< Ufunuo 13 >
1 Yule joka akajikita katika mchanga ulioko ufuoni mwa bahari. Nami nikamwona mnyama akitoka ndani ya bahari. Mnyama huyo alikuwa na pembe kumi na vichwa saba, akiwa na taji kumi kwenye hizo pembe zake, na juu ya kila kichwa kulikuwa na jina la kukufuru.
And I stood upon the sand of the sea. And I saw a beast rising up out of the sea, having ten horns and seven heads; and upon his horns ten diadems, and upon his heads names of blasphemy.
2 Mnyama yule niliyemwona alifanana na chui, lakini miguu yake ilikuwa kama ya dubu na kichwa chake kama cha simba. Lile joka likampa huyo mnyama nguvu zake, kiti chake cha enzi na mamlaka makubwa.
And the beast which I saw was like a leopard, and his feet were as the feet of a bear, and his mouth like the mouth of lions: and the dragon gave him his power, and his throne, and great authority.
3 Kimojawapo ya vichwa vya huyo mnyama kilikuwa kama kilichokwisha kupata jeraha la mauti, lakini jeraha hilo la mauti likapona. Ulimwengu wote ukashangaa ukamfuata huyo mnyama.
And I saw one of his heads as it had been smitten unto death; and the wound of his death was healed. And the whole earth wondered after the beast:
4 Watu wakaliabudu lile joka kwa sababu lilikuwa limempa huyo mnyama mamlaka yake, pia wakamwabudu huyo mnyama na kuuliza, “Ni nani aliye kama huyu mnyama? Ni nani awezaye kupigana vita naye?”
and they worshiped the dragon, because he gave authority to the beast; and they worshiped the beast, saying; Who is like the beast? and who is able to make war with him?
5 Huyo mnyama akapewa kusema maneno ya kiburi na kukufuru na kutumia mamlaka yake kwa muda wa miezi arobaini na miwili.
and a mouth was given to him speaking great things and blasphemies; and authority was given unto him to prevail forty-two months.
6 Akafungua kinywa chake ili kumkufuru Mungu, akilitukana Jina lake na mahali aishipo na wale wakaao mbinguni.
And he opened his mouth in blasphemies against God, to blaspheme his name, and his tabernacle, those dwelling in the heaven.
7 Pia akaruhusiwa kufanya vita na watakatifu na kuwashinda. Akapewa uwezo juu ya watu wa kila kabila, jamaa, lugha na taifa.
And it was given to him to make war with the saints and to conquer them: and authority was given unto him over every tribe, and people, and tongue, and nation.
8 Nao watu wote waishio duniani watamwabudu huyo mnyama, yaani, wale wote ambao majina yao hayakuandikwa kwenye kitabu cha uzima cha Mwana-Kondoo aliyechinjwa tangu kuumbwa kwa ulimwengu.
And all those who dwell upon the earth, whose name has not been written in the book of life of the Lamb that was slain from the foundation of the world, will worship him.
9 Yeye aliye na sikio na asikie.
if any one has ears, let him hear.
10 Ikiwa mtu ni wa kuchukuliwa mateka, atachukuliwa mateka. Ikiwa mtu ni wa kuuawa kwa upanga, atauawa kwa upanga. Hapa ndipo penye wito wa subira na imani ya watakatifu.
If any one leads into captivity he goes into captivity: if any one kills with a sword, it behooves him to be killed with a sword. Here is the patience and the faith of the saints.
11 Kisha nikamwona mnyama mwingine, akipanda juu kutoka dunia. Alikuwa na pembe mbili kama mwana-kondoo, lakini akanena kama joka.
And I saw another beast coming up out of the earth; and he had two horns like a lamb, and he continued to speak as the dragon.
12 Akatumia mamlaka yote ya yule mnyama wa kwanza kwa niaba yake, naye akawafanya wote wakaao duniani kumwabudu yule mnyama wa kwanza, ambaye jeraha lake la mauti lilipona.
And he exercises all the authority of the first beast before him. And he makes the earth and those dwelling in it, that they shall worship the first beast, whose wound of his death was healed.
13 Naye akafanya ishara kuu na za ajabu, hata kusababisha moto kushuka toka mbinguni kuja duniani watu wakiona waziwazi.
And he performs great signs, so that he can indeed make fire descend out of the heaven to the earth in presence of the people.
14 Kwa sababu ya zile ishara alizokuwa amepewa uwezo wa kuzifanya kwa niaba ya yule mnyama wa kwanza, akawadanganya wakaao duniani. Akawaamuru wasimamishe sanamu kwa heshima ya yule mnyama aliyekuwa amejeruhiwa kwa upanga lakini akaishi.
And he deceives those dwelling upon the earth through the signs which it was given unto him to perform in the presence of the beast, saying to those dwelling on the earth, that they should make an image to the beast, who had the wound of the sword, and did live.
15 Akapewa uwezo wa kuipa pumzi ile sanamu ya yule mnyama wa kwanza, ili iweze kusema na kuwasababisha wale wote waliokataa kuiabudu hiyo sanamu kuuawa.
And it was given unto him to give spirit to the image of the beast, in order that the image of the beast may indeed speak, and he may cause so many as will not worship the image of the beast that they should be killed.
16 Pia alimlazimisha kila mmoja, mdogo na mkubwa, tajiri na maskini, mtu huru na mtumwa, atiwe chapa kwenye mkono wake wa kuume au kwenye kipaji chake cha uso,
And he causes all, small and great, both rich and poor, both free and bond, that they may give them a mark on their right hand, or on their forehead:
17 ili kwamba mtu yeyote asiweze kununua wala kuuza isipokuwa amekuwa na hiyo chapa, ambayo ni jina la huyo mnyama au tarakimu za jina lake.
that no one may be able to buy or sell, except the one having the mark, the name of the beast, or the number of his name.
18 Hapa ndipo penye hekima. Yeye aliye na ufahamu na ahesabu tarakimu za huyo mnyama, kwa maana ni tarakimu za kibinadamu. Tarakimu zake ni 666.
Here is wisdom. Let the one having understanding count the number of the beast: for it is the number of a man. And his is, Six hundred and sixty-six.