Hawa wamekombolewa kutoka miongoni mwa wanadamu wakawa malimbuko kwa Mungu na kwa Mwana-Kondoo.
Totoť jsou ti, kteříž s ženami nejsou poskvrněni; nebo panicové jsou. Tiť jsou, jenž následují Beránka, kamž by koli šel; tiť jsou koupeni ze všech lidí, prvotiny Bohu a Beránkovi.
5 Vinywani mwao hapakuonekana uongo, wala hawakuwa na hatia yoyote.
A v ústech jejich není nalezena lest; neboť jsou bez úhony před trůnem Božím.
6 Kisha nikamwona malaika mwingine akiruka juu angani, naye alikuwa na Injili ya milele ya kuwatangazia wale waishio duniani, yaani, kwa kila taifa, kabila, lugha na jamaa. (aiōnios g166)
I viděl jsem jiného anděla letícího po prostředku nebe, majícího evangelium věčné, aby je zvěstoval těm, jenž bydlí na zemi, a všelikému národu, i pokolení, i jazyku, i lidu, (aiōnios g166)
7 Akasema kwa sauti kubwa, “Mcheni Mungu na kumpa utukufu, kwa maana saa ya hukumu yake imewadia. Mwabuduni yeye aliyeziumba mbingu, dunia, bahari na chemchemi za maji.”
Řkoucího velikým hlasem: Bojte se Boha, a vzdejte jemu chválu, neboť přišla hodina soudu jeho; a klanějte se tomu, kterýž učinil nebe i zemi i moře i studnice vod.
8 Malaika wa pili akafuata akisema, “Umeanguka! Umeanguka Babeli Mkuu, ule uliyafanya mataifa yote kulewa kwa mvinyo wa ghadhabu ya uasherati wake.”
A jiný anděl letěl za ním, řka: Padl, padl Babylon, město to veliké, nebo vínem hněvu smilství svého napájelo všecky národy.
9 Malaika wa tatu akawafuata hao wawili akisema kwa sauti kubwa, “Kama mtu yeyote anamwabudu huyo mnyama na sanamu yake na kutiwa chapa yake kwenye kipaji chake cha uso au kwenye mkono wake,
A třetí anděl letěl za nimi, pravě velikým hlasem: Bude-li se kdo klaněti šelmě a obrazu jejímu, a vezme-li znamení její na čelo své aneb na ruku svou,
10 yeye pia atakunywa mvinyo wa hasira kali ya Mungu ambayo imemiminwa katika kikombe cha ghadhabu yake pasipo kuchanganywa na maji. Naye atateswa kwa moto uwakao na kiberiti mbele ya malaika watakatifu na mbele za Mwana-Kondoo.
I tenť také bude píti víno hněvu Božího, víno, pravím, kteréž jest vlito do kalichu hněvu jeho; a trápen bude ohněm a sirou před obličejem andělů svatých a před obličejem Beránka.
11 Nao moshi wa mateso yao hupanda juu milele na milele. Hakuna mapumziko, mchana wala usiku, kwa wale wamwabuduo huyo mnyama na sanamu yake, au kwa yeyote anayepokea chapa ya jina lake.” (aiōn g165)
A dým muk jejich vstoupíť na věky věků, a nebudouť míti odpočinutí dnem i nocí ti, kteříž se klanějí šelmě a obrazu jejímu, a jestliže kdo přijme znamení jména jejího. (aiōn g165)
12 Hapa ndipo penye wito wa subira na uvumilivu wa watakatifu; wale wanaozishika amri za Mungu na kudumu katika uaminifu kwa Yesu.
Tuť jest trpělivost svatých, tu jsou ti, kteříž ostříhají přikázání Božích a víry Ježíšovy
13 Kisha nikasikia sauti kutoka mbinguni ikisema, “Andika: Wamebarikiwa wafu wafao katika Bwana tangu sasa.” “Naam,” asema Roho, “watapumzika kutoka taabu zao, kwa kuwa matendo yao yatawafuata.”
I slyšel jsem hlas s nebe, řkoucí ke mně: Piš: Blahoslavení jsou od této chvíle mrtví, kteříž v Pánu umírají. Duch zajisté dí jim, aby odpočinuli od prací svých, nebo skutkové jejich následují jich.
14 Nikatazama, hapo mbele yangu palikuwa na wingu jeupe, na aliyekuwa ameketi juu ya hilo wingu alikuwa “kama Mwana wa Adamu” mwenye taji ya dhahabu kichwani mwake na mundu mkali mkononi mwake.
I pohleděl jsem, a aj, oblak bělostkvoucí, a na tom oblaku seděl podobný Synu člověka, maje na hlavě své korunu zlatou a v ruce své srp ostrý.
15 Kisha malaika mwingine akaja kutoka hekaluni naye akamwita kwa sauti kubwa yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akasema, “Chukua mundu wako ukavune kwa kuwa wakati wa mavuno umewadia, kwa maana mavuno ya dunia yamekomaa.”
A jiný anděl vyšel z chrámu, volaje hlasem velikým na toho, kterýž seděl na oblaku: Pusť srp svůj a žni; nebť jest přišla tobě hodina žni, nebo již dozrala žeň země.
16 Hivyo yule aliyekuwa ameketi juu ya lile wingu akauzungusha mundu wake duniani, nayo dunia ikavunwa.
I spustil ten, kterýž seděl na oblaku, srp svůj na zem, a požata jest země.
17 Malaika mwingine akatoka katika hekalu lililoko mbinguni, naye pia alikuwa na mundu mkali.
A jiný anděl vyšel z chrámu toho, kterýž jest na nebi, maje i on srp ostrý.
18 Kisha malaika mwingine, aliyekuwa na mamlaka juu ya moto, akatoka kwenye madhabahu, naye akamwita yule malaika mwenye mundu mkali kwa sauti kubwa, akisema, “Chukua mundu wako mkali ukakusanye vichala vya mizabibu ya dunia, maana zabibu zake zimeiva.”
Opět vyšel jiný anděl z oltáře, kterýž měl moc nad ohněm, a volal křikem velikým na toho, jenž měl srp ostrý, řka: Pusť srp svůj ostrý, a zbeř hrozny vinice zemské; neboť jsou uzrali hroznové její.
19 Hivyo yule malaika akauzungusha mundu wake duniani na kukusanya zabibu za dunia na kuzitupa kwenye shinikizo kubwa la ghadhabu ya Mungu.
I spustil anděl srp svůj na zemi, a sebral vinici země, a vmetal hrozny do jezera velikého hněvu Božího.
20 Lile shinikizo likakanyagwa nje ya mji, nayo damu ikatiririka kama mafuriko kutoka hilo shinikizo kufikia kimo cha hatamu za farasi, kwa umbali wa maili 200.
I tlačeno jest jezero před městem, a vyšla krev z jezera až do udidl koňům za tisíc a za šest set honů.

< Ufunuo 14 >