< Ufunuo 13 >
1 Yule joka akajikita katika mchanga ulioko ufuoni mwa bahari. Nami nikamwona mnyama akitoka ndani ya bahari. Mnyama huyo alikuwa na pembe kumi na vichwa saba, akiwa na taji kumi kwenye hizo pembe zake, na juu ya kila kichwa kulikuwa na jina la kukufuru.
The dragon stood on the ocean shore. I saw a beast that was coming up out of the ocean. It had ten horns and seven heads. On each [of] its horns there was a royal crown. On [each] of its heads there was a name that insulted [God].
2 Mnyama yule niliyemwona alifanana na chui, lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kichwa chake kama cha simba. Lile joka likampa huyo mnyama nguvu zake, kiti chake cha enzi na mamlaka makubwa.
The beast that I saw was like a leopard. But its feet were like the feet of a bear, and its mouth was like the mouth of a lion. The dragon gave the beast [power]. From his own throne he also gave it authority [to rule people] [DOU].
3 Kimojawapo ya vichwa vya huyo mnyama kilikuwa kama kilichokwisha kupata jeraha la mauti, lakini jeraha hilo la mauti likapona. Ulimwengu wote ukashangaa ukamfuata huyo mnyama.
One of the heads of the beast had been wounded {[The Lord] had wounded one of the heads of the beast}, causing the beast to almost die. But its wound was healed. [As a result, nearly] all [the people of] the earth [HYP, MTY] marveled at the beast and became his disciples.
4 Watu wakaliabudu lile joka kwa sababu lilikuwa limempa huyo mnyama mamlaka yake, pia wakamwabudu huyo mnyama na kuuliza, “Ni nani aliye kama huyu mnyama? Ni nani awezaye kupigana vita naye?”
They worshipped the dragon, because he had given to the beast authority [to rule people]. They also worshipped the beast, saying, “No one is [as powerful] as the beast!/ [RHQ] (No one would dare to fight against it!/Who would dare to fight against it?)” [RHQ]
5 Huyo mnyama akapewa kusema maneno ya kiburi na kukufuru na kutumia mamlaka yake kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
The beast was allowed {[God] allowed the beast} to speak [MTY] in a boastful way and to insult [God]. [It was also] allowed {[God] also allowed it} to rule [over people] for 42 months.
6 Akafungua kinywa chake ili kumkufuru Mungu, akilitukana Jina lake na mahali aishipo na wale wakaao mbinguni.
It [MTY] insulted God, insulted the place where he lives, and insulted everyone who lives with him in heaven.
7 Pia akaruhusiwa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda. Akapewa uwezo juu ya watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa.
[It was] allowed {[God] allowed it} to fight against God’s people and to conquer them. [It was] allowed {[God] allowed it} to have authority [to rule] over every tribe, over every people-[group], over [speakers of] every language [MTY], and over every nation.
8 Nao watu wote waishio duniani watamwabudu huyo mnyama, yaani, wale wote ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
Most of [HYP] the [people] living on earth worshipped it. They were people whose names were not written in a book by the [one who is like a] lamb, the one who had been killed. Since the beginning of the world [he wrote in it the names of the people who] will have [eternal] life.
9 Yeye aliye na sikio na asikie.
Everyone who wants to understand [MTY] must listen carefully to [this message from God]:
10 Ikiwa mtu ni wa kuchukuliwa mateka, atachukuliwa mateka. Ikiwa mtu ni wa kuuawa kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hapa ndipo penye wito wa subira na imani ya watakatifu.
If [God has determined] that some people will be captured by their [enemies], they will be captured. If [God has determined that] some people will be killed with a sword, they will be killed with a sword. So God’s people [must be] steadfast, and remain faithful [to him].
11 Kisha nikamwona mnyama mwingine, akipanda juu kutoka dunia. Alikuwa na pembe mbili kama mwana-kondoo, lakini akanena kama joka.
I saw another beast, which was coming up from the earth. It had two small horns [on its head] like a sheep has. But it spoke [things to deceive people], like the dragon does.
12 Akatumia mamlaka yote ya yule mnyama wa kwanza kwa niaba yake, naye akawafanya wote wakaao duniani kumwabudu yule mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona.
While the first beast watched, it used all the [same] authority [to rule people that the first beast had]. It forced the people who live on the earth [MTY, DOU] to worship the first beast, that is, the one who was healed of the wound that had caused it to almost die.
13 Naye akafanya ishara kuu na za ajabu, hata kusababisha moto kushuka toka mbinguni kuja duniani watu wakiona waziwazi.
The second beast performed awesome miracles, even causing fire from the sky to fall to earth while people watched.
14 Kwa sababu ya zile ishara alizokuwa amepewa uwezo wa kuzifanya kwa niaba ya yule mnyama wa kwanza, akawadanganya wakaao duniani. Akawaamuru wasimamishe sanamu kwa heshima ya yule mnyama aliyekuwa amejeruhiwa kwa upanga lakini akaishi.
He performed miracles (on behalf of/with the authority of) the [first] beast. By doing that he deceived the [unbelieving] people on the earth so that they [believed that they should worship the first beast. But this happened only because God] allowed [it to happen]. The second beast told the people living on earth to make an image of the [first] beast, the one that [people] had almost killed with a sword and that then came back to life again.
15 Akapewa uwezo wa kuipa pumzi ile sanamu ya yule mnyama wa kwanza, ili iweze kusema na kuwasababisha wale wote waliokataa kuiabudu hiyo sanamu kuuawa.
The image of the [first] beast was allowed to breathe, in order that it might speak and in order that [it might command that] whoever refused to worship its image should be killed {that [people] should kill whoever refused to worship its image}.
16 Pia alimlazimisha kila mmoja, mdogo na mkubwa, tajiri na maskini, mtu huru na mtumwa, atiwe chapa kwenye mkono wake wa kuume au kwenye kipaji chake cha uso,
[The second beast] required also that [the first beast’s name] be marked {[its agents] mark [the first beast’s name]} on the right hand or on the forehead of everyone, those of little [social importance] and of great [social importance], the rich and the poor, free [people] and slaves. [Everyone]!
17 ili kwamba mtu yeyote asiweze kununua wala kuuza isipokuwa amekuwa na hiyo chapa, ambayo ni jina la huyo mnyama au tarakimu za jina lake.
They did this in order that people could not buy [anything] or sell [anything] if they did not have the mark, which represents the name of the beast or the number of its name, [on their foreheads].
18 Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na ufahamu na ahesabu tarakimu za huyo mnyama, kwa maana ni tarakimu za kibinadamu. Tarakimu zake ni 666.
You must [think] wisely to understand [the meaning of the mark]. Anyone who thinks wisely should calculate from the number of the beast what the man’s name is. That number is 666.