< Ufunuo 13 >

1 Yule joka akajikita katika mchanga ulioko ufuoni mwa bahari. Nami nikamwona mnyama akitoka ndani ya bahari. Mnyama huyo alikuwa na pembe kumi na vichwa saba, akiwa na taji kumi kwenye hizo pembe zake, na juu ya kila kichwa kulikuwa na jina la kukufuru.
And I stood upon the sand of the sea. And I saw a beast coming up out of the sea, having ten horns and seven heads, and upon his horns ten diadems, and upon his heads names of blasphemy.
2 Mnyama yule niliyemwona alifanana na chui, lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kichwa chake kama cha simba. Lile joka likampa huyo mnyama nguvu zake, kiti chake cha enzi na mamlaka makubwa.
And the beast which I saw was like a leopard, and his feet were as the feet of a bear, and his mouth as the mouth of a lion. And the dragon gave him his power, and his throne, and great authority.
3 Kimojawapo ya vichwa vya huyo mnyama kilikuwa kama kilichokwisha kupata jeraha la mauti, lakini jeraha hilo la mauti likapona. Ulimwengu wote ukashangaa ukamfuata huyo mnyama.
And I saw one of his heads as it were wounded to death; and his deadly wound was healed. And the whole earth wondered after the beast.
4 Watu wakaliabudu lile joka kwa sababu lilikuwa limempa huyo mnyama mamlaka yake, pia wakamwabudu huyo mnyama na kuuliza, “Ni nani aliye kama huyu mnyama? Ni nani awezaye kupigana vita naye?”
And they worshipped the dragon, because he gave the authority to the beast; and they worshipped the beast, saying, Who is like to the beast, and who is able to make war with him?
5 Huyo mnyama akapewa kusema maneno ya kiburi na kukufuru na kutumia mamlaka yake kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
And there was given to him a mouth speaking great things and blasphemy; and power was given to him to work forty-two months.
6 Akafungua kinywa chake ili kumkufuru Mungu, akilitukana Jina lake na mahali aishipo na wale wakaao mbinguni.
And he opened his mouth in blasphemies against God, to blaspheme his name, and his tabernacle, and those who dwell in heaven.
7 Pia akaruhusiwa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda. Akapewa uwezo juu ya watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa.
And it was given to him to make war with the saints, and to overcome them; and power was given him over every tribe, and people, and tongue, and nation.
8 Nao watu wote waishio duniani watamwabudu huyo mnyama, yaani, wale wote ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
And all who dwell on the earth wilt worship him, every one whose name hath not been written in the book of life of the Lamb that was slain from the foundation of the world.
9 Yeye aliye na sikio na asikie.
If any one hath an ear, let him hear.
10 Ikiwa mtu ni wa kuchukuliwa mateka, atachukuliwa mateka. Ikiwa mtu ni wa kuuawa kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hapa ndipo penye wito wa subira na imani ya watakatifu.
If any one [[leadeth]] into captivity he shall go into captivity; if any one shall kill with the sword, he must be killed with the sword. Here is the endurance and the faith of the saints.
11 Kisha nikamwona mnyama mwingine, akipanda juu kutoka dunia. Alikuwa na pembe mbili kama mwana-kondoo, lakini akanena kama joka.
And I saw another beast coming up out of the earth; and he had two horns like a lamb, and he spoke as a dragon.
12 Akatumia mamlaka yote ya yule mnyama wa kwanza kwa niaba yake, naye akawafanya wote wakaao duniani kumwabudu yule mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona.
And he exerciseth all the authority of the first beast in his presence; and causeth the earth and those who dwell therein to worship the first beast, whose deadly wound was healed.
13 Naye akafanya ishara kuu na za ajabu, hata kusababisha moto kushuka toka mbinguni kuja duniani watu wakiona waziwazi.
And he doeth great signs, so that he even causeth fire to come down from heaven on the earth, in the sight of men.
14 Kwa sababu ya zile ishara alizokuwa amepewa uwezo wa kuzifanya kwa niaba ya yule mnyama wa kwanza, akawadanganya wakaao duniani. Akawaamuru wasimamishe sanamu kwa heshima ya yule mnyama aliyekuwa amejeruhiwa kwa upanga lakini akaishi.
And he deceiveth them that dwell on the earth, by reason of the signs which it was given him to do in the presence of the beast; commanding those who dwell on the earth to make an image to the beast which had the wound by a sword, and lived.
15 Akapewa uwezo wa kuipa pumzi ile sanamu ya yule mnyama wa kwanza, ili iweze kusema na kuwasababisha wale wote waliokataa kuiabudu hiyo sanamu kuuawa.
And it was given to him to give breath to the image of the beast, that the image of the beast should even speak, and cause that all who did not worship the image of the beast should be killed.
16 Pia alimlazimisha kila mmoja, mdogo na mkubwa, tajiri na maskini, mtu huru na mtumwa, atiwe chapa kwenye mkono wake wa kuume au kwenye kipaji chake cha uso,
And he causeth all, the small and the great, and the rich and the poor, and the flee and the bond, to receive a mark on their right hand, or on their forehead;
17 ili kwamba mtu yeyote asiweze kununua wala kuuza isipokuwa amekuwa na hiyo chapa, ambayo ni jina la huyo mnyama au tarakimu za jina lake.
and that no one shall be able to buy or sell, except him that hath the mark, the name of the beast, or the number of his name.
18 Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na ufahamu na ahesabu tarakimu za huyo mnyama, kwa maana ni tarakimu za kibinadamu. Tarakimu zake ni 666.
Here is wisdom. Let him that hath understanding count the number of the beast; for it is the number of a man, and his number is six hundred and sixty-six.

< Ufunuo 13 >